Radical-1
New Member
- May 31, 2023
- 2
- 4
Hili jambo nimekuwa nikijiuliza na sijawahi kupata ufumbuzi..
Naombeni msaada wadau.
Ni kosa kisheria kuvua, kusafirisha na kuuza sangara (Nile Perch) wa ziwa Victoria wenye urefu chini ya sentimita 50.
Hii nimeitoa kwenye kanuni za uvuvi 2009.
KINACHONITATIZA NI HIKI HAPA:
Wavuvi wanatakiwa wafanye nini ili wasiwakamate Sangara hao kwenye nyavu zao?
Kwa mfano wavuvi wa dagaa ziwa Victoria hutumia taa(mwanga) kuvua. Na Sangara hufuata mwanga ili kula hao dagaa waliokusanyika kwenye taa za wavuvi.
Pindi wavuvi watakapotumia nyavu halali (mm 10) kwajili ya uvuvi wa dagaa hujipatia pia Sangara wa size tofauti tofauti.
Wakati mwingine hadi Sangara wenye 3cm yaani vitoto kabisa.
Je wawafanye nini hao Sangara wakijinchnganya kwenye nyavu za dagaa?
Ukisema wawarudishe ziwani Sangara hao wachanga hakuna mvuvi atakuelewa kwasababu uvuvi wao unahitaji kufanyika haraka haraka, basi wanapata wapi muda wa kuchambua watoto wa Sangara wawarudishe ndani ya maji?
(Nazungumza haya yote kwasababu nimewahi kuvua dagaa kwa muda zaidi ya miezi 9 mwaka 2023)
Na kawaida tulikuwa hatuwachambui sangara waliochini ya cm 50 ili kuwarudisha majini.
Na hata kama ukisema ufanye hivyo, utakuwa haujasaidia kitu, maana Sangara ni wachovu sana kuliko samaki kama Kambare..
Kitendo cha kumbwaga Sangara kwenye mtumbwi, kisha umrudishe majini tena kuna uwezekano mdogo wa kuendelea kuishi kama awali
Na kwa kuwa wavuvi hawatupi Sangara waliozuiliwa kuvuliwa je wafanya biashara huku nchi kavu wafanye nini?
Nimetembea sehemu nyingi Mkoan Mwanza ambazo wavuvi wa dagaa huuza dagaa wao pamoja na Sangara waliojichanganya kwenye nyavu za dagaa, lakini sijaona watu wa mamlaka yoyote wakiwazuia wavuvi hao kwa kuja nchi kavu na watoto wa sangara.
Sasa kama wavuvi hawazuiliwi kuleta watoto wa Sangara nchi kavu, kwanini wanunuzi na wasafirishaji wazuiliwe kuuza ama kusafirisha?
Na je kama Watanzania wazalendo tuwafanye nini Sangara wachanga ambao wameshafika nchi kavu ama sokoni au nyumbani, au wapo mezani tayari kwa kuliwa
Naombeni msaada wadau.
Ni kosa kisheria kuvua, kusafirisha na kuuza sangara (Nile Perch) wa ziwa Victoria wenye urefu chini ya sentimita 50.
Hii nimeitoa kwenye kanuni za uvuvi 2009.
KINACHONITATIZA NI HIKI HAPA:
Wavuvi wanatakiwa wafanye nini ili wasiwakamate Sangara hao kwenye nyavu zao?
Kwa mfano wavuvi wa dagaa ziwa Victoria hutumia taa(mwanga) kuvua. Na Sangara hufuata mwanga ili kula hao dagaa waliokusanyika kwenye taa za wavuvi.
Pindi wavuvi watakapotumia nyavu halali (mm 10) kwajili ya uvuvi wa dagaa hujipatia pia Sangara wa size tofauti tofauti.
Wakati mwingine hadi Sangara wenye 3cm yaani vitoto kabisa.
Je wawafanye nini hao Sangara wakijinchnganya kwenye nyavu za dagaa?
Ukisema wawarudishe ziwani Sangara hao wachanga hakuna mvuvi atakuelewa kwasababu uvuvi wao unahitaji kufanyika haraka haraka, basi wanapata wapi muda wa kuchambua watoto wa Sangara wawarudishe ndani ya maji?
(Nazungumza haya yote kwasababu nimewahi kuvua dagaa kwa muda zaidi ya miezi 9 mwaka 2023)
Na kawaida tulikuwa hatuwachambui sangara waliochini ya cm 50 ili kuwarudisha majini.
Na hata kama ukisema ufanye hivyo, utakuwa haujasaidia kitu, maana Sangara ni wachovu sana kuliko samaki kama Kambare..
Kitendo cha kumbwaga Sangara kwenye mtumbwi, kisha umrudishe majini tena kuna uwezekano mdogo wa kuendelea kuishi kama awali
Na kwa kuwa wavuvi hawatupi Sangara waliozuiliwa kuvuliwa je wafanya biashara huku nchi kavu wafanye nini?
Nimetembea sehemu nyingi Mkoan Mwanza ambazo wavuvi wa dagaa huuza dagaa wao pamoja na Sangara waliojichanganya kwenye nyavu za dagaa, lakini sijaona watu wa mamlaka yoyote wakiwazuia wavuvi hao kwa kuja nchi kavu na watoto wa sangara.
Sasa kama wavuvi hawazuiliwi kuleta watoto wa Sangara nchi kavu, kwanini wanunuzi na wasafirishaji wazuiliwe kuuza ama kusafirisha?
Na je kama Watanzania wazalendo tuwafanye nini Sangara wachanga ambao wameshafika nchi kavu ama sokoni au nyumbani, au wapo mezani tayari kwa kuliwa