AdvocateMtetezi
Member
- Sep 26, 2015
- 10
- 11
Kupita mkutano wa UVCCM unaofanyika muda huu hapo Mwembe Yanga, Mwenyekiti wa UVCCM Taifa Sadifa Juma amesisika akisema kupitia televisheni ya Star TV kuwa "Lowassa anatokwa na mikojo barabarani" hii ni kauli yenye lengo la kuvunja amani ya nchi.
Ikumbukwe kuwa Lowassa anayeambiwa na UVCCM kuwa anatokwa na mikojo barabarani ni baba wa familia, ni babu wa wajukuu na zaidi ya yote ni kiongozi wa nchi hii aliitumikia nchi hii akiwa waziri mkuu (2005-2008), pia ni Mgombea Urais wa CHADEMA na UKAWA chama na umoja ambao una mashabiki na wapenzi wengi ambao wasingeweza kuvumilia kuona kiongozi wao anatukanwa hadharani na UVCCM.
Sadifa Juma na UVCCM ni mchochezi na wanavunja amani ya nchi hii wakiwa ni sehemu ya chama tawala CCM, hii inamaanisha kuwa CCM imemtuma Sadifa kumtukana Lowassa na ni dhahiri kuwa CCM ndio chama kinachoanzisha vurugu na uvunjifu wa amani.
Wakati Sadifa Juma wa UVCCM anamtukana Lowassa uwanja anaotumia umejaa askari ambao hawakuonekana kumchukulia hatua za kumkamata kwa kutoa lugha za uchochezi, matusi na udhalilishaji hadharani.
CCM inaimba wimbo wa amani lakini inavunja amani kwa matamshi yake yenyewe. CCM inaimba kama malaika na inacheza kama mashetani. CCM ni waongo sana, wanajifanya Kuimba amani kila kona ya nchi wakati huo huo wanavunja amani kwa kumtukana Lowassa hadharani. Shirika moja lililofanya utafiti limebaini Lowassa ameshatukanwa na CCM mara 121 katika majukwaa mbalimbali ya kampeni.
Mimi kama AdvocateMtetezi nalishauri "jeshi la policy", wamchukulie hatua Sadifa Juma mwenyekiti wa UVCCM kwa kumtukana Lowassa hadharani kuepusha vijana wa UKAWA na vijana wanaompenda Lowassa nchini kujibu mapigo. Nawashauri pia vijana wa UKAWA endapo "jeshi la policy" halitachukua hatua dhidi ya UVCCM na Sadifa Juma basi wao pia wajibu mapigo kwa namna watakavyoona wao inafaa, kama alivyofanya mwenzao Sadifa Juma akitumia jukwaa la UVCCM na kurushwa live na kituo cha Star TV.
Ikumbukwe kuwa Lowassa anayeambiwa na UVCCM kuwa anatokwa na mikojo barabarani ni baba wa familia, ni babu wa wajukuu na zaidi ya yote ni kiongozi wa nchi hii aliitumikia nchi hii akiwa waziri mkuu (2005-2008), pia ni Mgombea Urais wa CHADEMA na UKAWA chama na umoja ambao una mashabiki na wapenzi wengi ambao wasingeweza kuvumilia kuona kiongozi wao anatukanwa hadharani na UVCCM.
Sadifa Juma na UVCCM ni mchochezi na wanavunja amani ya nchi hii wakiwa ni sehemu ya chama tawala CCM, hii inamaanisha kuwa CCM imemtuma Sadifa kumtukana Lowassa na ni dhahiri kuwa CCM ndio chama kinachoanzisha vurugu na uvunjifu wa amani.
Wakati Sadifa Juma wa UVCCM anamtukana Lowassa uwanja anaotumia umejaa askari ambao hawakuonekana kumchukulia hatua za kumkamata kwa kutoa lugha za uchochezi, matusi na udhalilishaji hadharani.
CCM inaimba wimbo wa amani lakini inavunja amani kwa matamshi yake yenyewe. CCM inaimba kama malaika na inacheza kama mashetani. CCM ni waongo sana, wanajifanya Kuimba amani kila kona ya nchi wakati huo huo wanavunja amani kwa kumtukana Lowassa hadharani. Shirika moja lililofanya utafiti limebaini Lowassa ameshatukanwa na CCM mara 121 katika majukwaa mbalimbali ya kampeni.
Mimi kama AdvocateMtetezi nalishauri "jeshi la policy", wamchukulie hatua Sadifa Juma mwenyekiti wa UVCCM kwa kumtukana Lowassa hadharani kuepusha vijana wa UKAWA na vijana wanaompenda Lowassa nchini kujibu mapigo. Nawashauri pia vijana wa UKAWA endapo "jeshi la policy" halitachukua hatua dhidi ya UVCCM na Sadifa Juma basi wao pia wajibu mapigo kwa namna watakavyoona wao inafaa, kama alivyofanya mwenzao Sadifa Juma akitumia jukwaa la UVCCM na kurushwa live na kituo cha Star TV.