Wont be the same
JF-Expert Member
- Aug 15, 2024
- 1,564
- 2,483
MWENYEKITI wa Umoja wa Vijana UVCCM wilaya ya Moshi (Moshi Vijijini ) Yuvenal Shirima ameeleza kuwa katika Wilaya ya hiyo hakuna Kijana yoyote anaesema "No Election" na kwamba wote wanaunga mkono uchaguzi kufanyika.
Ameeleza hayo Jumamosi Mei 17, 2025 wakati wa fainali za mashindano ya mpira wa Miguu ya YUVE CUP LEAGUE 2025 iliyofanyika katika Kata ya Kilema Kati Wilaya ya Moshi.
Amesema "Vijana wanaunga Mkono Serikali yetu kwasababu inafanya kazi kubwa na tutaendelea kushirikiana na Serikali yetu kuhakikisha kwamba tunakuwa na ulinzi mzuri, tutakwenda kufanya uchaguzi kwa amani na usalama".
Nae Mkuu wa Wilaya ya Moshi Godfrey Mnzava amesema kuwa "Kuna watu wanapita huko wanahamasisha makundi mbalimbali hasa ya vijana kugomea uchaguzi, wanahitaji vurugu tu, Kwanza kwa Serikali tulivyojipanga hawatafanikiwa kwa namna yoyote".
Ameeleza hayo Jumamosi Mei 17, 2025 wakati wa fainali za mashindano ya mpira wa Miguu ya YUVE CUP LEAGUE 2025 iliyofanyika katika Kata ya Kilema Kati Wilaya ya Moshi.
Amesema "Vijana wanaunga Mkono Serikali yetu kwasababu inafanya kazi kubwa na tutaendelea kushirikiana na Serikali yetu kuhakikisha kwamba tunakuwa na ulinzi mzuri, tutakwenda kufanya uchaguzi kwa amani na usalama".
Nae Mkuu wa Wilaya ya Moshi Godfrey Mnzava amesema kuwa "Kuna watu wanapita huko wanahamasisha makundi mbalimbali hasa ya vijana kugomea uchaguzi, wanahitaji vurugu tu, Kwanza kwa Serikali tulivyojipanga hawatafanikiwa kwa namna yoyote".