Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,501
- 9,280
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, George Simbachawene amesema serikali itaangalia namna ya kubadilisha Sheria ya Jumuiya ili kuwe na utaratibu wa utoaji wa huduma za kiroho, hasa kutokana na kuwapo kwa utitiri wa vibanda imani.
Simbachawene aliyabainisha hayo alipozungumza na waandishi wa habari kuhusu ajali iliyotokea Moshi, ambako watu 20 wamepoteza maisha na wengine 16 kujeruhiwa. Kati ya hao watoto ni wanne na 16 ni watu wazima.
Alisema pamoja na kongamano hilo kuwa na kibali cha siku tatu, kuanzia Januari 30 hadi Februari Mosi mwaka huu, kilichoombwa na Mchungaji wa Kanisa la Calvary Assemblies of God, Elia Mwambapa, lakini wanaonesha walikiuka masharti ya kibali ambacho ni kongamano kuendelea baada ya saa 12 jioni.
Simbachawene ambaye alitoa pole kutokana na tukio hilo, alisema ili kuepukana na madhara makubwa zaidi siku zijazo, wizara yake itaangalia namna ya kuifanyika marekebisho ya Sheria ya Jumuiya ambayo ndiyo inayotumika kusajili taasisi za dini.
“Serikali inaheshimu haki ya kuabudu na ni haki ya kikatiba, lakini lazima tuangalie pengine hata sheria na kanuni zetu haziko sawa sawa, kwa sababu wengine wanakuja na sabuni ukiogea matatizo yameisha na utakuwa na tajiri.
Mwingine atakuja na maji, mafuta au maziwa, na wakati mwingine ukisikiliza mahubiri unaweza kujiuliza kuna Mungu kweli hapa,” alisema Simbachawene aliyeshika wadhifa huo hivi karibuni.
Aliongeza, “tunaona ni vizuri watu tukaweka utaratibu wa utoaji wa huduma za kiroho, vibanda imani vimekuwa vingi lazima kuweka utaratibu.
Mfano Rwanda ukitaka kuanzisha huduma lazima uwe na shahada ya kwanza ya Theolojia, sisi hajutaweka hilo sharti, ila tutaanza kufikiria huko.”
Simbachawene aliyabainisha hayo alipozungumza na waandishi wa habari kuhusu ajali iliyotokea Moshi, ambako watu 20 wamepoteza maisha na wengine 16 kujeruhiwa. Kati ya hao watoto ni wanne na 16 ni watu wazima.
Alisema pamoja na kongamano hilo kuwa na kibali cha siku tatu, kuanzia Januari 30 hadi Februari Mosi mwaka huu, kilichoombwa na Mchungaji wa Kanisa la Calvary Assemblies of God, Elia Mwambapa, lakini wanaonesha walikiuka masharti ya kibali ambacho ni kongamano kuendelea baada ya saa 12 jioni.
Simbachawene ambaye alitoa pole kutokana na tukio hilo, alisema ili kuepukana na madhara makubwa zaidi siku zijazo, wizara yake itaangalia namna ya kuifanyika marekebisho ya Sheria ya Jumuiya ambayo ndiyo inayotumika kusajili taasisi za dini.
“Serikali inaheshimu haki ya kuabudu na ni haki ya kikatiba, lakini lazima tuangalie pengine hata sheria na kanuni zetu haziko sawa sawa, kwa sababu wengine wanakuja na sabuni ukiogea matatizo yameisha na utakuwa na tajiri.
Mwingine atakuja na maji, mafuta au maziwa, na wakati mwingine ukisikiliza mahubiri unaweza kujiuliza kuna Mungu kweli hapa,” alisema Simbachawene aliyeshika wadhifa huo hivi karibuni.
Aliongeza, “tunaona ni vizuri watu tukaweka utaratibu wa utoaji wa huduma za kiroho, vibanda imani vimekuwa vingi lazima kuweka utaratibu.
Mfano Rwanda ukitaka kuanzisha huduma lazima uwe na shahada ya kwanza ya Theolojia, sisi hajutaweka hilo sharti, ila tutaanza kufikiria huko.”