Serikali isiingilie dini au imani za madhehebu na manabii wa kizazi kipya wanaozuka kwa kasi

Yoda

JF-Expert Member
Jul 22, 2018
37,661
46,349
Kumekuwepo na matamanio ya watu wengi serikali kufanya udhibiti wa baadhi ya imani za kidini hasa za baadhi ya madhehebu ya Kikristo ambayo yamekuwa yakizuka kwa kasi miaka ya hivi karibuni.

Kwanza, lazima tufahamu uhuru wa kidini katika nchi hii upo katika katiba, kutaka kuuingiliwa uhuru huo kwa sababu ya kutozipenda baadhi ya imani au madhehebu ni kuhalalisha uvunjaji katiba.

Pili, Serikali haina uwezo wa kutambua dini ya kweli ni ipi, haina uwezo wa kujua nabii au mtume wa kweli ni yupi na pi aina uwezo wa kufahamu tafsiri sahihi ya maandiko yoyote. Kufanya uingiliaji wowote kwa manabii, mitume, walimu na imani zilizozuka kwa kasi itakuwa pasipo na vigezo vyovyote/"arbitrary".

Tatu, Serikali hapaswi kuingilia uhuru wa dini yoyote kwa namna yoyote ile, ni mfano/precedent/slippery slope mbaya sana kuelekea kukandamiza uhuru mwingine wa raia serikali inapokuwa na mkono mrefu katika masuala dini na imani.

Mwisho, Kinachotakiwa ni Serikali kuweka mazingira bora sana ya elimu kama Ulaya kuhakikisha raia wake wanapata elimu bora na wengi wanaweza kufanya tafakuri sahihi za logic kisha hao raia wataachana wenyewe tu na utapeli wa kidini au superstitions.
 
Ok. Ila kwa mtazamo wangu mimi serikali ingefuta tu hizi dini mana hazina faida yoyote zaidi ya kuleta chuki, utengano, unafiki na kuongeza ujinga katika jamii. Tembelea thread yoyote humu uone chuki zilizopo baina ya hizi dini.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mijadala sio chuki, watu wasioweza kuvumulia maoni ya wengine ndio hufikiri kupingwa au kukoselewa ni chuki
 
Kwani hamna taasisi kubwa zinazodeal na dini yenu? inakuwaje mtu anatoka huko nje anakuja tu hapa kufungua kanisa...

Hivi mfano ishu ya imani watu wanapanga kuleta mzaha na kuharibu watu.....

Haya mambo yapewa TEC kusimamia hizi ishu ,kuna kanisa moja niliona wamevaa uchi kabisa kama bar eti wanaita hakuna kuhukumu mtu😅😅
 
Kumekuwepo na matamanio ya watu wengi serikali kufanya udhibiti wa baadhi ya imani za kidini hasa za baadhi ya madhehebu ya Kikristo ambayo yamekuwa yakizuka kwa kasi miaka ya hivi karibuni.

Kwanza, lazima tufahamu uhuru wa kidini katika nchi hii upo katika katiba, kutaka kuuingiliwa uhuru huo kwa sababu ya kutozipenda baadhi ya imani au madhehebu ni kuhalalisha uvunjaji katiba.

Pili, Serikali haina uwezo wa kutambua dini ya kweli ni ipi, haina uwezo wa kujua nabii au mtume wa kweli ni yupi na pi aina uwezo wa kufahamu tafsiri sahihi ya maandiko yoyote. Kufanya uingiliaji wowote kwa manabii, mitume, walimu na imani zilizozuka kwa kasi itakuwa pasipo na vigezo vyovyote/"arbitrary".

Tatu, Serikali hapaswi kuingilia uhuru wa dini yoyote kwa namna yoyote ile, ni mfano/precedent/slippery slope mbaya sana kuelekea kukandamiza uhuru mwingine wa raia serikali inapokuwa na mkono mrefu katika masuala dini na imani.

Mwisho, Kinachotakiwa ni Serikali kuweka mazingira bora sana ya elimu kama Ulaya kuhakikisha raia wake wanapata elimu bora na wengi wanaweza kufanya tafakuri sahihi za logic kisha hao raia wataachana wenyewe tu na utapeli wa kidini au superstitions.
Hapo mwisho hapo ndo umeharibu,,,unasema itoe elimu kama ulaya,,,,watu wa ulaya wameelimika mpaka elimu imewasaidia wamejua kuwa kufirana ni jambo la msingi kwa akina baba na ukipinga maswala yakufirana unaingia matatizoni,,,,hao jamaa wa ulaya usije watolea mfano hawanaga maana kabisa
 
Hapo mwisho hapo ndo umeharibu,,,unasema itoe elimu kama ulaya,,,,watu wa ulaya wameelimika mpaka elimu imewasaidia wamejua kuwa kufirana ni jambo la msingi kwa akina baba na ukipinga maswala yakufirana unaingia matatizoni,,,,hao jamaa wa ulaya usije watolea mfano hawanaga maana kabisa
Watu wamekuwa wakifirana tangu karne za kale, Kufirana hakujaanzia Ulaya.
 
Kwani hamna taasisi kubwa zinazodeal na dini yenu? inakuwaje mtu anatoka huko nje anakuja tu hapa kufungua kanisa...

Hivi mfano ishu ya imani watu wanapanga kuleta mzaha na kuharibu watu.....

Haya mambo yapewa TEC kusimamia hizi ishu ,kuna kanisa moja niliona wamevaa uchi kabisa kama bar eti wanaita hakuna kuhukumu mtu
Sio kila watu wanataka kuwa chini ya TEC au BAKWATA au kupewa muongozo nao.
 
Sio kila watu wanataka kuwa chini ya TEC au BAKWATA au kupewa muongozo nao.
Sasa serikali itafanya nn? Wakisema theology hawaitambui !? Kigezo cha theology ni wakatoliko ,je wao wakisema hawapo chini ya ukatoliki.

Na kanisa ni lazima lisajaliwa kwa maana hiyo lazima liwe chini ya taasisi husika ipate kibali kwa taasisi ya kikristo (dhehebu) halafu wapate na cha serikali.

Serikali haina vigezo ila qualifications za kupate cheti lazima viwe chini ya taasisi ya kikristo ndio wahusika. Wakishaaprove ndio serikali inatoa kibali.

Hata ile ndoa unayopata cheti cha serikali lqzima ipitia hatua za kidini mpaka mkafungishwa kwa wakristo na waislamu.
 
Degree ya theology haibadilishi chochote katika jamii ya watu kuamini imani au dini zao.
Degree ya theology ni msingi wa Imani na mafundisho ya Dini katika Jamii kwa hio waende Shule kwanza au wawe na muajiriwa mwenye degree ya theology kwenye hayo makanisa yao ambae anahost mahubiri wao wabaki kua waandishi behind the scene sababu hawana elimu ya theology
 
Back
Top Bottom