Uteuzi wa Job Masima kuwa Balozi Israel ni ishara ya Rais Magufuli kuinoa na kuiimarisha TISS

Balozi Job Masima ameanza kazi rasmi ya kuiwakilisha Tanzania nchini Israel akiwa balozi wa kwanza nchini humo tangu Tanzania (wakati huo ikiitwa Tanganyika) ivunje uhusiano wake na taIfa hilo teule yapata miaka 43 ilopita.

Ni mmoja wa mabalozi waloapishwa jana Ikulu kabla ya kwenda kuiwakilisha Tanzania katika nchi za Ujerumani, Israel na Oman.

Kwa mara ya kwanza katika historia ya mahusiano kati ya nchi hizo mwezi October mwaka 2015 aliekuwa raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Kikwete alimkaribisha balozi wa Israel bwana Yahel Vilan alipokwenda kukabidhi hati za utambulisho tayari kuridhia mahusiano ya kimataifa kwa nchi hizi mbili.

Baada ya raisi John Magufuli kuingia madarakani mwezi January mwaka jana Balozi Vilan alimtembelea raisi Magufuli na kumhakikishia uhusiano huo kwamba upo na kusisitiza kwamba Israel itafungua ofisi ya ubalozi nchini Tanzania.

Raisi John Magufuli nae akamhakikishia balozi Vilan kwamba Tanzania ilikuwa mbioni kuhakikisha inakuwa na ubalozi mjini Tel Aviv.

Baada ya Tanzania kupata uhuru wake December 1 mwaka 1961, Tanzania ilifungua ubalozi wake nchini Israel lakini makazi yakiwa nchini Misri.

Mwaka 1973 umoja wa nchi za kiafrika uliamua kujitenga na Israel baada ya nchi hiyo kuwa inaitawala Palestina kwa kuwa na sera za kibaguzi na za kuitenga Palestina na kuizuia kuvuka ukanda wa Gaza.

Lakini pia sababu ingine ilikuwa ni khasa baada ya vita ya Yom Kippor ambapo mataifa sita ya kiarabu yakiongozwa na Misri na Syria yalikuwa yakipigana vita na Israel katika milima ya Golan na Sinai.

Kusudio ya vita hiyo ilikuwa ni kuyakomboa maeneo hayo kutoka kwa Israel ambayo iliyateka baada ya vita ilojulikana kama "six days war" ya mwaka 1967 na pia raisi wa Misri Anwar Sadat alikuwa na mpango wa kufungua mfereji wa Suez.

Pamoja na hayo uhusiano wa nchi hizi haukuwa umezimwa moja kwa moja na ilipofikia mwaka 1995 mahusiano kati ya nchi hizi yalirudishwa na Tanzania ikarejesha ubalozi wa Tanzania Israel lakini makazi yakiwa nchini Misri na Israel ikawa na ofisi ya ubalozi mjini Nairobi nchini Kenya.

Tanzania na Israel walikuwa wakishirikina katika miradi mbalimbali na mmojawapo ni mradi mkubwa wa Bugando nchini Mwanza na miradi mingine.

Mwezi Julai mwaka jana Waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu alihudhuria mkutano wa viongozi wa nchi za Afrika Mashariki ulofanyika nchini Uganda na akakabidhiwa barua rasmi na waziri wa mambo ya nje ya ushirikiano wa kimataifa na kikanda Dr Augustine Mahiga, kutoka kwa raisi John Magufuli.

Katika barua hiyo raisi Magufuli alimweleza waziri mkuu Netanyahu kwamba Tanzania ilikuwa imeamua kufungua rasmi ofisi ya ubalozi nchini Israel.


Dr Augustine Mahiga akisalimiana na Waziri mkuu wa Israel mjini Entebbe mwezi julai mwaka 2016. (Picha na Kobi Gideon wa GPO)

Israel inajulikana duniani kwa kuwa wataalam kwenye maeneo ya kilimo na umwagiliaji, Israel ina kiwanda kikubwa cha plastiki kijulikanacho kama Plazit Polygal Group ambacho kina wafanyakazi wapatao 500 na kinapata faida ya mauzio kiasi cha doka milioni 250 kwa mwaka.

Pia Israel inajulikana duniani kwa utengenezaji bidhaa mbalimbali za kiteknolojia zikiwemo satellite, silaha za kivita kama makombora na ndege zijiendeshazo zenyewe au Drones.

Lakini kikubwa zaidi ni kuhusu jeshi la Israel ambalo mpaka kufikia mwaka 2015 matumizi ya jeshi la Israel yaani "military expenditure" nchi hiyo ni ya 15 duniani huku ikiwa ni nchi ya 8 kwa uuzaji wa silaha duniani.

Lakini asilimia 20 ya bajeti ya ulinzi ya nchi hiyo inatolewa na Marekani sawa na dola bilioni 3.8 kwa mwaka baada ya kutiliana saini mkataba utakaokuwa ni wa mwaka 2018 hadi 2028.

Lakini uteuzi wa balozi Job Masima hauwezi kupita bila kuangaliwa kwa jicho la tatu kwani unaelekeza wadadisi kuona kwamba ni uteuzi wa kimkakati zaidi.

Kabla ya uteuzi wa balozi Masima, alikuwa ni katibu mkuu wizara ya Ulinzi na jeshi la kujeng taifa nafasi ambayo aliichukua mwaka 2011 alopoteuliwa na aliekuwa raisi wa serikali ya awamu ya nne Jakaya Kikwete.

Lakini balozi Job Masima ni mmoja wa watu muhimu sana katika kuimarisha ulinzi na usalama wa Tanzania, akiwa tayari amekaa sehemu mbalimbali za ulinzi na usalama, raisi Magufuli ameamua kumpa majukumu ya kuimarisha uhusiano wake na Israel lakini kukiwa na malengo maalum.

Raisi John Magufuli ametambua haja ya kuimarisha idara ya ujasusi Tanzania TISS na amekusudia kuiimarisha kiutawala na kiutendaji ambapo vijana wengi sasa wanapata nafasi za kujiendeleza zaidi na kijifunza mbinu mpya za ulinzi wa taifa khasa katika ulimwengu wa leo ambao umejaa mikikimikii ya kila aina.

Hapo ndipo unapokuja kuwaamini Israel katika masuala ya ulinzi na usalama kwani wana msemo wao ambao unasema kwa kiingereza kwamba "Security is a subject that can be taught theoretically, but nothing is a substitute for a real hands-on experience and we've got lots of it."- yaani wakimaanisha kwamba usalama ni somo ambalo laweza kufundishwa kinadharia, lakini hakuna mbadala wa mikono halisi yenye uzoefu ambayo tunayo mingi tu.

Ni dhahiri kuwa yanayojiri leo hii ni pamoja na nafasi pana ya mawasiliano kati ya maofisa, muunganiko yaani "coordination" kati ya idara na idara na uimarishaji wa "kitengo" ambacho ndicho kiko katika ngazi ya juu kabisa ya uangalizi wa taifa hili.

Bila shaka Israel inatusaidia katika nyanza mbalimbali za ulinzi na usalama, uchumi na maendeleo mengine kwa ujumla, lakini Amani na ulutivu na ustawi wa watanzania unahitaji ulinzi na usalama imara.

Ulinzi na usalama imara ndiyo nguzo ambayo inahitaji kuboreshwa kwa gharama yoyote ile na hiyo ni moja ya mipango ya serikali ya awamu ya tano.

Waweza kupata mwanga wa nini nimekusudia katika Makala hii ndogo kwa kujikumbusha Makala hizo hapo chini, lakini wenzangu wadadisi wa masuala ya ujasusi kama mkulu Yeriko Nyerere naomba michango yenu kwa kuongezea nyama kwenye hili.

Je, raisi John Magufuli anajimaarisha kiusalama zaidi au anaisuka zaidi TISS?

Je, balozi Job Masima ana cheo gani kijeshi?

Ujasusi wa Kiuchumi na Kiteknolojia unakuwa kwa kasi, Je Tanzania iko tayari

Wazee Mwang'onda na Hassy Kitine waasisi wa TISS imara Tanzania

https://www.jamiiforums.com/threads/hili-ni-jaribio-jingine-kwa-system-state-au-kitengo.896405/


Aisee safi sana kwahiyo mfumo wa kutuma na kupokea pesa kwa njia ya kieletroniki yaani TISS utaimarishwa safi sana hivi pesa ya Israel inaitwaje
 
Mkuu umeleta uzi mzuri sana, Mkuu ana nia ya dhati kabisa ya kuumarisha taasisi yetu hii ya Usalama ambayo kiuhalisia imekuwa iko operate locally sana na haitakii kubadilika kwa mwavuli tu wa kuwa utendaji wao ni secret Mheshimiwa JPM alianza kuonesha nia ya ya dhati pale tu alipo mteua Modestus kipilimbi kama GD wa idara Kumuweka tu mtu ambae ni professional wa Computer science basi kutamfanya aipelekee idara Kisasa kabisa , Mbinu za Intelligence karibia katika agency zote ni Moja tunachozidiana Ni technology leo ukiangalia M15 ya uk au FBI utaona wanapopishana ni Tech tu, Uteuzi huo wa Job masima kama Balozi utaleta matokeo chanya katika kujifunza na kupata mapya juu ya usalama Huko.
M16 not M15.
 
Awa tiss Ndo watoa kucha
Idara HII ni muhimu ila kwa nchi yetu imegeuka na kuwa idara ya WAHUNI, mbaya zaidi UHUNI wenyewe unaonekana kama vile unafurahiwa na WATAWALA..

Hadhi ya idara hii kwa nchi yetu imeshuka sana, na sidhani kama waliopo wana UWEZO wa kuihuisha.. Nafikiri wanachoweza kukifanya ni kuiboresha na kuwa ya KIHUNI ZAIDI..

Kwa sababu, wamedhihirisha kuwa ni WATAWALA wenye kupenda uhuni..
 
Idara HII ni muhimu ila kwa nchi yetu imegeuka na kuwa idara ya WAHUNI, mbaya zaidi UHUNI wenyewe unaonekana kama vile unafurahiwa na WATAWALA..

Hadhi ya idara hii kwa nchi yetu imeshuka sana, na sidhani kama waliopo wana UWEZO wa kuihuisha.. Nafikiri wanachoweza kukifanya ni kuiboresha na kuwa ya KIHUNI ZAIDI..

Kwa sababu, wamedhihirisha kuwa ni WATAWALA wenye kupenda uhuni..

Mkuu, ni vitu gani unadhani vinaifanya idara hii ionekane imegeuka kuwa idara ya WAHUNI?

Funguka mkuu.
 
Mkuu, ni vitu gani unadhani vinaifanya idara hii ionekane imegeuka kuwa idara ya WAHUNI?

Funguka mkuu.
Brother Richard, I do believe, you have a very sound thinking capacity....

Sasa hivi ni KAWAIDA kabisa, kuwaona watumishi wa idara hiyo wakitumia nafasi zao kwa mambo ya kihuni mitaani..

Mfano mwepesi, siku chache zilizopita, tumewashuhudia pale protea hotel wakifanya uhuni dhidi ya Nape..... Wameonekana kwa huyo kwa sababu tu jamaa aliyefanyiwa ana title...

Matukio mangapi kwa mfano huo yanatokea mitaani kwa wananchi wasio na majina?????

Ile TISS ya akina Mzee Mzena imeondoka na wenyewe.

Sasa hivi bila hata soni, wanajinasibu kwa nafasi zao jambo ambalo lilikuwa haliwezekani kabisa kwa kipindi kile. Wengine hata wake zao walikuwa hawajui kama wanafanya kazi hiyo.

Kwa kweli ukizingatia nature ya kazi zao, na jinsi walivyo sasa, ni uhuni mtupu.

Na nionavyo, si rahisi kuirejesha ilipokuwa kutokana na watumishi wenyewe kutojitambua au tamaa na kujikurubisha sana kwa wanasiasa, kiasi cha kuwa watumwa wa wanasiasa, hivyo kulazimika kupokea na kutii maelekezo ya kipuuzi...

NAITAMANI TISS YETU ILIYOKUWA NA WELEDI, HADHI NA HESHIMA YA HALI YA JUU, SIO TZ TU, BALI DUNIANI KOTE........ NASIKITIKA SIIONI...
 
Brother Richard, I do believe, you have a very sound thinking capacity....

Sasa hivi ni KAWAIDA kabisa, kuwaona watumishi wa idara hiyo wakitumia nafasi zao kwa mambo ya kihuni mitaani..

Mfano mwepesi, siku chache zilizopita, tumewashuhudia pale protea hotel wakifanya uhuni dhidi ya Nape..... Wameonekana kwa huyo kwa sababu tu jamaa aliyefanyiwa ana title...

Matukio mangapi kwa mfano huo yanatokea mitaani kwa wananchi wasio na majina?????

Ile TISS ya akina Mzee Mzena imeondoka na wenyewe.

Sasa hivi bila hata soni, wanajinasibu kwa nafasi zao jambo ambalo lilikuwa haliwezekani kabisa kwa kipindi kile. Wengine hata wake zao walikuwa hawajui kama wanafanya kazi hiyo.

Kwa kweli ukizingatia nature ya kazi zao, na jinsi walivyo sasa, ni uhuni mtupu.

Na nionavyo, si rahisi kuirejesha ilipokuwa kutokana na watumishi wenyewe kutojitambua au tamaa na kujikurubisha sana kwa wanasiasa, kiasi cha kuwa watumwa wa wanasiasa, hivyo kulazimika kupokea na kutii maelekezo ya kipuuzi...

NAITAMANI TISS YETU ILIYOKUWA NA WELEDI, HADHI NA HESHIMA YA HALI YA JUU, SIO TZ TU, BALI DUNIANI KOTE........ NASIKITIKA SIIONI...

My friend Gryulka, ahsante kwa appreciation yako kutokana na michango yangu.

Ni kweli kabisa baada ya mzee Mzena kuondoka basi idara imeharibika kimaadili.

Maadili mahali popote ndiyo yanajenga taasisi imara.

Tatizo ni kule juu na mfumo mzima kwamba kuna mahali palikosewa baada ya Mwalimu.

Kurudisha maadili, nidhamu na kuondoa uhuni kazi kubwa inayoikabili tiss.

Kwa mfano mdogo tu ni tukio la Clouds na baada ya hapo kinachofuatia watu wanaodaiwa kufanya kazi tiss wanaanikwa picha zao mitandanoni.

Hii haiwezi kutokea katika tiss imara.

Naungana na wewe kabisa.
 
My friend Gryulka, ahsante kwa appreciation yako kutokana na michango yangu.

Ni kweli kabisa baada ya mzee Mzena kuondoka basi idara imeharibika kimaadili.

Maadili mahali popote ndiyo yanajenga taasisi imara.

Tatizo ni kule juu na mfumo mzima kwamba kuna mahali palikosewa baada ya Mwalimu.

Kurudisha maadili, nidhamu na kuondoa uhuni kazi kubwa inayoikabili tiss.

Kwa mfao mdogo tu ni tukio la Clouds na baada ya hapo kinachofuatia watu wanaodaiwa kufanya kazi tiss wanaanikwa picha zao mitandanoni.

Hii haiwezi kutokea katika tiss imara.

Naungana na wewe kabisa.
MUNGU IBARIKI TANZANIA..
 
Mkuu, ni vitu gani unadhani vinaifanya idara hii ionekane imegeuka kuwa idara ya WAHUNI?

Funguka mkuu.


Mkuu Richard nina mfano mwingine hai wa (someone I know) kuhusiana na suala la kukiuka maadili kulikopitiliza, kwa hii idara ya kipindi hiki.
Hii ilitokea chini ya tawala za nyuma kidogo, ambapo huyu mfanyakazi wao alikuwa akizidisha kilevi mara kwa mara na wakaogopa angeweza kutoa nyaraka nyeti za Serikali.
Ingawa alikuwa mmoja wa Vichwa muhimu sana ktk Idara, na pia mkuu wa kitengo alichokuwepo, wakubwa wa wakati ule hawakusita kumsimamisha kazi "kwa manufaa ya umma"
As opposed to now ambapo kuna kila aina ya drama, na watu bado wanajidai na kazi zao na kuendelea kutisha watu.
 
Kwa mara ya kwanza katika historia ya mahusiano kati ya nchi hizo mwezi October mwaka 2015 aliekuwa raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Jakaya Kikwete alimkaribisha balozi wa Israel bwana Yahel Vilan alipokwenda kukabidhi hati za utambulisho tayari kuridhia mahusiano ya kimataifa kwa nchi hizi mbili.

Balozi wa Israel wapi?

Baada ya raisi John Magufuli kuingia madarakani mwezi January mwaka jana Balozi Vilan alimtembelea raisi Magufuli na kumhakikishia uhusiano huo kwamba upo na kusisitiza kwamba Israel itafungua ofisi ya ubalozi nchini Tanzania.


Mkuu Richards,
Hivyo vifungu viwili hapa vinahitaji uvipitie upya, binafsi naona kama vinajichanganya.
 

Mkuu Richards,
Hivyo vifungu viwili hapa vinahitaji uvipitie upya, binafsi naona kama vinajichanganya.

upload_2017-4-3_9-18-47.png

Ilikuwa ni tarehe 28 October 2015 Mkuu, raisi wa awamu ya nne Jakaya Kikwete alimkaribisha bwana Yahel Vilan.

Siku hiyo JK aliwapokea mabalozi wa kutoka nchi za Misri, Singapore, Israel na Ufilipino.

Kumbuka baada ya uchaguzi bado raisi wa awamu ya nne Kikwete alikuwa madarakani na raisi Magufuli likuwa akisubiri kuapishwa.

Baada ya raisi Magufuli kuapishwa balozi Vilan akaja tena tarehe 20 mwezi January 2016 kujitambulisha.

Soma link hii ya figganigga -https://www.jamiiforums.com/threads/rais-magufuli-akutana-na-balozi-wa-israel-nchini-ikulu-leo.1000540/page-6

Sasa nadhani utaelewa hapo.
 
Mkuu Richard nina mfano mwingine hai wa (someone I know) kuhusiana na suala la kukiuka maadili kulikopitiliza, kwa hii idara ya kipindi hiki.
Hii ilitokea chini ya tawala za nyuma kidogo, ambapo huyu mfanyakazi wao alikuwa akizidisha kilevi mara kwa mara na wakaogopa angeweza kutoa nyaraka nyeti za Serikali.
Ingawa alikuwa mmoja wa Vichwa muhimu sana ktk Idara, na pia mkuu wa kitengo alichokuwepo, wakubwa wa wakati ule hawakusita kumsimamisha kazi "kwa manufaa ya umma"
As opposed to now ambapo kuna kila aina ya drama, na watu bado wanajidai na kazi zao na kuendelea kutisha watu.

Kwa kuwa DG mpya yupo, nadhani si sehemu ya wale ambao labda kwa namna moja au ingine wameingia humo kwa bahati mbaya.

Moja ya misingi muhimu kabisa ni kuhakikisha watu hawachukuliwi kwa bahati mbaya.

Sasa kwa miaka karibu 20 kuna watu wasostahili ambao waliingia humo na hawa ni wa kuwachuja huko tuendako.
 
Ilikuwa ni tarehe 28 October 2015 Mkuu, raisi wa awamu ya nne Jakaya Kikwete alimkaribisha bwana Yahel Vilan.

Siku hiyo JK aliwapokea mabalozi wa kutoka nchi za Misri, Singapore, Israel na Ufilipino.

Kwa hiyo mpaka hapo unataka kusema tayari kulikua na ubalozi wa Isirael!
Sawa.

Baada ya raisi John Magufuli kuingia madarakani mwezi January mwaka jana Balozi Vilan alimtembelea raisi Magufuli na kumhakikishia uhusiano huo kwamba upo na kusisitiza kwamba Israel itafungua ofisi ya ubalozi nchini Tanzania.

Na hapo alipokutana na Magufuli alisema Israel itafungua ofisi ya ubalozi nchini Tanzania, ina maana huyo balozi alikuwa anawakilisha nchi yake hapa Tanzania bila ofisi?

Rudia kuyasoma maelezo yako katika bandiko lako la kwanza.katika aya mbili zinazomtaja huyo balozi na Marais wetu Kikwete na Magufuli.
Hayo maelezo hayapo sawa, yaani hayajakamilika.

Hint: Huyo balozi alikuwa mwakilishi wa Israel nchini Tanzania au nchi jirani na Tanzania?

 
Anhaa, mimi nahitaji akili za ziada? Okay.

Kwanza acha ku speculate na kutudanganya sababu ya Profesa Ntalikwa kutumbuliwa Nishati, hujui! Nobody knows, msomi hafanyi fanyi ma wild speculation kama hayo kwamba Ntalikwa ameshindwa ukatibu mkuu kwa sababu hawezi kujadili masuala muhimu japo kasoma. Such ridiculous, wild and woolly conclusions.

Kama ni mfuatiliaji mzuri wa siasa za Tanzania basi unatakiwa kujua kwamba teua-tengua za utawala huu ziko erratic and inexplicable, hazielezeki, and sometimes vindictive, visasi, kama Nape. TRA, kwa mfano, ina mabosi wangapi toka JPM achukue nchi, kwa nini hafanyi thorough vetting and prior perfomance evaluation of his nominees?

Hakuna teuzi za JPM ambazo ni thought through and strategic. Balozi wa Israel kachaguliwa kwa mtindo wa random draws.

Israel ni nchi ya kawaida tu, ila nyinyi ambao mnasema the bible is literally true then of course Israel ndio mwisho wa kila kitu. Incredibly feeble mind.


Hapo umeingiza ubashano wa kidini sasa. Ambao ktk namna ya kuelewa mambo utachemka. Kitu kikiwa halisi ni halisi tu, kama Israel wapo vizuri kwenye ulinzi wanakuwa hivyo tu haijalishi hutaki kukubaliana na hilo na kuthibitisha hilo US taifa ambalo linaongoza ktk masuala ya kujali ulinzi wa nchi wanawatumia hawa wa Israel kila siku. Vitu vingine ni dhahiri kabisa yani ni sawa mtu kwa sababu ni mweusi basi akatae kwamba wafanyabiashara wakubwa hapa nchini ni wahindi haitamsaidia kubadilosha uhalisia. Mambo mengine unakubaliana nayo tu then inachapa raba.
 
Miaka ya nyuma kidogo ilikua ni ngumu mkumjua afisa usalama wa Taifa nakumbuka niliwahi kujitia chizi mkoa fulani nikaibuka ofisi zao ili kuulizia nafasi za mafunzo nilienda asubuhi ila nilitoka jioni sanaaaa nikiwa nimeweka uchi ID yangu wale jamaa walinikomalia nimeambiwa na nani kua kuna nafasi siwezi sahau,siku hizi nikiwa bar mwehu anaanzisha ugomvi na anakimbilia kutoa kitambulisho kua yeye ni kitengo kuna mmoja alinikera sana alitoa kitambulisho na akasema hadi mshahara wao duh nimeshangaa juzi yule kilazà mwingine anatoa silaha kibwege vile alafu anamlenga mtu mchana kweupe tena mtua ambae hana silaha mbaya zaidi anakuja kudhibitiwa na Kitenge inaonyesha tumeoza kama Masima anapelekwa kwa nia ya kuimarisha kitengo naona ni vyema ila kama kumuimarisha mtu binafsi ni tatizo.
Sisi huwa tunaenda enda tu. Sijui ni kwa sababu ya kuwaacha watu wenye true passion na kazi fulani km jeshi na ku recruit watoto wa mjomba na shangazi?! Watu wanashindwa kufanya kazi zao wanabaki kusema tu usicheze na mimi unanijua?anatoa kitambulisho chake ate nae ni afisa wa TISS, kweli! Hilo neno INTELLIGENCE hapo linakuwa na maana gani sasa? Anyway tuna mengi ya kujifunza kutoka kwa wenzetu km CIA coz mbali na kuangalia usalama wa nchi zao wameenda mbali zaidi kwa kuangalia na kucontrol masuala ya uchumi kwa interest za nchi yao
 
Hivi ukilaza mtaacha lini watanzania? Lumumba inaingiaje hapa? Huu ni mjadala wa kichama huu?

Acha wivu kijana
Ukombozi wa kwa kutoka kwa mkolono ulishafanyika mwaka 1961. Sasa sijui huu unaohusu akili ambao ni mkubwa kuliko ule wa kwanza utafanyika lini? Maana taifa linaangamia kwa kuwa na vijana wasiojelewa.
 
Umeandika vyema sana.

Japo, nimesikitika sana kuona ama kusoma.kuwa pana mtu alikuja akapata shida ya kuingia japo JNIA yaani, sielewi kabisa sisi hapo Tanzania, unawezaje ukamuita mkufunzi toka nchi nyingine halafu ushindwe kumpokea hadi Simu ipigwe kutoka feri na chuoni?

Hii ni aibu kubwa na pia ni uratibu na ukaribisha wa wageni kuto nje ya nchi kuja huko Tanzania wa kiwango cha zero brains kabisa.

Intelligence services, wanashindwaje kumpokea mtu kwa ajili yao?

Ni aibu kama hayo ni kweli , wanahiitaji kufanyiwa msasa na PR and Protocol unity iwepo.

Ila, nimuulize mwandishi wa thread hii, kwa nini wewe unaona ulinzi na usalama kwa Tanzania kushirikiana na Israel na siyo nyanja zingine za maendeleo maana naona ndiyo sekta umeipatia kipaumbele? Ni kwa nini?
Ahsante.
Mkuu huyu Jamaa kadanganya huwezi kwenda sehemu kwa kazi nyeti usipokewe na mwenyeji wako,
 
Mkuu huyu Jamaa kadanganya huwezi kwenda sehemu kwa kazi nyeti usipokewe na mwenyeji wako,

Ndiyo maana, nami nimejiuliza maswali mengi na kusikitika sana kuwa kama tumefikia hapo basi. Tunahitaji miujiza ya mbinguni ili tuponye Taifa.
 
Back
Top Bottom