Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,809
- 218,463
Makada kadhaa wa ccm Mkoani Dar es Salaam , wameshangazwa na kuchukizwa na uteuzi wa Kada wa zamani wa Chadema , Ally Bananga kuwa Mwenezi wa Chama hicho Mkoani humo , makada hao wafia chama walidhani kama ni uteuzi basi wao ndio walipaswa kukumbukwa , kutokana na kutowahi kusaliti chama chao
Badala yake ameteuliwa aliyesaliti Chama na kukihujumu majukwaani , tena Wakuja ! jambo hili limewasononesha sana chawa waliodhani teuzi za DSM zitakuwa zao .
Mytake : CCM ina wenyewe , na hao wenyewe ndio wanaopanga safu ya uongozi , nyie wengine endeleeni kuvishwa fulana wakati wa uchaguzi .