Utendaji wa TBA, Mzee, si tulikutonya?

Utendaji wa TBA, Mzee, si tulikutonya?

Jana mh. Rais kaja juu.
Idara yake penzi ya TBA inasuasua.
Huko Magereza Ukonga ligwaride la ujenzi wa nyumba unaenda kwa mwendo wa kinyonga!

TBA walipewa, CASH, bilioni 20 kujenga nyumba za wana Magereza mwaka 2016, mpaka sasa mradi umefikia 35% ya maendeleo.

Mradi majuzi ulitembelewa na waziri mdogo Mambo ya Ndani, ndg Masauni.

Kwa spidi ya utekelezaji wa mradi TBA itawachukua miaka 12 kukamilisha kazi, leo ni mwaka wa 3-4 toka kazi ianze.

Lakini ngoja kidogo mzee, mh Rais.

Si tulikutonya hapa JF na kwingineko mitandaoni?

Ile ilikuwa early warning.


TBA sio mkandarasi, ni wakala wa nyumba za serikali , na tulijua hilo walitambua vema, maana si mgeni Wizara ya Ujenzi.

WAKALA TBA kazi yake ku manage masuala ya nyumba za serikali, si kujenga.

Vituko vilianza na mabweni ya chuo kikuu Mlimani.

Sitaongelea pesa ndogo kiduchu zinazosemekana kutumika, lakini ni wazi , kazi ilikuwa chini ya viwango
Mwanafunzi aliyelalamika mitandaoni juu ya kupasuka kuta, aliwekwa ndani, lakini si kwa amri yako , ni wale wapambe wasiotaka kukutonya ukweli.
Na kwa kweli hawakutakii mema.


Mawazo yangu mzee, TBA warudi kwenye kazi yao ya Uwakala wa nyumba za serikali, kazi za Ujenzi wawaachie wabobezi, Makandarasi.
Ila fahamu kuna miradi wameitekeleza kwa wakati na kwa ufanisi,nyumba za wanafunzi,udsm,ikulu ya rais Dodoma,wasilaumie moja kwa moja,pengine kuna tatizo lisilo lao,sema mkubwa hakosei

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ila fahamu kuna miradi wameitekeleza kwa wakati na kwa ufanisi,nyumba za wanafunzi,udsm,ikulu ya rais Dodoma,wasilaumie moja kwa moja,pengine kuna tatizo lisilo lao,sema mkubwa hakosei

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu upo Tanzania kweli?
Unatoa mfano wa hosteli za wanafunzi UDSM?
You are not serious, umezisikia "expansion joints"
 
Kazi ipo tena sio ndogo!!! Tatizo ni pale mtu anapotoa makadirio ya uongo ili tu amfurahishe mtu, ila anapopewa hiyo pesa sasa itumie kwenye huo ujenzi ndio hesabu zinapogoma, na kutoa zako za mfukoni huwezi unaamua potelea mbali bora lawama!! Ndio kinachotokea, waliona kuwa wakandarasi wanatoa mahesabu ya juu sana, bora wawatumie hao!!! Hata yule kiongozi wa jana anaposema eti ndani ya miezi miwili tu watakuwa wamekamilisha hayo majengo sio kadhi rahisi hivyo!!! Sehemu yenye utaalam waache siasa!!! NAFUU SIKU ZOTE NI GHARAMA
Hiyo ni kawaida mafundi ujenzi hasa mtaani, unampa ramani au unamwonyesha sehemu anakwambia hapa hela ndogo tuu, ukianza huo ujenzi hela aliyokwambia wala si robo kwa gharama halisi.
 
Jana mh. Rais kaja juu.
Idara yake penzi ya TBA inasuasua.
Huko Magereza Ukonga ligwaride la ujenzi wa nyumba unaenda kwa mwendo wa kinyonga!

TBA walipewa, CASH, bilioni 20 kujenga nyumba za wana Magereza mwaka 2016, mpaka sasa mradi umefikia 35% ya maendeleo.

Mradi majuzi ulitembelewa na waziri mdogo Mambo ya Ndani, ndg Masauni.

Kwa spidi ya utekelezaji wa mradi TBA itawachukua miaka 12 kukamilisha kazi, leo ni mwaka wa 3-4 toka kazi ianze.

Lakini ngoja kidogo mzee, mh Rais.

Si tulikutonya hapa JF na kwingineko mitandaoni?

Ile ilikuwa early warning.


TBA sio mkandarasi, ni wakala wa nyumba za serikali , na tulijua hilo walitambua vema, maana si mgeni Wizara ya Ujenzi.

WAKALA TBA kazi yake ku manage masuala ya nyumba za serikali, si kujenga.

Vituko vilianza na mabweni ya chuo kikuu Mlimani.

Sitaongelea pesa ndogo kiduchu zinazosemekana kutumika, lakini ni wazi , kazi ilikuwa chini ya viwango
Mwanafunzi aliyelalamika mitandaoni juu ya kupasuka kuta, aliwekwa ndani, lakini si kwa amri yako , ni wale wapambe wasiotaka kukutonya ukweli.
Na kwa kweli hawakutakii mema.


Mawazo yangu mzee, TBA warudi kwenye kazi yao ya Uwakala wa nyumba za serikali, kazi za Ujenzi wawaachie wabobezi, Makandarasi.
Bilioni 10!!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ila fahamu kuna miradi wameitekeleza kwa wakati na kwa ufanisi,nyumba za wanafunzi,udsm,ikulu ya rais Dodoma,wasilaumie moja kwa moja,pengine kuna tatizo lisilo lao,sema mkubwa hakosei

Sent using Jamii Forums mobile app
Hapana labda km upo TBA unawatetea kwa TBA, hapa Dodoma TBA walipewa nyumba zote za CDA badala ya kuwapa NHC sasa wakawafukuza wapangaji wote ambao si watumishi sehemu mbalimbali km Area C, Mjini kati Uzunguni nk ambako hata Mkuu wa mkoa huko kusini alikuwepo katika upangaji huo na akakarabati mpaka kujenga fensi.
Tamko likatoka kuwa ondokeni kuna Watumishi wa Serikali wanahamia kutoka DSM tunataka kuzikarabati.
Fungu walilopewa naona ni maji ya moto yaliyopoa kwani hakuna ukarabati mpaka nyasi zimevamia ndani mpaka viwanja vya watoto kuchezea,
TBA mnamuangusha Rais na hizi nyumba za Dodoma mnyang'anywe hata hizo nyumba za Serikali huko Mtumba ni kituko bora Wizara zibaki kwanza UDOM mpaka watakapopata wakandarasi binafsi na si Serikali yenyewe, wapewe Makampuni binafsi hata na ya nje km China nk
Jamani Serikali ya Kenya imejitoa kabisa katika ujenzi wa Majengo ktk Mji wa Nairobi majengo marefu ni ya makampuni ya nje km BRITAM TOWER ambapo Ofisi nyingi na za Serikali zimepanga
1552837467256.png
 
Kazi za ujenzi wapewe makampuni ya ukandarasi, TBA wabaki na kazi zao za kutangaza na kutathmini tender na ubora wa majengo na kufanya utafiti kwenye maswala ya ujenzi
 
Mimi nipo Kijiji cha Mwendakulima huku,nauliza hivi zile ghorofa za Magomeni kota zimeshaisha?maana sisi huku habari za Tanzania (Dar es salaam) tunazipata kwa nadra Sana
Mwenye taarifa naomba tafadhali

Sent using Jamii Forums mobile app
 
serikali kitu inaweza ni kuthibiti watu wenye kuonesha njia kwa kukosoa madhaifu yao.

hapo watafanya kila kitu ila sijui kutoa huduma za kijamii,ulinzi, hapo ni bashite
Hapo kwenye kutoa huduma za kijamii ni 0 kabisa ...reference ni mradi wa mwendo kasi na viwanda vilivyokufa nchini

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom