Utawala wa Marehemu Magufuli - Blessing in Disguise

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,543
41,047
Wengi waliumizwa vibaya na utawala wa Marehemu Magufuli. Taifa liliumizwa na utawala wa Magufuli:

1) Katiba iliwekwa kapuni

2) Sheria ziliwekwa jalalani

3) Utekaji, upotezaji na mauaji ya watu walioonekana kuukosoa utawala wake likawa jambo la kawaida (tupo kwenye vita ya uchumi. Atakayekwenda tofauti ni msakiti. Ninyi wanajeshi mnajua msaliti huwa anafanywa nini - Magufuli)

4) Demokrasia ikatupwa chooni (sasa ni wakati wa kujenga nchi. Napiga marufuku mikutano ya vyama vya siasa - Magufuli)

5) Kesi za kubambika watu ikawa adhabu kwa wale ambao utawala unataka kuwatia adabu (tajiri naweza kumfanya chochote wakati wowote - Magufuli)

6) Uporaji wa pesa za matajiri kikawa chanzo cha mapato ya serikali (DPP ongea na hao tunaowashtaki kwa ujumu uchumi. Wakikubali kutulipa, uwaachie, wakigoma, tena waache wakae huko moja kwa moja - Magufuli)

7) Kuibuka kwa wasaidizi wake majambazi (Sabaya, et al) wakiwa na mamlaka yasiyoguswa na chombo chochote

8) Matumizi ya pesa ya umma yasiyozingatia taratibu (report ya CAG)

9) Ufisadi uliolindwa na dola kwa kuziba midomo ya watu na uhuru wa vyombo vya habari (Magufuli aliiondoa Tanzania kwenye nchi zinazotekeleza mwongozo wa kuendesha Serikali kwa uwazi)

10) Kudororesha mahusiano ya kimataifa kwa ujeuri (vifaranga toka nchi jirani walichomwa, ng'ombe wa wafugaji wa nchi jirani 4,000 walioingia ardhi ya Tanzania walitaifishwa, na Magufuli akasema, Tanzania siyo shamba la bibi. Wiki moja baadaye ng'ombe wa wafugaji wa Tanzania 9,000 walikamatwa ndani ya ardhi ya Kenya, Wakaenya wakawarushia wafugaji wa Tanzania ng'ombea wote, na gavana wa Kenya kutamka kuwa uongozi wa Magufuli ulikuwa ni aibu ya Afrika. Watanzania wanalia, Wakenya wanalia)

11) Kuwajaza watu ujinga kwa propaganda mbalimbali (Magufuli akadai kuwa nchi yetu imekwishakuwa tajiri kiasi cha kuwa donor country, na miradi yote inajengwa kwa pesa zetu)

12) Kuwahadaa watu waamini kuwa mambo makubwa sana na ya pekee yanafanywa na utawala wake wakati mengi ya hayo mambo yalikwishafanywa hata na awamu zilizotangulia (SGR ya TAZARA ilijengwa wakati wa Mwalimu Nyerere, barabara za lami zenye urefu wa zaidi ya kilometa 12,000 zilijengwa wakati wa Kikwete, wakati wa Magufuli zilijengwa 2,800 tu. Ndege mpya 13 zilinunuliwa wakati wa Nyerere ukilinganisha ndege 8 zilizonunuliwa wakati wake. Daraja la Umoja wakati wa Mkapa, la Kigamboni wakati wa Kikwete, Mabwawa ya umeme ya Mtera, Kigansi, Kidatu, umeme wa gas ilikuwa wakati wa watanguluzi wake; yeye bwawa la Nyerere ikawa kelele kila siku. Vyuo vikuu UDSam, Sokoine, Dodoma; wakati wake hakuna hata kimoja. Hospitali kubwa Muhimbili, Mlaganzila, Taasisi ya Moyo ya Jakaya, Hospitali ya Mkapa; wakati waje hakuna hospitali kubwa hata moja; na mengine mengi, lakini aliwajaza ujinga raia wasio na uelewa waone kuwa watangulizi wake hawakufanya kitu)

13) Utawala wenye viashiria vya upendeleo na ubaguzi na wakati fulani kutamka wazi kabisa kuwa majimbo fulani ya uchaguzi hayatapelekewa maendeleo kwa sababu walichagua wapinzani

14) Kufuta uwepo wa bunge huru la wananchi na kumwagiza spika kuwa awashughulikie wabunge kule ndani kwa kuwatoa nje, halafu nje yeye atawashughulikia.

Kitu kilicho dhahiri ni kwamba Tanzania haijawahi kuwa na katiba nzuri bali ilitegemea hekima ya Rais, akiamua kuwaburuza, hakuna wa kumzuia.

Kuwepo kwa Marais waungwana, Nyerere, Mwinyi, Mkapa na Kikwete, kuliwafanya watu waamini tuna katiba na sheria nzuri. Rais marehemu Magufuli ndiye aliyewafumbua macho Watanzania waone kuwa tuna katiba mbaya sana na tuna sheria mbaya sana. Hivyo ujio wa Rais Magufuli, pamoja na hasara tuliyoipata, umetusaidia sana kutambua ubovu na ubaya wa katiba na sheria zetu. Hivyo badala ya kuona kuwa utawala wa marehemu ilikuwa ni laana tupu, tushukuru pia kuwa ndio uliowafumbua wengi macho kutambua katiba yetu ni mbovu kiasi gani. Utambuzi huo iwe ni kichocheo kikubwa cha kutaka katiba mpya, siyo kesho wala keshokutwa bali SASA.

Tusipofanya hivyo, utawala wa Samia, kwa sababu na wenyewe umejaa uungwana, utatusahaulisha tatizo la msingi la Taifa letu, ambalo ni KATIBA MBAYA.
 
Authoritarian ni aina ya Uongozi pia , ndivo ilivyo china, Urusi, Cuba, Iran .

Lkn hizi nchi ziko wapi???.


Afrika haiwezi kuendelea ikiwa mtaendelea kufurahia aina ya viongozi ambao kichwan ni weupe, Et kisa Wanaongea Maneno mepesi mepesi.


JPM wakat fulan alilazimika kuweka katiba pemben, Kwa sababu KATIBA YENYEWE NI MBOVU.

JPM ni mwafalsafa aloamin katika maendeleo kama alivyoyaona yeye.

Na kweli, alifanya mambo makubwa ya ajabu ambayo ukichanganya watangulizi wake wote, kwa pamoja, hawajafikia Mazuri alofanya JPM., kiongozi hakutafuta faida yake, hakua fisadi , hakujineemesha, alisema nafufua shirika la ndege,akafufua, akasema najenga hiki nakile, vikaonekana, akasema natumbua wafanyakazi hewa, akatumbua ,akasema natumbua vyeti feki,akatumbua ,NANI ANGEJENGA DARAJA LA BUSISI???? LEO HII SENGEREMA IMEUNGANISHWA KWA BARABARA .NANI ANGEJENGA????. Akasema Dodoma, serikali ikahamia ,sasahivi Dodoma inachanua, akasema Bwawa la umeme, Kazi ikaanza, sasahivi mnapigwa danadana ...

Alisema,akatenda, hakua mwanasiasa, yule alikua ni MCHAPAKAZI ALIYEJITOA KWA AJILI YA WENGI.



Labda, Tuweke mambo Sawa, Sasa hivi simnacheka , KAMA KUNA LA MAANA ATAKALOFANYA HUYU MAMA YENU , LIKAONEKANA, NA WATU WAKAPIGA MAKOFI , basi mtajipongeza.
 
Watanzania tumerogwa,Taifa Zima,Mkuu wa nchi(Rais), Viongozi mbalimbali wa siasa kumsimanga Marehemu hii inaonesha ni jinsi gan tulivyo malofa, wapumbavu,tuna mengi sana ya kujadili na si mtu mfu
 
Authoritarian ni aina ya Uongozi pia , ndivo ilivyo china, Urusi, Cuba, Iran .

Lkn hizi nchi ziko wapi???.


Afrika haiwezi kuendelea ikiwa mtaendelea kufurahia aina ya viongozi ambao kichwan ni weupe, Et kisa Wanaongea Maneno mepesi mepesi.


JPM wakat fulan alilazimika kuweka katiba pemben, Kwa sababu KATIBA YENYEWE NI MBOVU.

JPM ni mwafalsafa aloamin katika maendeleo kama alivyoyaona yeye.

Na kweli, alifanya mambo makubwa ya ajabu ambayo ukichanganya watangulizi wake wote, kwa pamoja, hawajafikia Mazuri alofanya JPM., kiongozi hakutafuta faida yake, hakua fisadi , hakujineemesha, alisema nafufua shirika la ndege,akafufua, akasema najenga hiki nakile, vikaonekana, akasema natumbua wafanyakazi hewa, akatumbua ,akasema natumbua vyeti feki,akatumbua ,NANI ANGEJENGA DARAJA LA BUSISI???? LEO HII SENGEREMA IMEUNGANISHWA KWA BARABARA .NANI ANGEJENGA????. Akasema Dodoma, serikali ikahamia ,sasahivi Dodoma inachanua, akasema Bwawa la umeme, Kazi ikaanza, sasahivi mnapigwa danadana ...

Alisema,akatenda, hakua mwanasiasa, yule alikua ni MCHAPAKAZI ALIYEJITOA KWA AJILI YA WENGI.



Labda, Tuweke mambo Sawa, Sasa hivi simnacheka , KAMA KUNA LA MAANA ATAKALOFANYA HUYU MAMA YENU , LIKAONEKANA, NA WATU WAKAPIGA MAKOFI , basi mtajipongeza.
Usiseme Mama yenu, sema Mama yetu, au Rais wetu. Kwani wewe una Rais mwingine?

Mimi siyo shabiki wa Samia, ni shabiki wa Tanzania. Kwa hiyo tusifanye arguments kiupambe au kiushabiki, mimi si shabiki wala mpambe wa kiongozi yeyote.

Kitu kimoja nakubaliana nawe kwa Magufuli, ni kuwa alikuwa akitaka kitu fulani kifanyike, basi alikuwa na uwezo wa kulazimisha/kuhakikisha kinafanyika. Hiyo ilikuwa positive qualification.

Shida ilikuwa katika kutambua ni jambo gani ni priority kwa wakati fulani au jambo gani litakuwa na positive impact kwa jambo jingine.

Na bahati mbaya sana alikosa quality nyingine nyingi za uongozi.
 
Authoritarian ni aina ya Uongozi pia , ndivo ilivyo china, Urusi, Cuba, Iran .

Lkn hizi nchi ziko wapi???.


Afrika haiwezi kuendelea ikiwa mtaendelea kufurahia aina ya viongozi ambao kichwan ni weupe, Et kisa Wanaongea Maneno mepesi mepesi.


JPM wakat fulan alilazimika kuweka katiba pemben, Kwa sababu KATIBA YENYEWE NI MBOVU.

JPM ni mwafalsafa aloamin katika maendeleo kama alivyoyaona yeye.

Na kweli, alifanya mambo makubwa ya ajabu ambayo ukichanganya watangulizi wake wote, kwa pamoja, hawajafikia Mazuri alofanya JPM., kiongozi hakutafuta faida yake, hakua fisadi , hakujineemesha, alisema nafufua shirika la ndege,akafufua, akasema najenga hiki nakile, vikaonekana, akasema natumbua wafanyakazi hewa, akatumbua ,akasema natumbua vyeti feki,akatumbua ,NANI ANGEJENGA DARAJA LA BUSISI???? LEO HII SENGEREMA IMEUNGANISHWA KWA BARABARA .NANI ANGEJENGA????. Akasema Dodoma, serikali ikahamia ,sasahivi Dodoma inachanua, akasema Bwawa la umeme, Kazi ikaanza, sasahivi mnapigwa danadana ...

Alisema,akatenda, hakua mwanasiasa, yule alikua ni MCHAPAKAZI ALIYEJITOA KWA AJILI YA WENGI.



Labda, Tuweke mambo Sawa, Sasa hivi simnacheka , KAMA KUNA LA MAANA ATAKALOFANYA HUYU MAMA YENU , LIKAONEKANA, NA WATU WAKAPIGA MAKOFI , basi mtajipongeza.
Hatuhitaji dikteta mjinga kama Magufuli
 
hakuna kitu cha kufanya wametazama mwaka mmoja wa kuwa madarakani hakuna hata kimoja alichofanya wamemtungia wimbo unasema mama anaupiga mwingi maana hakuna cha kusemea
 
Bila kusema sana magu alikuwa kiongozi nchi hii haijawahi kupata,Mambo mengi yaloshindikana miaka, magu alitaka kuyaona yakifanyika na kweli yakifanyika ingawa siyo sawa kusema eti hakujenga hata km moja ya lami Wala hospitali kubwa hizo ni chuki tu waulize waishio simiyu,huko mtwara hakuna hospitali mpya?magu alikuwa na akili kubwa sana na uzalendo wa Hali ya juu mambo hayo tutayakosa sana kwa akili hizi.
 
Bila kusema sana magu alikuwa kiongozi nchi hii haijawahi kupata,Mambo mengi yaloshindikana miaka, magu alitaka kuyaona yakifanyika na kweli yakifanyika ingawa siyo sawa kusema eti hakujenga hata km moja ya lami Wala hospitali kubwa hizo ni chuki tu waulize waishio simiyu,huko mtwara hakuna hospitali mpya?magu alikuwa na akili kubwa sana na uzalendo wa Hali ya juu mambo hayo tutayakosa sana kwa akili hizi.
Hakuwa mkweli
Hii itamuandama vizazi na vizazi
 
Wengi waliumizwa vibaya na utawala wa Marehemu Magufuli. Taifa liliumizwa na utawala wa Magufuli:

1) Katiba iliwekwa kapuni

2) Sheria ziliwekwa jalalani

3) Utekaji, upotezaji na mauaji ya watu walioonekana kuukosoa utawala wake likawa jambo la kawaida (tupo kwenye vita ya uchumi. Atakayekwenda tofauti ni msakiti. Ninyi wanajeshi mnajua msaliti huwa anafanywa nini - Magufuli)

4) Demokrasia ikatupwa chooni (sasa ni wakati wa kujenga nchi. Napiga marufuku mikutano ya vyama vya siasa - Magufuli)

5) Kesi za kubambika watu ikawa adhabu kwa wale ambao utawala unataka kuwatia adabu (tajiri naweza kumfanya chochote wakati wowote - Magufuli)

6) Uporaji wa pesa za matajiri kikawa chanzo cha mapato ya serikali (DPP ongea na hao tunaowashtaki kwa ujumu uchumi. Wakikubali kutulipa, uwaachie, wakigoma, tena waache wakae huko moja kwa moja - Magufuli)

7) Kuibuka kwa wasaidizi wake majambazi (Sabaya, et al) wakiwa na mamlaka yasiyoguswa na chombo chochote

8) Matumizi ya pesa ya umma yasiyozingatia taratibu (report ya CAG)

9) Ufisadi uliolindwa na dola kwa kuziba midomo ya watu na uhuru wa vyombo vya habari (Magufuli aliiondoa Tanzania kwenye nchi zinazotekeleza mwongozo wa kuendesha Serikali kwa uwazi)

10) Kudororesha mahusiano ya kimataifa kwa ujeuri (vifaranga toka nchi jirani walichomwa, ng'ombe wa wafugaji wa nchi jirani 4,000 walioingia ardhi ya Tanzania walitaifishwa, na Magufuli akasema, Tanzania siyo shamba la bibi. Wiki moja baadaye ng'ombe wa wafugaji wa Tanzania 9,000 walikamatwa ndani ya ardhi ya Kenya, Wakaenya wakawarushia wafugaji wa Tanzania ng'ombea wote, na gavana wa Kenya kutamka kuwa uongozi wa Magufuli ulikuwa ni aibu ya Afrika. Watanzania wanalia, Wakenya wanalia)

11) Kuwajaza watu ujinga kwa propaganda mbalimbali (Magufuli akadai kuwa nchi yetu imekwishakuwa tajiri kiasi cha kuwa donor country, na miradi yote inajengwa kwa pesa zetu)

12) Kuwahadaa watu waamini kuwa mambo makubwa sana na ya pekee yanafanywa na utawala wake wakati mengi ya hayo mambo yalikwishafanywa hata na awamu zilizotangulia (SGR ya TAZARA ilijengwa wakati wa Mwalimu Nyerere, barabara za lami zenye urefu wa zaidi ya kilometa 12,000 zilijengwa wakati wa Kikwete, wakati wa Magufuli zilijengwa 2,800 tu. Ndege mpya 13 zilinunuliwa wakati wa Nyerere ukilinganisha ndege 8 zilizonunuliwa wakati wake. Daraja la Umoja wakati wa Mkapa, la Kigamboni wakati wa Kikwete, Mabwawa ya umeme ya Mtera, Kigansi, Kidatu, umeme wa gas ilikuwa wakati wa watanguluzi wake; yeye bwawa la Nyerere ikawa kelele kila siku. Vyuo vikuu UDSam, Sokoine, Dodoma; wakati wake hakuna hata kimoja. Hospitali kubwa Muhimbili, Mlaganzila, Taasisi ya Moyo ya Jakaya, Hospitali ya Mkapa; wakati waje hakuna hospitali kubwa hata moja; na mengine mengi, lakini aliwajaza ujinga raia wasio na uelewa waone kuwa watangulizi wake hawakufanya kitu)

13) Utawala wenye viashiria vya upendeleo na ubaguzi na wakati fulani kutamka wazi kabisa kuwa majimbo fulani ya uchaguzi hayatapelekewa maendeleo kwa sababu walichagua wapinzani

14) Kufuta uwepo wa bunge huru la wananchi na kumwagiza spika kuwa awashughulikie wabunge kule ndani kwa kuwatoa nje, halafu nje yeye atawashughulikia.

Kitu kilicho dhahiri ni kwamba Tanzania haijawahi kuwa na katiba nzuri bali ilitegemea hekima ya Rais, akiamua kuwaburuza, hakuna wa kumzuia.

Kuwepo kwa Marais waungwana, Nyerere, Mwinyi, Mkapa na Kikwete, kuliwafanya watu waamini tuna katiba na sheria nzuri. Rais marehemu Magufuli ndiye aliyewafumbua macho Watanzania waone kuwa tuna katiba mbaya sana na tuna sheria mbaya sana. Hivyo ujio wa Rais Magufuli, pamoja na hasara tuliyoipata, umetusaidia sana kutambua ubovu na ubaya wa katiba na sheria zetu. Hivyo badala ya kuona kuwa utawala wa marehemu ilikuwa ni laana tupu, tushukuru pia kuwa ndio uliowafumbua wengi macho kutambua katiba yetu ni mbovu kiasi gani. Utambuzi huo iwe ni kichocheo kikubwa cha kutaka katiba mpya, siyo kesho wala keshokutwa bali SASA.

Tusipofanya hivyo, utawala wa Samia, kwa sababu na wenyewe umejaa uungwana, utatusahaulisha tatizo la msingi la Taifa letu, ambalo ni KATIBA MBAYA.
No blessing at all, it was a great curse.
 
Bila kusema sana magu alikuwa kiongozi nchi hii haijawahi kupata,Mambo mengi yaloshindikana miaka, magu alitaka kuyaona yakifanyika na kweli yakifanyika ingawa siyo sawa kusema eti hakujenga hata km moja ya lami Wala hospitali kubwa hizo ni chuki tu waulize waishio simiyu,huko mtwara hakuna hospitali mpya?magu alikuwa na akili kubwa sana na uzalendo wa Hali ya juu mambo hayo tutayakosa sana kwa akili hizi.
Nimesema hospitali kubwa siyo hospitali za Wilaya au vituo vya afya.

Kwa ufafanuzi zaidi, hospitali zote za Wilaya na vituo vya afya vilivyojengwa wakati wa awamu ya 5, katika thamani havifikii hospitali moja kubwa kama Mloganzila au Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete, zilizojengwa awamu ya 4.

Wakati wa awamu ya 5, kulijengwa 2,800km za lami. Wakati wa awanu ya 4 zilijengwa 12,000km za lami. Compare the difference.
 
Authoritarian ni aina ya Uongozi pia , ndivo ilivyo china, Urusi, Cuba, Iran .

Lkn hizi nchi ziko wapi???.


Afrika haiwezi kuendelea ikiwa mtaendelea kufurahia aina ya viongozi ambao kichwan ni weupe, Et kisa Wanaongea Maneno mepesi mepesi.


JPM wakat fulan alilazimika kuweka katiba pemben, Kwa sababu KATIBA YENYEWE NI MBOVU.

JPM ni mwafalsafa aloamin katika maendeleo kama alivyoyaona yeye.

Na kweli, alifanya mambo makubwa ya ajabu ambayo ukichanganya watangulizi wake wote, kwa pamoja, hawajafikia Mazuri alofanya JPM., kiongozi hakutafuta faida yake, hakua fisadi , hakujineemesha, alisema nafufua shirika la ndege,akafufua, akasema najenga hiki nakile, vikaonekana, akasema natumbua wafanyakazi hewa, akatumbua ,akasema natumbua vyeti feki,akatumbua ,NANI ANGEJENGA DARAJA LA BUSISI???? LEO HII SENGEREMA IMEUNGANISHWA KWA BARABARA .NANI ANGEJENGA????. Akasema Dodoma, serikali ikahamia ,sasahivi Dodoma inachanua, akasema Bwawa la umeme, Kazi ikaanza, sasahivi mnapigwa danadana ...

Alisema,akatenda, hakua mwanasiasa, yule alikua ni MCHAPAKAZI ALIYEJITOA KWA AJILI YA WENGI.



Labda, Tuweke mambo Sawa, Sasa hivi simnacheka , KAMA KUNA LA MAANA ATAKALOFANYA HUYU MAMA YENU , LIKAONEKANA, NA WATU WAKAPIGA MAKOFI , basi mtajipongeza.
Hizo nchi karibu zote ulizotaja ni za kijamaa
Ni system ambayo inazalisha watu wavivu ,wajinga na wanafiki kwa kiasi kikubwa

Nimefanya biashara na wachina personally, they are nut heads , ni matapeli na wanawaza kukupiga kila hatua , hata hii ya serikali yetu kuwakumbatia sana wachina huko mbele tutakuja kupata majibu, yale. yaliyitokea zambia police na zambia power ndio exactly malengo ya wachina wote hapa Africa .

Hizi sio enzi za authoritarian leadership na yeyote anayejaribu kupractise , aina hii ya uongozi anafeli vibaya , it juct cant click with the current environments.
 
Kuna mipumbavu imelipwa humu kumsema Jpm hebu kanyeni mkalale hizo kenge zenu mnazo zitetea ndo zinajimilikisha nchi kama ni ya ukoo wao.... nyie kenge mkiambulia buku saba jioni mnarudi kukaa kwa shemeji zenu na kulala sebureni shwain kabisa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom