Utatu unaokiangamiza kizazi cha kesho. Utatu wa kuogofya kwa maslahi ya chama "chawala''

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,648
698,243
Uchumi unahujumiwa hapa

1. Bodaboda
Nchi zinakotoka zimeshapigwa marufuku kutokana na kuongezeka kwa walemavu, yatima na wajane huku nguvukazi ya taifa ikipungua na hata kutishia kizazi kijacho.

2. Kamari
Wawekezaji wa hii michezo ya kubahatisha na kamari nchini kwao ni marufuku na ni kosa la jinai lenye adhabu kali ukikutwa unacheza hii michezo, Taifa lao limetenga eneo maalum la visiwa mbali na wengine kwa wale wenye kupenda kuchezea pesa.. Sisi huku hatuna hiyo mipaka kwakuwa tu washika dau pamoja na chama chawala wanakula %.

3. Pombe kali za vichupa vya plastic mbadala wa viroba.
Wawekezaji ni mixer na wabongo lakini mashine zinatoka kulekule.

Picha likoje!
Kijana aliyefeli maisha kwa namna zote anapata pikipiki ya mkataba. Lakini kumbuka huyu ni kijana damu changa na limbukeni wa mengi na vingi.. Kwa bahati mbaya sana anaingia kwenye mtego wa kuhudumia familia, wazazi na wengine hata ndugu.. Lakini pia anahitaji matumizi binafsi

Picha linaendelea
Boda boda lake na hata kijiweni nyingi zimefungwa FM radio ambazo nyingi muda wote zinahamasisha michezo ya bahati na sibu na kamari kama njia ya kutoboa kimaisha kwa kujishindia mamilioni. Akifikiria ndoto zake, akifikiria majukumu yake anajikuta hana jinsi bali ajaribu bahati yake, prngine Mungu atamuona

Asichojua kamari ni biashara ya kitapeli isiyo na chembe ya huruma inayozingia faida yake tu. Anacheza michezo miwili mitatu na kuputwa mapato yote ya siku na pengine na hakiba.

Picha linafikia patamu sasa. Kwa stress za kuliwa na kukosa utajiri wa haraka, huku akiwa hana sent mfukoni anakopa kwa mshkaji 5000 aweke mafuta ya buku, anunue chochote cha buku 2 cha kurudi nacho home.. Kishapo! Buku 2 atoe lock kwa vipombe vikali maana hiyo ni sawa na bia moja ambayo haimfikishi popote!

Anakapiga kachupa chap bila kuzingatia kuwa kako dry kisha anaenda home kupumzika. Lakini huko njiani anaweza kukutana na mengi Kutokana na kilevi. Ajali ndogo ya kumlaza ndani siku mbili tatu
Ajali kubwa ya kupelekwa hospital akuwa majeruhi na kutumia siku kadhaa akiwa kitandani. Ajali kubwa zaidi ya kumsababishia majeraha makubwa na ulemavu na kubaji kuwa tegemezi badala ya tegemewa!
Ajali kubwa kabisa ya kumsababishia kifo Na kuacha yatima na wajane.

Serikali ya chama chawala inaruhusu baadhi ya biashara bila kutafakari madhara yake kwa kina ya sasa na ya baadae. Wanachoangalia na kujali ni kile kinachoingia mifukoni mwao. Huu ni uhujumi uchumi mkubwa sana kwa baraka za chama chawala.

bodaboda.jpg
Bodaboda%202.jpg
boda.jpg
 
Ukweli huu mchungu ndio maana wapangaji wa pale Lumumba wanashindwa kuujibu kwa ukweli,vijana ambao ndio taifa la leo wanajiona wameshafanikiwa kimaisha kwa kuwa bodaboda, politicians wetu wametumia mtaji wa uduni wa kielimu wa vijana hawa na kuwaaminisha kuwa eti bodaboda nayo ni ajira, na mbaya zaidi hawa royal families watoto wao sio bodaboda.
 
Bila kuweka mihemko na hisia binafsi ni dhahiri kuwa serikali na jamii kwa ujumla kuna sehemu ya majukumu muhimu yamepewa kisogo na uhalisia ulio wazi ni kwamba tunako kwenda ni hatari sana maana imekuwa kawaida ya watu kufanya vitu vya ajabu kuonekana kawaida moja wapo ni hizi kamari kwa jina michezo ya bahati nasibu.

"Fikra yakinifu lazima itoke kwenye akili yakinifu"
 
In the long run nguvu kazi imekufa. Bado dili za magendo wanazoingizwa huko ndio wanapotelea bila alama kuonekana.

Jamaa yangu alikuwa boda mara leo amebebeshwa mirungi mara nyaya za Tanesco, ukiuliza dau analopewa ni 7000 zaidi 10,000 at such high risk stake.

Siku alikuja kukamatwa familia ilijikamua vilivyo kumtoa huko, tajiri mmiliki hana habari
 
Bila kuweka mihemko na hisia binafsi ni dhahiri kuwa serikali na jamii kwa ujumla kuna sehemu ya majukumu muhimu yamepewa kisogo na uhalisia ulio wazi ni kwamba tunako kwenda ni hatari sana maana imekuwa kawaida ya watu kufanya vitu vya ajabu kuonekana kawaida moja wapo ni hizi kamari kwa jina michezo ya bahati nasibu.

"Fikra yakinifu lazima itoke kwenye akili yakinifu"
Maofisa usafirishaji lakini changamoto zao zinafumbiwa macho
 
Ni kweli , ukikwepa kuwekeza ktk Taifa,unawekeza ktk uroho wa madaraka,na kukiteketeza kizazi cha Taifa,kwa kuwalisha maneno feki ,ili wajione wamepata ajira na bahati,"Tuki amka ,tutafanikiwa"
Maofisa usafiri
 
Hapo namba moja, tupate suluhu ya hili tatizo as we all brand it. Kila changamoto inayokuwa raised lazima ipatiwe solution la sivyo zinakuwa stories tu ambazo kesho kila mtu anasahau.

Let's come up with solutions, tunaondoaje bodaboda barabarani?
...Graduates wa vyuo vikuu kila mwaka ni kiasi gani?
...Dropouts wa vyuo vikuu ni wangapi kila mwaka?
...Wahitimu wa vyuo vya kati ni wangapi?
...Waliomaliza form iv na vi bila kuendelea vyuo vya ufundi no wangapi?

Serikali inaajiri kiasi gani cha wahitimu kila mwaka, sekta binafsi je?

Hawa 'leftovers" waende wapi, wafanye nini?

Let's be concrete..tusilalamike tu.
 
Hapo namba moja, tupate suluhu ya hili tatizo as we all brand it. Kila changamoto inayokuwa raised lazima ipatiwe solution la sivyo zinakuwa stories tu ambazo kesho kila mtu anasahau.

Let's come up with solutions, tunaondoaje bodaboda barabarani?
...Graduates wa vyuo vikuu kila mwaka ni kiasi gani?
...Dropouts wa vyuo vikuu ni wangapi kila mwaka?
...Wahitimu wa vyuo vya kati ni wangapi?
...Waliomaliza form iv na vi bila kuendelea vyuo vya ufundi no wangapi?

Serikali inaajiri kiasi gani cha wahitimu kila mwaka, sekta binafsi je?

Hawa 'leftovers" waende wapi, wafanye nini?

Let's be concrete..tusilalamike tu.
Thinking great way.. Cha kwanza ndio hiki nilichofanya kuainisha tatizo... Automatically hatua ya pili ni mjadala wa bunge tena ikibidi kwa hati ya dharura LAKINI wabunge haohao ndio ombaomba na wahemeaji kwa hao wafanyabiashara wanaofanya hizo biashara
 
Maisha ya vijana yapo hatarini sana, bodaboda, kamari, pombe, energy drink, masturbation, kuruka kijoti nk.

Muda sasa wa kuangalia upya azimio la Arusha vijiji vya ujamaa virudi , vijana turudi kijijini tukalime na kufuga.
 
Bora wale wanasiasa wa chama hicho waache kujipendekeza kwa makundi yanayofanya shughuli tata. Bodaboda, betting na zingine za hovyohovyo ni ishara ya umasikini uliokithi katika jamii
 
Bora wale wanasiasa wa chama hicho waache kujipendekeza kwa makundi yanayofanya shughuli tata. Bodaboda, betting na zingine za hovyohovyo ni ishara ya umasikini uliokithi katika jamii
Pesa tamu hasa ikiwa ya rushwa bila kutanguliza maslahi ya taifa
 
Back
Top Bottom