Utata wa wafanyabiashara wa Zanzibar kulipa kodi mara mbili inachukua miaka zaidi ya 40!

Ileje

JF-Expert Member
Dec 20, 2011
8,798
12,240
Nimesikitishwa na kauli ya waziri wa fedha Dr. Mgimwa kuwa ataunda tume itakayojumuisha TRA na wizara yake kujadili namna ya kuondoa kodi mbili wanazotozwa wafanyabiashara za Zanzibar!

  1. Hivi kweli serikali ya CCM imeshindwa kushughulikia kero hii ya muungano kwa miaka yote hii ikiwa madarakani?
  2. Ni sheria ipi imekuwa ikiwakwaza mawaziri wote na viongozi wa TRA waliopita kuondoa kero hii?
  3. Ni ugumu gani ulioifanya serikali ya muungano kutowasilisha marekebisho ya sheria hiyo ya wizi kama ipo?
  4. Hivi si kweli tumekuwa na mawaziri wa fedha wasiowajibika au wasiojua kazi yao kwa kipindi chote cha muungano?

HEY SERIKALI YA CCM ONDOENI AIBU HII YA KERO HARAKA!
 
Jamaa katoka zenji leo na luninga na oven moja. Kafika bandarini DSM, TRA wamembana alipe 25% ya kila kimoja wakati ZNZ katoka free of charge.
Hili suala bado linaleta utata sana kuhusu Muungano na imepelekea mpaka baadhi ya wasafiri kususia mizigo yai na kurudi nayo ZNZ.

Maana ya Muungano hapa iko wapi? Nisaidieni wandugu labda sielewi...
 
Back
Top Bottom