Loading failed
JF-Expert Member
- Sep 14, 2023
- 1,945
- 5,849
Ndugu wana Jf kwa heshima kubwa nawasalimu sana.
Humu ndani kuna watu wa imani tofauti tafauti na kila rika kwa nafasi zao naombeni msaidie ushauri wa haraka hapa
Katika pilika pilika za kimaisha mdogo wangu (mkristo) alijipatia binti wa imani ya kislam wazazi wake ni swala tano (5), na ameka na binti yao kwenye urafiki na mahusiano ya kimapenzi kwa muda mrefu wa miaka mitatu takribani kiasi cha kuaminiana na kumpa binti mimba.
Binti ana mimba ya miezi saba sasa na mdogo wangu anataka kumuoa huyu binti awe mke wake kabisa kabisa kwani hapendi kuona anamtelekeza mwanamke walie pendana naye kisa imani zao tofauti
Shida imekuja kujitokeza ni kwamba wazazi wa binti wanataka dogo awe muislam ili amuoe binti yao ila dogo amesema hawezi kubadili dini yake kabisa wakuu japo binti yao anampenda na yupo teyari awe mke wake
Nime muuliza kwa upande wa huyo binti (mpenzi wake ) ana semaje yeye kasema binti hana shida yeyote shida ni yeye ana ogopa wazazi wake kuchange dini amfate dogo kwenye ukristo , ila anampenda sana dogo na yupo teyari kuwa mke wake na anampenda sana.
Dogo nae anasema tokea yupo na binti ana mfundisha na kusali na binti kwa imani ya kikristo na huyo mpenzi wake hana shida kabisa na ana furahia bila shaka yeyote
Ndugu wana Jf kwa imani zenu na kwa kila hali sisi kama ndugu wa mdogo wetu mpaka sasa tumeshindwa kujua tuwasaidie vipi huyu kijana na huyu binti ili wawe mume na mke na waendeshe maisha yao kwa amani na baraka tele kutoka kwa wazazi wa pande zote pamoja na huyo kiumbe aliye tumboni kwa mwanadada pindi atakapo zaliwa.
Nimekuja hapa kuomba mawazo yenu ya hali na mali kuwasaidia hawa vijana walio ingia katika utata huu wa kiimani katika mahusiano yao, pia ili kuwafanya wawe pamoja ukizingatia dogo hataki kabisa kufata dini ya mwanamke wake na mwanamke yupo teyari kumsikiliza dogo na kufata dini yake na kua mke wake ,shida ni wazazi wa mwanamke hapa .
Ndugu saidie huyu kijana na huyu binti wavuke hapa wakuu .
Asanteni
Humu ndani kuna watu wa imani tofauti tafauti na kila rika kwa nafasi zao naombeni msaidie ushauri wa haraka hapa
Katika pilika pilika za kimaisha mdogo wangu (mkristo) alijipatia binti wa imani ya kislam wazazi wake ni swala tano (5), na ameka na binti yao kwenye urafiki na mahusiano ya kimapenzi kwa muda mrefu wa miaka mitatu takribani kiasi cha kuaminiana na kumpa binti mimba.
Binti ana mimba ya miezi saba sasa na mdogo wangu anataka kumuoa huyu binti awe mke wake kabisa kabisa kwani hapendi kuona anamtelekeza mwanamke walie pendana naye kisa imani zao tofauti
Shida imekuja kujitokeza ni kwamba wazazi wa binti wanataka dogo awe muislam ili amuoe binti yao ila dogo amesema hawezi kubadili dini yake kabisa wakuu japo binti yao anampenda na yupo teyari awe mke wake
Nime muuliza kwa upande wa huyo binti (mpenzi wake ) ana semaje yeye kasema binti hana shida yeyote shida ni yeye ana ogopa wazazi wake kuchange dini amfate dogo kwenye ukristo , ila anampenda sana dogo na yupo teyari kuwa mke wake na anampenda sana.
Dogo nae anasema tokea yupo na binti ana mfundisha na kusali na binti kwa imani ya kikristo na huyo mpenzi wake hana shida kabisa na ana furahia bila shaka yeyote
Ndugu wana Jf kwa imani zenu na kwa kila hali sisi kama ndugu wa mdogo wetu mpaka sasa tumeshindwa kujua tuwasaidie vipi huyu kijana na huyu binti ili wawe mume na mke na waendeshe maisha yao kwa amani na baraka tele kutoka kwa wazazi wa pande zote pamoja na huyo kiumbe aliye tumboni kwa mwanadada pindi atakapo zaliwa.
Nimekuja hapa kuomba mawazo yenu ya hali na mali kuwasaidia hawa vijana walio ingia katika utata huu wa kiimani katika mahusiano yao, pia ili kuwafanya wawe pamoja ukizingatia dogo hataki kabisa kufata dini ya mwanamke wake na mwanamke yupo teyari kumsikiliza dogo na kufata dini yake na kua mke wake ,shida ni wazazi wa mwanamke hapa .
Ndugu saidie huyu kijana na huyu binti wavuke hapa wakuu .
Asanteni