Elias Msuya
Senior Member
- Dec 23, 2011
- 173
- 671
Tangu kundi la G55 linalohusisha makada wa Chadema wanaotaka chama hicho kishiriki uchaguzi, kumekuwa na maswali mengi kuhusu malengo ya kundi hilo.
Kundi hilo linakuja na msimamo wa kutaka kushiriki uchaguzi kinyume na kampeni ya No reforms No election (Hakuna mmabadiliko, hakuna uchaguzi) iliyopitishwa na vikao vya chama hicho na sasa inaenezwa nchini kote.
Kundi hilo limekutana na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Jumapili Aprili 6, 2025 na kuweka wazi maoni yao kwa chama.
Baada ya kikao hicho, msemaji wa G55, John Mrema akafanya mahojiano na Jamii Forums.
Endelea…
Swali: Hii kampeni ya No reforms no election ilianza tangu wakati Freeman Mbowe akiwa madarakani, mbona hamkuwahi kuipinga?
Jibu: Ni kweli baada ya uchaguzi wa mwaka 2020, tulifanya kikao cha retreat (kujipanga) kilichofanyika Kaunti ya Makuweni Nairobi Kenya, tulikaa hapo, siku saba na wajumbe woote wa kamati kuu, Mheshimiwa Lissu alikuwepo wakati huo alikuwa Makamu Mwenyekiti alitoka Ubeligiji akaja.
Tulichomaanisha wakati ule, hakuna mahali tulisema No reforms no election ni kuzuia uchaguzi, tulimaanisha kukusanya nguvu za wadau, taasisi za dini, asasi za kiraia, tubebe hilo wimbi wakati tunashinisha uandishi wa Katiba mpya.
Swali: Ni kama unapiga chenga tu, maana hapo mnasema, Hakuna mabadiliko hakuna uchaguzi?
Jibu: Hatujawahi kumaanisha kwamba hakuna uchaguzi ni kuzuia uchaguzi, kwa sababu tunajua gharama ya kuzuia uchaguzi ni nini. Kwa hiyo leo tunaposema tunazuia uchaguzi, tunauzuaiaje wakati tukko nje ya uchaguzi?
Ni Dhahiri, vyama vitakavyoingia kwenye uchaguzi vitapewa ruhusa ya kushiriki kwenye kamppeni, kuwekja mawakala, wagombea, sisi tutakuwa nje tutazuiaje huo uchaguzi? Tuongie ndani tuzuie tukiwa ndani. Kenya kina Raila Odinga, walijua kwamba wataumizwa watauawa, lakini walisonga mbele wakaleta mabadiliko.
Raila na nguvu yote aliyonayo hajawahi kusema atazuia uchaguzi, anaingia anapambana na mifumo hiyo hiyo Zambia Hichilema alipambana na rais aliyekuwa madarakani. Angesema leo hashiriki uchaguzi, asingekuwa rais. Ghana New Patriotic Party (NPP) imendolewa na NDC (National Democratic Congress), wangesema hakuna uchaguzi wangekuwa wai leo.
Tumeona hapop Kusini mwa Afrika, mpinzani ameshinda, Msumbiji hapo watu wameingia barabarani, wameshiriki.
Swali: Kwa hiyo unakiri kwamba kampeni hii ilikuwa haijaeleweka wakati mnaiandaa?
Jibu: Nimesema hatujawahi kusema tunazuia uchaguzi, dhana na andiko lake lipo, kuhakikisha kwamba tunakutana makundi yote, viongzoi wa dini na asasi za kiraia.
Hii dhana ya kuzuia uchaguzi tunaona utekelezaji wake hauonekani, hata ukitafuta kwa tochi, hatuoni unaendaje kuzuia uchaguzi kwa nchi zetu za Afrika.
Swali: Inaonyesha kundi hili la G55 linaundwa na makada wa Chadema waliokuwa wakimuunga mkono Freeman Mbowe katika uchaguzi na baada ya mgombea huyo kushindwa, sasa mmeamua kupinga kila kinachoelekezwa na uongozi mpya wa chama?
Jibu: Kwanza niseme tu, wakati wa uchaguzi wa ndani ya chama kulikuwa na kampeni, ziliendeshwa kwa usawa na kila mtu akamuunga mkono mtu anayemtaka, lakini wakati huu tuliopo sasa, uchaguzi wa ndabiu ya chama umeisha na sasa kinachofanyika ni kundi linalounganisha wanachama na viongozi wanaotaka uchaguzi, kwa sababu hatuoni mkakati wala muujiza wa kuzuia uchaguzi kwa mazingira ya sasa kama Taifa.
Kwa hiyo dhana ya kuzuia uchaguzi tunaona haitekelezeki, haiwezekani na hatuwezi kuifanikisha kwa mazingira ya sasa yaliopo kwa nchi yetu.
Kwa hiyo kundi hili lina nia njema ya kukushauri chama kushiriki uchaguzi kwa sababu hatuoni uwezo wa sisi kuzuia huo uchaguzi. Hicho hatukuioni.
Swali: Nimeuliza hivyo kwa sababu naona pia mnapinga kampeni ya uchangishaji wa fedha za chama maarufu Tone Tone. Kwa nini?
Jibu: Tone tone ilikuwepo kwenye program za chama, uongozi mpya umekuja kuiendeleza tu, sisi tuliita Tona Tona. Tulishai design, chini ya Reginald Munisi aliyekuwa Mkurugenzi wa Digital. Ilikuwepo, wao walikuta ilikuwepo. Wao wamebadili tu wakaweka Tone Tone.
Ipo ndani ya ofisi ya Katibu Mkuu, imeshawekwa kwenye Chadema App, sio kwamba wameianzisha. Wameikuta.
Swali: Sasa kwa nini mnaipinga?
Jibu: Sio kwamba tunaipinga, nilichosema ni kwamba, viongozi wanachama wanachangia wakiwa na sababu. Ndio maana viongozi walipowekwa gerezani mwaka 2018, ndani ya saa 48 tuliweza kuchangisha Sh350 milioni, kwa sababu wote waliona kuna sababu ya kuwatoa viongozi gerezani.
Leo ukiwaambia tunakwenda kuzuia uchaguzi, halafu unawaambia harakati za chama, wanachangia ili iweje? Kwa hiyo wakati tunataka wachangia, lazima tuwape sababu. Ukiwaambia unakwenda kuzuia uchaguzi, wao hawataki, sasa mnachangia ili mfanye nini?
Swali: Wamesema wanachangia kwa sababu ruzuku haitoishi na wamesema kama watachangia vizuri wanaweza kukiendesha chama bila kutegemea ruzuku. Hilo nalo mnapinga?
Jibu: Hatupingi dhana ya wanachama kuchangia, kwanza huo ni wajibu wa mwanachama, ila sisi tunasema ni lazima viongozi wawape sababu wanachama na wananchi.
Swali: Si ndio sababu hiyo ya kuendesha chama?
Jibu: Ndio, lakini kama chama hakishiriki uchaguzi maana yake ule uhalali wa kisiasa, unapepea. Kwa sababu chama kinaposema kinakwenda kuzuia uchaguzi, ieleweke sio kazi lelemama. Ni kazi ambayo mnatangaza kwamba, sisi kama chama tunapanga kwenda kupamnana na Dola.
Sasa hivi Dola linajiandaa kutudhibiti. Sasa wanachama wetu sio kwamba, hawaoni, wanaona na wanaelewa.
Kwa hiyo sisi tunawashauri viongozi wafikirie na waelewe kwamba huu uamuzi wa kuzuia uchaguzi, ni rahisi Zaidi kuzuia uchaguzi ukiwa ndani ya uchaguzi na niseme tu, kesho kutwa baada ya Bunge kuvunjwa Juni, vyama vyote vya siasa, vinajielekeza kwenye election mood (mtazanmo wa uchaguzi).
Chadema tukiendelea na huu msimamo wa kuzuia uchaguzi, hatutafanya shughuli yoyote ya siasa, kwa sababu kwenye kampeni hatutakuwepo, maana hatutashiriki uchaguzi, kuanzia Agosti mpaka Oktoba tutakuwa kimya, maana yake hatutakuwepo.
Kwa hiyo sisi tunaona hiyo hatari ya chama chetu ambacho tumekijenga kupitia chaguzi na chaguzi ndogo. Tuliposhinda uchaguzi mdogo wa Tarime tukaanzisha Operesheni Sangara tukakinyanyua chama, tulipoenda Arumeru Mashariki 2012 tukashinda, chama kinyanyuka kwa nguvu kubwa tena tukaanzisha M4C (Movement for Change), kwa hiyo tunazungumza tunachokielewa, kwamba chama kisiposhiriki uchaguzi kinajichimbia kaburi, tutasubiri niaka mingine 30 kujenga chama kifikie ngazi tulipo leo.
Swali: Tangu wakati kampeni ya No Reforms No Election ilipoanza, mlitaka iweje?
Jibu: Ukimsikiliza wakati aliyekuwa Mwenyekiti Freeman Mbowe alipozungumza Desemba 11, 2024, alisema ikifika wakati wa uchaguzi na hakuna mabadiliko, chama kitafanya uamuzi sahihi.
Swali: Uamuzi gani?
Jibu: Huo ni uamuzi wa vikao, kwa hiuo warudi kwenye vikao wahsauriane. Kama tumekata tamaa ya mabadiliko warudi kwenye vikao. Lakini mimi naona hawajakata tamaa ya mabadiliko. Juzi Mwenyekiti wetu (Tundu Lissu) ambaye ni mwenyekiti wa Kituo cha Demokrasia Tanzanoia (TCD), aliongoza kikao na akasema walikubaliana halafu maazimio yao watayaanduika wampelekee Mheshimiwa Rais.
Maana yake kuna jitihada bado zinaendelea. TCD wanachama wake ni pamoja na CCM na alikuwepo Makamu Mwenyekiti wa chama hicho (Bara), Stephen Wasira. Sasa mwenyejkiti wetu amesema wamekubaliana maazimio yao halafu wataalndika wampelekee Mheshimiwa Rais. Inawezekana kuna vitu wamekuabliana kuhusu hayo mabadiliko.
Ndio maana tunataka wakati jitihada hizo zikiendelea, chama nacho kiendelee kujiandaa, kwa sababu hatimaye mnaweza kukuta mabadiliko yametokea halafu hamjajiandaa, hivyo tunatahadharisha kwamba twende na yote mawili.
Swali: Wiki iliyopita viongozi wa Chadema waliitisha makada wanaotaka kutia nia ili wazungumze, ninyi mbona hakufika?
Jibu: Maoni yetu tuliyaandika Katibu Mkuu aliyapokea na Mwenyekiti Lissu akiwa pale, alijibu baadhi ya maoni yetu, ndio maana leo tukaamua tuyaweke yote hadharani ili watu wajue tulipeleka nini.
Kwa sababu wanaanzisha dhana kwamba hawa ni kundi la waasi, kwa hiyo tunataka wajue tulichopeleka nini, je ni uasi au ni mawazo mbadala.
Ni kweli hatukwenda pale kwa sababu ya kauli za mwenyekiti, makamu mwenyekiti, kauli za Godbless Lema zilikuwa zinatutia hofu. Mtu anasema kama mna mawazo mbadala ondokeni kwenye chama, ninyi ni vibaraka wa CCM. Sasa unatuita sisi ni vibaraka wa CCM halafu unatuita tuje tufanye nini? Tuje tushauriane nini wakati umeshatupa majina mabaya?
Swali: Sasa kama meshapewa majina mabaya, kwa nini tena mmepeleka mapni kwa maandishi?
Jibu: Sisi tuliona pale aliteleza na ndio maana tumeandika tukiamini kwamba aliteleza, kwamba siku nyingine usije ukaita watu halafu kabla hawajaja ukawa umeshawapa majina. Ndio maana tuliandika ili zibaki kwenye rekodi za chama na tulisaini mmoja mmoja, hazikusainiwa na mtu mmoja akaghushi saini.
Swali: Kama ilikuw ani maoni tu, kwa nini mmeanzisha kundi nje ya chama ambalo halitambuliki kwa katiba ya chama?
Jibu: Chama kina makundi mengi sogozi, nikikuonyesha kwenye simu yangu. Yapo ya Chadema Family na wanachangiana fedha. Hata chama chenyewe, wametupa petition wagombea tukasainishe wananchi milioni 15. Kwa hiyo ni utaratibu tu wa chama.
Kwa hiyo, chama kinayatambua hayo makundi ya Tehama na ndio maana taarifa za chama tunaletewa kwenye makundi, taarifa za katibu mkuu zinaletwa. Kwa hiyo sisi kuanzisha kundi sio kosa, yapo Zaidi ya 1,000.
Swali: Chama kikikataa maoni yenu mtachukua uamuzi gani?
Jibu: Tutaendelea kubaki Chadema, sisi ni wanachama. Chama kikikataa ushauri tutapima.
Swali: Au mtakwenda kugombea?
Jibu: Suala la kwenda kugombea, sisi bado ni watia nia, michakato ya kugombea bado, ila kutia nia tunaendelea kama walivyo watia nia wengine ambao bado wako ya chama. Hata wale waliokwenda makao makuu bado ni watia nia.
Swali: G55 ina ugomvi gani na Maria Sarungi?
Jibu: Sisi tumesema tunachoona kwamba anaingilia mamlaka za chama. Anapoandika kwamba chama kisema aliyeitisha hicho kikao ni nani wakati viongozi wakuu wako field, tunataka atuletee majina ya hao wanaotaka ubunge. Yeeni Katibu mkuu ameitisha kikao cha wagombea wake, yeye anahoji kama nani?
Tunajua uhusiano wake na baadhi ya viongozi, tunajua harakati anazofanya ndani ya chama, sisi sio wajinga. Tulikuwa kwenye chama na bado tuko kwenye chama. Tunachokitahadharisha chama, kisiruhusu makundi ya nje ya chama kuanza kukiendesha chama kwa rimoti.