Utaratibu wa vyeo JWTZ

Utaratibu wa vyeo JWTZ

Sasa wee umesema unauzeufu na mazingira ya jeshi halafu unakuja kuuliza watu ambao wengi Ni leymen.
Nadhani wee ungetiririka Sasa huo uzeufu wako.maana tunajua hata Kama wewe siyo mwanajeshi basi uliwauliza wanajeshi wenyewe.akiwemo na mwenyeji wako.
 
Mimi ni raia ila nilibahatika kuishi kambini kama miaka 20 iliyopita maana Mzee wangu alikuwa mwanajeshi hivyo kidogo nina ufahamu wa juu juu na mambo madogomadogo ya wanajeshi wetu.

Ninachojua kuhusu vyeo ni kwamba askari akishaanza na V begani basi ni ngumu kufika kwenye nyota sana sana ataishia kuwa Sir meja au kolokolo 1 & 2, pia form vi waliofanya vizur au graduates wa vyuo ndio wanaruhusiwa kwenda Monduli kutafuta nyota.

Kitu ninachoomba kufahamishwa inakuwaje form iv anaingia jeshini anafika mpaka kuwa koplo wa Jeshi Kisha baadae anaenda Monduli kutafuta nyota?
Nanga mkubwa wewe unaufahamu gani kuhusu JWTZ
 
Captain, kwa utaratibu upi alipanda mpaka kufika hicho cheo?
Ishu ni elimu kijana.

Anaweza akawa aliingia na form four pengine akifanya kazi kwa miaka 6 huku ndani ya miaka 6 hiyo akijiendeleza kwa diploma mpaka kufika degree.

Pengine sasa alipata bahati ndani ya miaka minne ya kazi yake akaenda cheo cha coplo huku pengine anaanza degree.

Aliporudi coplo akaendelea na degree,alipomaliza degree akasajili cheti chake kazini kikatambulika na jeshi wakamtambua kama msomi.

Sasa kama jeshi limemtambua kwamba coplo fulani ana degree unadhani kuna kikwazo gani vyeo vya elimu vikija na yeye asiwemo katika watakaoenda somea nyota ?
 
Ishu ni elimu kijana.

Anaweza akawa aliingia na form four pengine akifanya kazi kwa miaka 6 huku ndani ya miaka 6 hiyo akijiendeleza kwa diploma mpaka kufika degree.

Pengine sasa alipata bahati ndani ya miaka minne ya kazi yake akaenda cheo cha coplo huku pengine anaanza degree.

Aliporudi coplo akaendelea na degree,alipomaliza degree akasajili cheti chake kazini kikatambulika na jeshi wakamtambua kama msomi.

Sasa kama jeshi limemtambua kwamba coplo fulani ana degree unadhani kuna kikwazo gani vyeo vya elimu vikija na yeye asiwemo katika watakaoenda somea nyota ?
Nimekuelewa vizur mkuu mm nilikuwa nadhani once ukishapata vii basi cheo cha mwisho ni WO.
 
Urio hana degree wala diploma wala form six lakini luteni.Wako vijana jeshini wana degree wengi na sio officers. Bahati/Michongo/Dili lolote lawezekana
 
Nimekuelewa vizur mkuu mm nilikuwa nadhani once ukishapata vii basi cheo cha mwisho ni WO.
Sidhani kama inakuwa hivyo,kwenye majeshi ukiwa na elimu unapanda vyeo haraka kuliko kusubiri vyeo vya wakati ufike.

Pengine jeshini ili uwe koplo kiwakati basi inatakiwa uwe umetimiza miaka mfano 5 na usiwe umeshtakiwa ndo unaweza kwenda cheo cha kopulo.

Ila wakati huo hio pengine mtu aliyeingia na masters akafanya kazi miaka mitatu tu akaenda nyota yake anakuwa amepiga hatua kubwa kuliko angesubiri cheo cha wakati ambacho kinaenda kwa utaratibu,japokuwa na hivi vyeo vya elimu navyo vina bahati yake ila ukiwa na elimu hata kama cheo huna basi mshahara wa slimu yako unapata.

Sijui kwa nini askari wengi hawasomi kuongeza elimu
 
Sidhani kama inakuwa hivyo,kwenye majeshi ukiwa na elimu unapanda vyeo haraka kuliko kusubiri vyeo vya wakati ufike.

Pengine jeshini ili uwe koplo kiwakati basi inatakiwa uwe umetimiza miaka mfano 5 na usiwe umeshtakiwa ndo unaweza kwenda cheo cha kopulo.

Ila wakati huo hio pengine mtu aliyeingia na masters akafanya kazi miaka mitatu tu akaenda nyota yake anakuwa amepiga hatua kubwa kuliko angesubiri cheo cha wakati ambacho kinaenda kwa utaratibu,japokuwa na hivi vyeo vya elimu navyo vina bahati yake ila ukiwa na elimu hata kama cheo huna basi mshahara wa slimu yako unapata.

Sijui kwa nini askari wengi hawasomi kuongeza elimu
Sio miaka tu na, kozi za uongozi (Jnr/Snr)
 
Kwa waliopita jeshini kuna kitu kinaitwa "baba kanituma" kwa wanaofahamu hiyo, hata hawatashangaa ngonjera za Luteni Urio
 
Back
Top Bottom