Utaratibu Ufuatwe Baina ya Twiga Cement na Tanga Cement

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
May 16, 2020
1,898
943

MBUNGE JUDITH KAPINGA ASISITIZA UTARATIBU UFUATWE BAINA YA TWIGA CEMENT NA TANGA CEMENT

Mbunge wa Viti Maalmu Vijana Kupitia Kundi la Vijna, Mhe. Judith Kapinga jana tarehe 04 Mei, 2023 amechangia Bungeni suala la Twiga Cement kuinunua Tanga Cement katika hoja ya bajeti ya Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Baishara iliyosomwa na Waziri Mhe. Dkt. Ashatu Kijaji

"Kigezo kikubwa ambacho Mahakama ya Ushindani wa Kibiashara (FCT) imetuongoza tukifuate katika sakata la Tanga Cement kununuliwa na Twiga Cement ni kigezo cha utawala wa soko kwamba nani atauza zaidi, ukichukua hisa za Tanga Cement na Twiga Cement kwa pamoja yatauza asilimia 52 katika soko, na inatuonesha kuwa kanda nne kati ya tano kubwa zitatawaliwa na kampuni hizi mbili kubwa" - Mhe. Judith Kapinga, Mbunge Viti Maalum kupitia kundi la Vijana

"Tume ya Ushindani wa Kibiashara na Haki (FCC) wamefanya utafiti na wana taarifa zinazoonesha kwamba kampuni ya Twiga Cement na Tanga Cement zikiungana kwa pamoja zitapelekea utawala wa soko kwa asilimia 35" - Mhe. Judith Kapinga, Mbunge Viti Maalum kupitia kundi la Vijana

Ni jambo la heri kampuni ya Scancem (kampuni yenye hisa nyingi katika kiwanda cha Twiga Cement) inataka kununua hisa za Afrisam (kampuni yenye hisa nyingi katika kiwanda cha Tanga Cement) lakini mgogoro ulianzia pale ambapo kumejiridhisha kwamba Twiga Cement na Tanga Cement wakiungana wanazidi utawala wa soko kwa 35" - Mhe. Judith Kapinga, Mbunge Viti Maalum kupitia kundi la Vijana

"Sababu ya sheria ya ushindani kuweka taratibu ni kudhibiti soko dhidi ya ushindani, kuhakikisha walaji wanapata bidhaa na bidhaa ni lazima ziwe stahimilivu katika soko. Tusipohakikisha taratibu zinafuatwa linakuwa ni jambo ambalo linazua maswali mengi sana" - Mhe. Judith Kapinga, Mbunge Viti Maalum kupitia kundi la Vijana

"Hakuna mwekezaji anayekatazwa kununua hisa za kampuni yoyote, ishu kubwa ni kwamba taratibu ambazo tumejiwekea ni lazima zifuatwe" - Mhe. Judith Kapinga, Mbunge Viti Maalum kupitia kundi la Vijana

"Sheria ya Ushindani inasema wazi kabisa kwenye makubaliano yoyote ambayo yanachagiza kuathiri soko kwa maana ya ushindani au yanajikita katika kuharibu ushindani ni makubaliano ambayo hayakubaliki kisheria" - Mhe. Judith Kapinga, Mbunge wa Viti Maalum kupitia kundi la vijana

FvSLVXdWwAEUFaO.jpg
 
Kwanini kila mmoja asiachiwe aendelee kufanya biashara yake na kuongeza ushindani na ufanisi?
 
Wanunue tu,

Kama hao wakipandisha bei ya saruji zao, kuna viwanda vingine vya saruji, tutatumia saruji zao...
 
NILIWAHI KUGUSIA SEHEMU HILI SAKATA LA TWIGA KUNUNUA TANGA CEMENT. Nianze kusema kuwa hii sekta ya Cement ni non regulated sector japo ni sector muhimu sana kwa ujenzi wa Taifa.Cement ni moja kati ya mahitaji muhimu kwa kwa ujenzi wa nchi hii na kuna mahali haina mbadala(Substute).Unaporuhusu watu wachache watawale soko nanuzalishaji wa cement ni hatari sanaa, uuzwaji wa Tanga kwa Twiga Cement Unamaanisha kwamba unapunguza wazalishaji sokoni kuwa wachache zaidi hivyo kupelekea umiliki wa soko hulia,Maana yake ni kwamba TWiga atakua anaamua azalishe kiasi gani kwa muda gani maana viwanda ni vyake.Tanzania tunaviwanda vikubwa vinne.Dangote cement,Twiga,Mbeya na Tanga Cement.Kuruhusu Twiga kununua Tanga Cement ni shida kubwa inamaana Tanga itakua chini ya Twiga na wazalishaji watakua watatu sio wanne tena,Hatari ya Upangaji Bei itatokea.Upangaji Bei utaiweka nchi katika wakati mgumu na kuathiri shughuli za kiujenzi kwa serikari na wananchi moja mmoja.VIpi Dangote akiinunua Mbeya Cement? Ikumbukwe kuwa Tanga Cement Ndio Kiwanda pekee chenye malighafi kubwa zaidi na nyingi kuliko vyote katika ukanda wa afrika mashariki,Najiuliza Unakuaje anapata hasara?Hapa kuna harufu ya usimamizi mbovu
 
Back
Top Bottom