Utapeli

CPU

JF-Expert Member
Jan 13, 2011
3,863
686

Kijana mmoja anayesoma katika chuo cha kimoja kilichopo huko maeneo ya Uwanja wa ndege alipata dhahama inayotia uchungu sana maeneo ya Posta.

Mkasa wenyewe ulianza hivi:

Kijana huyo alikuwa anasubiri daladala ili awahi kurudi chuoni maeneo ya posta mpya. Mara akatokea mama mwenye heshima hivi ana mtoto ambaye ana dalili za kuumwa. Akamwomba kijana simu yake ili ampigie mumewe pengine kumweleza mtoto mgonjwa. kijana akasema simu ina shilingi 600, mama akamsisitizia kuwa haitotatosha ila anaomba aweke laini yake ya simu na kijana akakubali. Mama akapokea simu akatoa laini ya kijana akaweka laini yake na kupiga na kisha kumrudishia simu kijana. Kijana hakuangalia kama laini iliyowekwa ni yake au la...... Kosa kubwa!

Mara usafiri wa daladala ukafika kijana akaingia na baada ya kuanza safari abiria mmoja akasikika kaibiwa simu. Kijana aliyekuwa naye, yaonekana ni mwizi mwenziwe, baada ya kutafuta chini ya kiti akashauri wajaribu kuipiga na ndipo simu ya kijana msamaria huyu ikatoa mlio. Wale vijana wakaanza kumpiga kipigo cha mbwa mwizi wakidai kaiba simu na kulazimisha kuichukua kutoka kwa kijana kwa nguvu. Kwa busara za mzee mmoja aliyekuwa ndani ya gari lile walifanikiwa kufika kituo cha polisi na polisi bila kuuliza wala kupokea maelezo ya kijana wakamnyan'ganya kijana simu na kuwapa wale vijana waliodai simu imeibiwa na wakaondoka. Vijana wale walikuwa wakifanya kila wanaloweza kijana yule asijieleze.

Baadaye, ndipo maskini kijana wa watu akaanza kuwaeleza Polisi kilichotokea. Polisi wakabaki mdomo wazi, na kujaribu kutoa maneno ya kuashiria samahani. Lakini tayari alikuwa na majeraha kichwani na simu yake halali kabisa ikiwa imeibwa . . . .
 
lol maskini ya Mungu kweli dunia si mbaya bali walimwengu ndo wabaya!
 
lol maskini ya Mungu kweli dunia si mbaya bali walimwengu ndo wabaya!

Naona hata wanaodai mwisho wa dunia unakaribia itabidi tuanze kuwafikiria kuwa wanasema ukweli kiasi fulani
 
Mimi yamewahi nikuta kama hayo na siku hizi mtu nisiyemfahamu akitaka msaada namuelekeza kituo cha polisi tu akaupate huko
 
Mimi yamewahi nikuta kama hayo na siku hizi mtu nisiyemfahamu akitaka msaada namuelekeza kituo cha polisi tu akaupate huko

Hahahahah . . . hata ukiambiwa ana mgonjwa mahututi??
 
Hahahahah . . . hata ukiambiwa ana mgonjwa mahututi??

Itabidi ampe namba ya monchwari kabisa...lol. Ila hali ya sasa inafanya mtu bora uwe na roho mbaya kusave shingo yako kuliko kujidai una huruma. Hakueleweki kabisa....
 
inauma sana lisikie ivyo ivyo kwa mwenzako ila ss imefika mahali inabidi tuwe makatili mana ujui unayetaka kumsaidi ni kweli anaitaji msaada au msanii
 
Polisi na ulinzi shirikishi ni kama mbinu za kusaidia matapeli tu bora kila mtu aishi kivyake na shida zake.
 
inauma sana lisikie ivyo ivyo kwa mwenzako ila ss imefika mahali inabidi tuwe makatili mana ujui unayetaka kumsaidi ni kweli anaitaji msaada au msanii

Kuna watu wengine hupenda kuonja hata sumu, ili mradi athibitishe kuwa inaua! Hasa wasomi wenzangu ndo wanaongoza kwa kuwa na hiyo kasumba
 
Itabidi ampe namba ya monchwari kabisa...lol. Ila hali ya sasa inafanya mtu bora uwe na roho mbaya kusave shingo yako kuliko kujidai una huruma. Hakueleweki kabisa....

Hivi ubinadamu tumeupeleka wapi??? Kitu gani hasa kinatufanya tuwe mashetani na makatili kiasi hichi ambacho hata SHETAKI mwenyewe anaogopa hii mbinu???!!! Atakushangaa umeijuaje???!!!
 
Kumsaidia mtu nisiemjua barabarani ni big noo!Bora nionekane mbaya kuliko kujisabashia matatizo kwa kujifanya nna huruma!Yalishanikuta..kurudia tena siwezi!
 
Back
Top Bottom