ALAF wawe wanatoa matangazo ya maagent wao mara kwa mara ili wale waliowafukuza wasiwe wanatapeli watu. Na hilo la maagent kujazana hapo makao makuu na kusumbua wateja litafutiwe dawa maana mpaka baadhi ya wafanyakazi wanakujengea mazingira magumu huku wanakushawishi wakuunganishe na hao maagent waliopo pale ili mzigo utoke mapema. Lakini kuna haja gani ya kuwa na agent wakati wanaweza kuwa na ofisi ndogo ndogo pamoja na godown dogo kila wilaya kwa ajili ya kupokea oda. Mbona ofisi yao iliyopo JOSAM HOUSE Mwenge ipo vizuri tu japo haina godown. Kwa unayeenda kununua bati pale ofisini ALAF wewe usiwape nafasi maagent wewe komaa kila kitu kiende kiofisi kwa sababu hata ukichelewa bati zako utazipata zikiwa na vipimo sahihi na idadi kamili uliyolipia hata kama zitzachelewa kidogo kupatikana.
Tahadhari nyingine kwa unayetaka kupaua ukiepuka mtego huo hapo juu chunga sana fundi wako anayepaua. Baada ya kupiga mbao zote akifanya mahesabu ya idadi ya bati zinazotakiwa chukua hayo mahesabu kanunue bati zote mwenyewe. Halafu hakikisha unasimamia mwenyewe (ikiwezekana kama ni mfanyakazi omba likizo kabisa) au weka mtu wako unayemwamini asimamie fundi awe anapiga bati moja moja. Kama fundi hana roho ngumu ikifika nusu lazima akimbie kazi maana huchelewi kukuta bado una mzigo wa bati za kutosha hata nyumba mbili. Ukizubaa tu hachelewi kubandika bati mbili mbili pamoja kwa sababu anajua mchezo alioucheza kwenye mahesabu ya ununuzi wa bati. Hapo ndio watu huwa wanashangaa vipi nyumba ndogo tu imepauliwa kwa gharama kubwa au sawa na nyumba nyingie kubwa. Kwa wale mnaojifanya mko bize mnamwachia fundi apime mwenyewe anunue bati mwenyewe apaue mwenyewe mkae mkijua mnapaua nyumba mbili au hata tatu kwa wakati mmoja.
Tahadhari nyingine kwa unayetaka kupaua ukiepuka mtego huo hapo juu chunga sana fundi wako anayepaua. Baada ya kupiga mbao zote akifanya mahesabu ya idadi ya bati zinazotakiwa chukua hayo mahesabu kanunue bati zote mwenyewe. Halafu hakikisha unasimamia mwenyewe (ikiwezekana kama ni mfanyakazi omba likizo kabisa) au weka mtu wako unayemwamini asimamie fundi awe anapiga bati moja moja. Kama fundi hana roho ngumu ikifika nusu lazima akimbie kazi maana huchelewi kukuta bado una mzigo wa bati za kutosha hata nyumba mbili. Ukizubaa tu hachelewi kubandika bati mbili mbili pamoja kwa sababu anajua mchezo alioucheza kwenye mahesabu ya ununuzi wa bati. Hapo ndio watu huwa wanashangaa vipi nyumba ndogo tu imepauliwa kwa gharama kubwa au sawa na nyumba nyingie kubwa. Kwa wale mnaojifanya mko bize mnamwachia fundi apime mwenyewe anunue bati mwenyewe apaue mwenyewe mkae mkijua mnapaua nyumba mbili au hata tatu kwa wakati mmoja.