Eustadius
Member
- Aug 17, 2013
- 10
- 21
Habarini za leo wadau,
Eneo la Buguruni Chama ni eneo ambalo lililozoeleka na umaarufu sana kwa biashara ya mbao pamoja na utapeli kwa wateja wanaofanyiwa katika kununua mbao kwa kutumia ule mchezo wa kupunguza zile futi kamba wakati wa upimaji wa mbao (waliowahi fanyiwa huu mchezo wanajua).
Zaidi ya hapo, kwa sasa kuna makampuni yanayojifanya ni mawakala wa kampuni ya ALAF Tanzania kumbe ni matapeli tu wanaoishia kuchukua hela za watu kwamba watawapatia mabati toka ALAF na mwishowe kuishia kuwazungusha wananchi hao.
Mimi mwenyewe imenitokea kusumbuliwa na hao matapeli wanaojiita dealers wa ALAF kumbe sio na kibaya zaidi nilielekezwa kwa huyo anayejiita wakala wa ALAF na mtu ambaye tunaheshimiana SANA. Kumbe uwakala wake umeishasimamishwa na amebaki mjini kusumbua na kutapeli watu. Hivi ninavyo andika ujumbe huu tapeli huyo yupo ndani katika Kituo cha Polisi Buguruni na maneno anayoongea muda huu hayaeleweki kabisa kuhusiana na mzigo wangu.
#mytake
1.Nawashauri endapo unahitaji bati kutoka ALAF ni bora kwenda kiwandani moja kwa moja maana haizuiliwi kabisa unakwenda unatoa order yako na kupatiwa bidhaa yako ndani ya muda mfupi sana kuliko kuendelea kusumbuka na hawa matapeli.
Hili nimeligundua baada ya kwenda kulalamika na kuwaeleza kuhusiana na maneno aliyokuwa ananiambia huyo aliyekuwa anajiita wakala kumbe sio.
Tuchukue tahadhari katika hili.
2. Kampuni ya ALAF ifanye chapisho kuwabainisha mawakala wao wote na kuwabainisha wote ambao ni matapeli wanaotumia jina lao kwani wanawajua na hizo kesi zinakwenda kwao kila leo.
Sent using Jamii Forums mobile app
Eneo la Buguruni Chama ni eneo ambalo lililozoeleka na umaarufu sana kwa biashara ya mbao pamoja na utapeli kwa wateja wanaofanyiwa katika kununua mbao kwa kutumia ule mchezo wa kupunguza zile futi kamba wakati wa upimaji wa mbao (waliowahi fanyiwa huu mchezo wanajua).
Zaidi ya hapo, kwa sasa kuna makampuni yanayojifanya ni mawakala wa kampuni ya ALAF Tanzania kumbe ni matapeli tu wanaoishia kuchukua hela za watu kwamba watawapatia mabati toka ALAF na mwishowe kuishia kuwazungusha wananchi hao.
Mimi mwenyewe imenitokea kusumbuliwa na hao matapeli wanaojiita dealers wa ALAF kumbe sio na kibaya zaidi nilielekezwa kwa huyo anayejiita wakala wa ALAF na mtu ambaye tunaheshimiana SANA. Kumbe uwakala wake umeishasimamishwa na amebaki mjini kusumbua na kutapeli watu. Hivi ninavyo andika ujumbe huu tapeli huyo yupo ndani katika Kituo cha Polisi Buguruni na maneno anayoongea muda huu hayaeleweki kabisa kuhusiana na mzigo wangu.
#mytake
1.Nawashauri endapo unahitaji bati kutoka ALAF ni bora kwenda kiwandani moja kwa moja maana haizuiliwi kabisa unakwenda unatoa order yako na kupatiwa bidhaa yako ndani ya muda mfupi sana kuliko kuendelea kusumbuka na hawa matapeli.
Hili nimeligundua baada ya kwenda kulalamika na kuwaeleza kuhusiana na maneno aliyokuwa ananiambia huyo aliyekuwa anajiita wakala kumbe sio.
Tuchukue tahadhari katika hili.
2. Kampuni ya ALAF ifanye chapisho kuwabainisha mawakala wao wote na kuwabainisha wote ambao ni matapeli wanaotumia jina lao kwani wanawajua na hizo kesi zinakwenda kwao kila leo.
Sent using Jamii Forums mobile app

