Utapeli.bayport.mikopo

Utapeli.bayport.mikopo

Nililipa 617 na machenchi hivi kwa mwaka mzima nadhani ilikua fair maana niliingiza 1,500,000 kwenye kuku

Kwenye vikoba yetu!kwa mkopo huo ningelipa 550!,na hiyo faida tungeigawana cc wenyewe!!huko hamnipati ng'oooooo
 
Ieleweke mimi sifanyi marketing wala sio mfanyakazi wao, nina biashara ya kuku na ninaona jinsi wapinzani wanavyonisema vibaya kwa wateja japo wananielewa na wanakuja kwangu kuniambia, nilivyoona comments na threads zenye maudhuu kama yenu nikaona ni upinzani unawasumbua tu kwamba mnatafuta wateja, note kwamba sijataja madhaifu ya kampuni zingine japo mi ni mkopaji mzoefu na ninafahamu mapungufu mengi kwa hiyo state your argument acheni kejeli, nimetoa observation aliyetari kuthibitisha si wapo kwann tusumbuane
Wewe Ni meneja wao WA tawi, Bayport sio pa kukopa, Ni balaa
 
6b55dc31f8ef3faa90e98ab9985b7066.jpg
 
Hawa jamaaa bayport wanaenda kukopa pesa benk alafu na wao wanakopesha so wanapiga cha juu.Ukichukua mkopo kwao wafwaaaaa
 
Hawa bayport riba zao kubwa sana,,yani unakatwa tuuuu,,mkopo hauishi,,ictoshe wafanyakaz wao wana system ya kubadili badili namba za simu
 
Mi bado siamni kama mikopo ya financial institution kama Bayport kwa kuwa wenyewe hakuna biashara wanayofanya zaidi ya kukopesha pia na wenyewe wanaenda kukopa kwenye institution kubwa kama CRDB na bank zingne so riba unalipa mara mbili ya kwao na wanayolipa walipokopa ni wizi wizi tu.Kinachowadanganya wafanyakazi ni ule urahisi wake wa kupata mikopo.Kama una shida ya mkopo ni bora uende kwenye institution kubwa kuliko hv vinavyojiita bayport.
 
Yaan wewe hiyo 1.5M na 500k ndio ujue bado wanakuvuta vuta, kimbembe kopa kuanzia 3M ndio utajua sasa Bashite anajisikiaje kumbumbuluka kuwa na vyeti vya Paulo!
 
Mbwa hao uthisubutu, kwanza ukishajaza mkataba watafanya ujanja usibaki nao hata kwa dawa. Pili ukikopa mil 2 watakuambia unalipa mil lets say 4.2 kwa miaka kadhaa, siku salary slip ikija utakuta ni milioni 6, ukirud kuomba mkataba wabakupiga chenga tushatuma makao makuu.

Kulipa deni kwa mkupuo pia hawataki
Najiuliza serikali kupitia bank kuu wanakaaje kimya kwa wizi huu
 
Nimeamini bayport imeliza wengi,kama hawajatajirika basi hawajikutajirika.Miye huwa sipendi kuwasikia kabisa kuna jamaa yangu alitaka kuacha kazi sababu ya hawa jamaa baada ya kupata mkopo hewa
 
Mbwa hao uthisubutu, kwanza ukishajaza mkataba watafanya ujanja usibaki nao hata kwa dawa. Pili ukikopa mil 2 watakuambia unalipa mil lets say 4.2 kwa miaka kadhaa, siku salary slip ikija utakuta ni milioni 6, ukirud kuomba mkataba wabakupiga chenga tushatuma makao makuu.

Kulipa deni kwa mkupuo pia hawataki
Najiuliza serikali kupitia bank kuu wanakaaje kimya kwa wizi huu
Pole mkuu,kwa kweli hivi vitaasisi mshenzi vimewajeruhi watanzania wengi sana kuna hawa bayport,letshego bank abc hawafai hata kidogo na wanatumia mwanya wa watanzania wengi sio watafiti sana pale linapokuja suala la pesa mtu akiambiwa anapewa milion tano haulizi atarejesha kias gn kila mwezi(monthly deductions),marejesho jumuishi na riba(total liability) na pia hawadai mikataba na hapa ndipo watumishi wengi hupigwa kipigo kitakatifu, juzi kuna dada amekuja ofisin analia anaomba tufanye loan buyback kutoka bayport nikampigia hesabu nikamwambia dada hapa baada ya kununua hili deni utabakiwa na 50k akaniambia hata nisipobak na chochote itafaa zaidi kuliko kubaki na hawa vibaka nilimuonea huruma sana inaumiza mno,lakini yote hayo huchangiwa na watumishi wengi kutokuwa na upembuzi yakinifu pale linapokuja suala la mikopo sijui nisema ni tamaa ama ndio kukurupuka maana haingii akilini mtumishi amechafua salary slip
Tunakopesha ltd-50k
Letshego -33.6k
Bayport -67k
Credit plutnum -102k

Huku chini anaweka bank mbili kubwa watumishi msipoachana na hivi vitaasisi mshenzi mtaichukia sana mikopo.
 
Nililipa 617 na machenchi hivi kwa mwaka mzima nadhani ilikua fair maana niliingiza 1,500,000 kwenye kuku
====================================================================================================

Hiyo ni sawa na riba ya asilimia 23.5% kwa mwaka (
 
Nililipa 617 na machenchi hivi kwa mwaka mzima nadhani ilikua fair maana niliingiza 1,500,000 kwenye kuku
====================================================================================================
Hiyo ni sawa na riba asilimia 23.5% kwa mwaka (FLAT INTEREST RATE); ambayo ni sawa na riba asilimia 40.88% kwa mwaka (REDUCING BALANCE RATE)

Viwango hivyo vya riba ni vikubwa mno !!!!!!
 
Nililipa 617 na machenchi hivi kwa mwaka mzima nadhani ilikua fair maana niliingiza 1,500,000 kwenye kuku
====================================================================================================
Hiyo ni sawa na riba asilimia 23.5% kwa mwaka (FLAT INTEREST RATE); ambayo ni sawa na riba asilimia 40.88% kwa mwaka (REDUCING BALANCE RATE)

Viwango hivyo vya riba ni vikubwa mno !!!!!!
 
Poleni sana, watumishi na wajasiriamali mliokopa kwnye hizi taasisi binafsi za fedha.

KINACHONISIKITISHA SANA SERIKALI KUPITIA HII WIZARA ISIYO NA HURUMA NA WANANCHI BALI MASLAHI YAO KWANZA/WIZARA YA FEDHA. Hakuna hatua wanachukua.

Hizi taasisi ni wakopaji kama wewe kwny taasisi kubwa za kifedha kama Bank.
Yaani wewe na wakina Bayport ni wateja sawa wa NMB au CRDB.

Lakini kwa kuwa wao ni taasisi wanakopesheka zaidi yako. Wakishapata mkopo mkubwa wanakuja mtaani wanakopesha kidogo kidogo hata kwa mwezi mmoja huku riba ikiwa ni ile ya Bank JUMLISHA riba yao yenye faida Yao.
Kwa hali hiyo ni LAZIMA RIBA ZAO ZIWE KUBWA MNO almost mara mbili ya zile za Bank.

Hapa wizara ya fedha ilibidi kuweka muongozo na si kukaa kimya huku wananchi wakiteseka na madeni makubwa.

Ikumbukwe tu Riba tu za Bank zenyewe kwa nchi hii bado ni kubwa mno pamoja na kujinadi wamepunguza mpk 17%.
Sehemu watu mlipo chezeshewa dish ni kuongeza miaka mpka 5 au 7 ya kurejesha Deni. Hakika nafuu haipo ila wengi hamfahamu hilo, kwa kuangalia makato kidogo ya kila mwezi.
Riba zinatakiwa kubakia asilimia isiyozidi 9%.
Maisha haya magumu kwa nchi maskini zote ni kutokana na madeni yenye Riba kubwa. Umaskini huu hautaisha kwa Miaka mingi ijayo.

Nafikiri kila kukicha mnasikia serikali ikikopa tena madeni makubwa Sana, hapo Riba hiyo yote ni yetu sisi Raia wa chini, TUTAPATA TAABU SANAAAA.

Ushauri wangu usikope BAYPORT na ndugu zake wala watu Binafsi. Tumieni Vikoba kwa wafanyabiashara wadogo, SACCOS kwa wafanyakazi na wafanyabiashara wakubwa. Anzisheni mifuko ya kusaidiana na Harambee za Mitaji.

TATIZO KUBWA WATANZANIA NI WATU WA KUTAKA HELA YA HARAKA, KWA MFANO MNALENGO MOJA KWA NINI MSIJIUNGE WATU 50 MKAJIPA MUDA HATA WA MIEZI 6, YA KUCHANGIA NA KUKUZA MTAJI WENU AMBAO HAUTAKUWA NA RIBA YA MTU VILEVILE BIASHARA YENU IKIANZA MNAKUWA MMESHAJIPATIA AJIRA YENU YA KUDUMU NA VIZAZI VYENU??

TAFAKARI HILO ANZA SASA.
 
Back
Top Bottom