Babu Ubwete
Senior Member
- Jan 26, 2008
- 169
- 29
Imefika wakati sasa tuangalie kama nchi na kila mmoja kwamba Fani ya Utangazaji wa redio na luninga sio kila binadamu anaiweza, ni sawa na kuendesha Talk show sio kwamba kila mtu anaweza kuendesha . Watangazaji wetu hapa bongo land wengi hawana kipaji na hawana uelewa wa kujifunza kutangaza vizuri, Naomba nitoe mfano kuna dada mmoja ameanzisha Talk show yake kutangaza hawezi kabisa anarudia maneno, time management hana, Redio kama Clouds ndio imejaa watangazaji wasiotulia katika kutangaza. hebu tujifikirie na kama hatuwezi tukae pembeni tuwaachie waliojaaliwa kipaji cha kutangaza.