Utajisikiaje ikikukuta hii?

Utajisikiaje ikikukuta hii?

twitybird

Member
Joined
Apr 15, 2013
Posts
69
Reaction score
8
Habari zenu wana jamii? Naomba kuuliza hivi pale unapokutana na rafiki yako wa muda mrefu kwa mfano umesoma nae sekondari baada ya miaka kadhaa kupita mnakutana kwenye daladala mnasalimiana vizuri na kubadilishana mawazo mawili matatu, ikatokea kwamba yeye ndie anaeanza kushuka kwenye kituo halafu anatoa noti ya sh elfu kumi na kumkabidhi konda. Konda anamuuliza nikate nauli ya wawili? Bila kusita rafiki yako huyo anasema kata mmoja. Ilinitokea juzi kati daaah kiukweli roho iliniuma na kujisikia aibu japokua sikuwa nategemea kulipiwa nauli il a ubinadamu jamani..nimeamini kuna watu wana roho ngumu .
 
Ndiyo maana yake! Kila mtu ana tabia yake binafsi anaijua mwenyewe.
 
Hahahaha huyo ni kauzu zaid ya dagaa au na wew shule ulikuwa humpend unamfichia sabun na kumfanyia vtuko vingne vya shule???
 
Habari zenu wana jamii? Naomba kuuliza hivi pale unapokutana na rafiki yako wa muda mrefu kwa mfano umesoma nae sekondari baada ya miaka kadhaa kupita mnakutana kwenye daladala mnasalimiana vizuri na kubadilishana mawazo mawili matatu, ikatokea kwamba yeye ndie anaeanza kushuka kwenye kituo halafu anatoa noti ya sh elfu kumi na kumkabidhi konda. Konda anamuuliza nikate nauli ya wawili? Bila kusita rafiki yako huyo anasema kata mmoja. Ilinitokea juzi kati daaah kiukweli roho iliniuma na kujisikia aibu japokua sikuwa nategemea kulipiwa nauli il a ubinadamu jamani..nimeamini kuna watu wana roho ngumu .

Bora konda asingemuuliza wangapi.
 
Huo ni upuuzi mwingine!! Kwani wakati unatoka nyumbani kwako hukuwa na nauli yako? Unajua anapoenda? Vipi kuhusu bajeti? Mulipanga wote? Hebu musilete ujamaa wenu wa kijima, kwa nini wewe hukumwambia asilipe ili ulipe wewe? Au wewe ni kilema uliyestahili kusaidiwa????????
 
jambo la busara ilitakiwa umwambie asilipe ili ulipe wewe,hizi habari za kusikilizia ulipiwe nauli kisha usipolipiwa unalalama sio nzuri,hata hivyo hukujua kajipangaje,kutoa 10000 hakumaanishi kua huyo bwana yuko vizuri mfukoni.
kutoa ni moyo wa mtu na ni hiari ata kama tumekaa siti moja tunafahamiana na stori nyingi.
 
Mmmh ila sijui kwanini huu uzi umenichekesha,,,lol!
 
Afadhali alikuwa mkweli, kuliko angekulipia nauli kinafiki na nkubaki na sononeko moyoni


Bado kwa upande mwingine yawezekana alihofia kukulipia kwakuwa ungemhisi anakunyanyasa kisaikolojia kama angekulipia, lakini pia inategemea mliishi nae vipi huko nyuma
 
Nimesoma majibu yenu wote nashukuruni sana ila ukweli tuliishi vizuri na sio kwamba Nilikua nategea ili nilipiwe hiyo nauli ...kuna vitu vingine bhana huwa vina muafect mtu kisaikolojia kweli iliniuma maana kila mtu aligeuka kutuangalia aliposema KATA mmoja.....
 
Habari zenu wana jamii? Naomba kuuliza hivi pale unapokutana na rafiki yako wa muda mrefu kwa mfano umesoma nae sekondari baada ya miaka kadhaa kupita mnakutana kwenye daladala mnasalimiana vizuri na kubadilishana mawazo mawili matatu, ikatokea kwamba yeye ndie anaeanza kushuka kwenye kituo halafu anatoa noti ya sh elfu kumi na kumkabidhi konda. Konda anamuuliza nikate nauli ya wawili? Bila kusita rafiki yako huyo anasema kata mmoja. Ilinitokea juzi kati daaah kiukweli roho iliniuma na kujisikia aibu japokua sikuwa nategemea kulipiwa nauli il a ubinadamu jamani..nimeamini kuna watu wana roho ngumu .

We VIP now dayz KILA mtu na budget zake....usishangae
 
Cdhani kama alifanya kosa unajua haya mambo lazima tufike mahali tubadilike huyo rafiki yako hakujua kama mtakutana kwenye daladala akulipie nauli ikiwa na maana kuwa haupo kwenye bajeti yake n sawa kabisa,pili mlishazungumza inatosha sanaa watz tubadilike mambo ya eti tumekutana bar kwa kuwa hatujaonana mda mrf basi nikununulie bia au nikulipie daladala wakati kwenye walleti yangu hujaingia kibajeti hiyo hapana kabisaa,
Tunabakia na mtazamo huohuo ndio maana wengi wetu maendeleo yanatuacha kwa kutaka kuvurugiana bajeti ata kama litasemwa suala la n utamaduni wetu upi wa kulipiana nauli kisa tumekutana ndani ya daladala hapana bhanaa ishi kulingana na bajeti yako halisi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom