Habari zenu wana jamii? Naomba kuuliza hivi pale unapokutana na rafiki yako wa muda mrefu kwa mfano umesoma nae sekondari baada ya miaka kadhaa kupita mnakutana kwenye daladala mnasalimiana vizuri na kubadilishana mawazo mawili matatu, ikatokea kwamba yeye ndie anaeanza kushuka kwenye kituo halafu anatoa noti ya sh elfu kumi na kumkabidhi konda. Konda anamuuliza nikate nauli ya wawili? Bila kusita rafiki yako huyo anasema kata mmoja. Ilinitokea juzi kati daaah kiukweli roho iliniuma na kujisikia aibu japokua sikuwa nategemea kulipiwa nauli il a ubinadamu jamani..nimeamini kuna watu wana roho ngumu .