Mfamaji
JF-Expert Member
- Nov 6, 2007
- 6,629
- 1,951
rafiki yetu karugendo,kama una ushahidi wa ufisadi wake wewe tuletee ili tumshughulikie
Hivi unaishi Tanzania au Kosovo? Mtu asiyejua kama Lowasa ni fisadi basi hajui kama uanaishi au nusu mfu
rafiki yetu karugendo,kama una ushahidi wa ufisadi wake wewe tuletee ili tumshughulikie
Lowassa anapiga kote kote nguvu ya fedha ni nguvu ya giza hupendwa na na wengi kwani hakuna kuabudu Mungu tena bali vito, thamani na fedha
prudencekarugendo@yahoo.com 0784 989 512
Ndugu prudence;uchambuzi wako hauko realistic pia napata wasiwasi na uelewa wako. Watu kumtuhumu mtu si kigezo cha kuwa mtu huyo tayari ni mkosaji na hasa ukizingatia mazingira ya kisiasa nchi Tanzania. Kwani wewe hujawahi kushutumiwa na watu maishani mwako?je ni kweli kuwa yote ambayo watu waliokaribu na wewe wanasema juu yako ni ya kweli? unasema hata wewe ukiambiwa uthibitishe ufisadi wa lowassa huwezi, iweje uyatake makanisa yamchukulie yeye kama fisadi?. Tuthibitishie ufisadi wa lowassa,toa takwimu za utajiri wake unaodai anawao kiasi cha kuitikisa nchi. au wivu ndo unakusumbua?. Nani kakuambia kuwa pesa zote katika harambee anatoa yeye?.kuhamasisha watu wachangie maendeleo ni kosa?. Nakushauri ndugu yangu kuwa na mawazo huru. zingatia hoja zaidi kuliko mihemko ya watu.
Mimi binafsi namkubili lowassa kwa kila anachoongea ni realistic.nani hajui kuwa elimu ni tatizo Tanzania?.matatizo yanayowakabili machinga yapo wazi. Ishitoshe katika nchi inayozinagatia utawala wa sheria,mahakama ndo chombo kilicho eligible kumtia mtu hatiani. Hayo yote juu ya lowassa ni wazi ni chuki,wivu na kutapatapa. The guy is charismatic and seem to be serious na ana uchungu na matatizo ya watu.
Ushauri kwa Lowassa
Mheshiwa (lowassa) usivunjwe moyo wa watu wenye mawazo finyu.Endelea kuhimiza watu katika maendeleo. Watapigana lakini hawatakushinda.Ushawishi wako na kukubalika kwako ni wazi kuwa Mungu yupo upande wako. Pia watu wote makini wapo na wewe. Stay blessed.
Mpendwa wangu, mimi si Karugendo ila nna maswali mengi ya kujiuliza juu ya ufadhili huu:
1. Utajiri huu wa mpendwa Lowasa unatokana na vyanzo vipi? Rejea: Karibu kila Jumapili anachangia mamilioni somewhere, kanisani na sasa misikitini huku akitaja kuwa yeye na marafiki zake. Hao marafiki ni watu halisi? Hatujawahi kumsikia amewatambulisha. Vyanzo hivyo ni halali kiasi gani? Mapato (rather faida) yatokanayo na vyanzo hivyo ni makubwa sana basi! Analipia kodi kiasi gani?
2. Motive ya uchangiaji: Ni kweli kwamba motive ni uchangiaji kutaka kupambana na umaskini au lack of resources zilizopo au kuna jambo nyuma ya pazia? Ikumbukwe huyu mtu ameshahusishwa na urais mwaka 2015...Je, hizo si kampeni za kisiasa makanisani, misikitini na kwa disadvantaged? Hii si manipulation?
3. Binafsi namheshimu sana Lowasa kama ambavyo nakuheshimu ndugu unayemtetea. Wasiwasi wangu nakuja pale tunapotumia vibaya nafasi na kujitetea eti hatuuoni umasikini wa waendesha bodaboda/wamachinga. Umasikini huu tunauona leo? kwa nini leo na si jana?
Watanzania wenzangu natoa wito tufike mahali pa kuiita dhambi dhambi bila ya kujali imefanywa na nani. Tusije tukafika mahali pa kuiuza nchi kwa misingi ya njaa ya leo...tukumbuke tuna watoto...historia itakuja kutuhukumu tusipotenda haki na haki tupu. Hakuna sababu ya kumhukumu mtu mdogo na kumwacha mkubwa
unaweza kutuambia sababu 1,2,3 za lowwasa kujiuzulu?
km alikuwa hana tuhuma,ni waz anawajua mafisad wenzake,mbona hakuwataja?
ww hata umpende vip,watz wote wanajua lowasa FSD,hafai kuongoza hata nyumba 10!
siyo makanisani tu mpaka misikitini pesa haramu zimeingizwa kazi kweli kweli yetu macho watanzania wanao sahau mara kwa mara
Mbona watushangaza? huyo Mh anaweza kuwa fisadi au sio fisadi sisi watu wa kawaida hatujui utajiri alio nao Lowassa, labda atuambie yeye kama hana akaunti huko Uswisi. La msingi ni kuwa alikuwa waziri mkuu na akashindwa kuwajibika! Ndio sababu akaachia ngazi. Lile la kuwafukuza wazung wa DAWASCO alifaulu lakini la Richmond likamshinda. Sasa kujipitisha pitisha makanisani na misikitini linatutatiza kwani yeye kama mwanasiasa anachotafuta huko ni nini? Apande kwenye majukwaa atuambie wananchi la Richmond lilinishinda lakini mkinipa kura nitakuwa Raisi wenu mchapa kazi na sitarudia maksosa kama yale ya Richmond.
Talanta aliyo nayo ni kama ya Mh Lyatonga Mrema!
Lowassa anapiga kote kote nguvu ya fedha ni nguvu ya giza hupendwa na na wengi kwani hakuna kuabudu Mungu tena bali vito, thamani na fedha
Kavishwa joho maalumu na BAKWATA au hujasikia?? Tafuta uzi upo humuhumu. Aibu kwa BAKWATA