Utajiri ni ile hali ya kumiliki mapesa mengi na kuwa na mali nyingi, utajiri ni mzuri kwa kuwa unakupa uwezo nguvu mamlaka sifa na umaarufu!kwa kifupi Utajiri ni kitu chema.
Watu wengi hutafuta utajiri kwa njia mbalimbali halali na haramu wao wanachotaka ni utajiri ili waweze kutimiza ndoto zao nyingi.
Sasa kuna wakati mtu hutafuta utajiri kwa njia za mkato hapa nazungumzia kwa njia za ushirikina na uchawi.
Utajiri huu ni mzuri na huja haraka lakini ukiwa na masharti mengi lakini kubwa likiwa ni kutoa kafara la damu kwa kuangamiza roho.
Unapoingia kwenye utajiri huu mwanzoni utafurahia na masharti utayaona mepesi lakini kadiri siku zinavyozidi kwenda mambo hubadilika na tabu huanzia hapo.
Mwanzoni utaambiwa toa kafara la damu ya kuku baadae itakuja mbuzi, halafu itafuatia ng'ombe na mwishowe itakuja binadamu mmoja na hatimaye kwa makundi.
Hii yote ni kutaka kulinda utajiri wako usiporomoke na ukivunja masharti kila kitu kinaharibika .
Kuna pia masharti ya kujisaidia kulala kula kuvaa na hata matumizi ya vitu mbalimbali. Mwanzoni inakuwa ni rahisi tu kwenda sambamba nayo lakini mbeleni mambo hubadilika hasa pale watu wanapoanza kuhoji hiki au kile.
Wote tunajua jamii ya watu wenye ulemavu wa ngozi inavyoteketea kutokana na waganga wa kienyeji kuwaaminisha wateja wao kuwa viungo hivyo vikichanganywa na dawa nyingine huleta utajiri bahati nguvu na uwezo! Kuna zaidi ya waganga 300 kwenye mahabusu na Magereza mbalimbali wenye kesi zinazowahusisha na mauaji ya albino.
Jamani utajiri wa masharti ya namna hii haufai na mwishowe huwa na anguko kuu tunashuhudia visa vya kila aina kuhusiana na utajiri wa namna hii lakini kila uchao watu hawakomi kuendelea kuutafuta.
Hakika dunia inaumwa.
Umekariri ... Siri ya utajiri ni ubahili. !
SISI wakinga hatutumii uchawi bali maarifa tu. Kwanza utakubaliana na mimi kwamba wakinga ni wachapa kazi, hili halina ubishi it is there for all to see.
Wakinga sio wahongaji, wakinga hawavai nguo za bei mbaya, hawanunui magari ya kutanulia, hawanywi pombe za matanuzi, hawali nyama, wakisafiri hawali njiani maana kuna ule mkate wao wa kikinga ambao husafiri nao, kanisani wanatoa kiasi kidogo tu. Kwanini wasilimbikize mali ? Hutegemei kuona tajiri mbondei kwasababu tabia zao ni kinyume kabisa na za wakinga. Kama kuna mtu alishawahi kuona tajiri wa kibondei aingie pm nimtumie vocha anipigie.
Teh teh teh mbavu zangu...eti kujifyokonyoa naniliu haa haa JF!Mamantilie ndio wanatulisha uchafu mwingi sana anadanganywa na mganga wake kuwa ukitaka uvute wateja wengi pikia chakula maji uliyoogea bila sabuni, basi utakuta mama na mdishi mkubwa wa maji hadi bafuni akifika huko atajitumbukiza mzimamzima na kujisugua na kujifyokonyoa mpaka kwenye naniliu halafu akitoka hapo maji yale machafu na uchafu wote ule ndio atayatumia kupikia vyakula na utakuta watu wamepanga msururu kwenye chakula chake wakikisifia kuwa ni kitamu sana HERI WANGEJUA
Mamantilie ndio wanatulisha uchafu mwingi sana anadanganywa na mganga wake kuwa ukitaka uvute wateja wengi pikia chakula maji uliyoogea bila sabuni, basi utakuta mama na mdishi mkubwa wa maji hadi bafuni akifika huko atajitumbukiza mzimamzima na kujisugua na kujifyokonyoa mpaka kwenye naniliu halafu akitoka hapo maji yale machafu na uchafu wote ule ndio atayatumia kupikia vyakula na utakuta watu wamepanga msururu kwenye chakula chake wakikisifia kuwa ni kitamu sana HERI WANGEJUA
Mkuu huyu hawajui wakinga anawasikia,atuulize tuliokua nao na kuishi nao
namie mapataka hapo, inakuwaje?Kwani naomba kuuliza hivi uhusiano wa pesa na hivyo vitu ni UPI?
Yaani kifo cha kiumbe hai na mie kuwa tajiri ni process gani inafanyika?
tang'ana;
Sijui ni mimi tu sikukuelewa. Huamini nini katika uchawi? Huamini kuwa kuna uchawi au huamini kutajirika kiuchawi? Vyote hivyo vipo kwani hata vitabu vitakatifu vimeandika habari za uchawi na wachawi.
Pia usiache kuamini kuwa kuna mali zinapatikana kiuchawi ila tatizo lake ni kuwa, mali zile ni za mda mfupi nazo hupotea na kukuacha katika aibu kuu.
Mali za kichawi hazirizishwi mtu mwingine. Ukifa na kila kitu chafa na weye. Kafara hutolewa kila siku, kama bungeni ndo usiombe. Watu waliwahi kwenda kuweka vitu mle kiasi kwamba hata cct camera zile hazikumshika jamaa akiwa kazini. Si wakumbuka enzi za Mh. Six??? Uchawi upo, na wachawi wapo ila they live for a short tyme na hizo raha zao.
Utajiri wa kweli hauji kwa kujinyima wala kwa uchawi ila kwa kukaa sawa sawa na mapenzi ya Mungu akubariki kwani ametuahidia baraka.
Wapo watu tunawajua, hawaruhusiwi kuvaa suruali, viatu, kulala kwenye nyumba zao ikifika saa 12 jioni ni mwisho wake kuingia ndani ya nyumba aliyoijenga. Kuna mwingine jirani yetu tu hapa, saa 11 alfajiri, lazima akanye njia panda kila siku. Mateso gani haya jamani??
Tafuta kwa njia nzuri na utatajirika tuuu. Mungu anipe utoshelevu na amani vyanitosha
Umekariri ... Siri ya utajiri ni ubahili. !
You are too Ghetto.We kweli ni Pasta mcharuko!
All the Glory to our Lord Jesus.well said be blessed
Ila wangetoka kaskazini ndo matajiri halali wakitoka kusini sio halali toa evidence ya uchawi kwa Wakinga
Mamantilie ndio wanatulisha uchafu mwingi sana anadanganywa na mganga wake kuwa ukitaka uvute wateja wengi pikia chakula maji uliyoogea bila sabuni, basi utakuta mama na mdishi mkubwa wa maji hadi bafuni akifika huko atajitumbukiza mzimamzima na kujisugua na kujifyokonyoa mpaka kwenye naniliu halafu akitoka hapo maji yale machafu na uchafu wote ule ndio atayatumia kupikia vyakula na utakuta watu wamepanga msururu kwenye chakula chake wakikisifia kuwa ni kitamu sana HERI WANGEJUA
Na kwenye haya masharti kuna
-ya kulala na mamaako/babaako/mwanao
-kulala na mtoto mdogo/mchanga.ndio maana kuna habari nyingi sana za watu kubaka vitoto vidogo kabisa tena vingine vya miezi tuu