Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe, ameitaka taasisi ya utafiti masuala ya kisiasa, kijamii na kiuchumi nchini ya Synovate kutoa matokeo ya mgombea na chama kinachoongoza kupendwa na wananchi katika kipindi hiki.
Mbowe alitoa kauli hiyo jana katika Viwanja vya Isanja, wilayani ya Siha, mkoani Kilimanjaro, wakati akimnadi mgombea urais wa Dk. Willibrod Slaa, mgombea ubunge na udiwani.
Alisema tayari chama hicho kina matokeo kamili yaliyofanyiwa kazi na taasisi hiyo hivi karibuni, ambayo yanaonyesha Dk. Slaa, anaongoza kwa asilimia 44, huku mgombea wa CCM, Jakaya Kikwete akifuatia kwa asilimia 41.
Alisema baada ya Synovate kukamilisha matokeo hayo, CCM ilipata taarifa, ikaamua kuwazuia kuyatangaza, kwa madai kuwa yatakidhalilisha chama hicho.
wadau, ndo maana tunasema hii threat iliyotolewa na utaki unaacha ina ukweli
Habari zilizopatikana ndani ya kikao cha siri kati ya vigogo waandamizi wa usalama wa taifa,Kikwete na Kinana wiki iliyopita zimedokeza kwamba JK amepokea report inayoonyesha kura za Dk Slaa atakazopata october 31 2010.
Mpashaji wa habari amebainisha ya kwamba baada ya JK kupewa tathimini hiyo hakuamini alichoambiwa, zaidi aliongea kwa kiingereza maneno mawili '' Is it?''.
Hii ni taarifa fupi iliyotolewa wiki tatu zilizopita ikulu jijini dar es salaam ikiwa ni mpango wa usalama wa taifa kukamilisha awamu ya kwanza ya utafiti wao kwa baadhi ya mikoa ya kanda ya ziwa, kati, pwani na kaskazini. Machache yameibwa kwenye taarifa hiyo:
Mara: Dr Slaa 59.7%
Mwanzar Slaa 58.3%
Kigomar Slaa 52.7%
Singida: Dr slaa 34.7%
Shinyanga: Dr Slaa 43.2%
Kilimanjaro: Dr Slaa 51.7%
Arusha: Dr Slaa 47.1%
Manyara: Dr Slaa 53.8%
Tangar Slaa 46.2%
Dar es Salaam: Dr Slaa 66.4%
Geita: Dr Slaa: 62.7%
Kagera: Dr Slaa 48.2%
Dodoma: Dr slaa 42.4%
Tabora: Dr Slaa 57.6%