Adharusi
JF-Expert Member
- Jan 22, 2012
- 14,493
- 7,417
Ulaji wa supu ya pweza,karanga mbichi,mihogo mibichi na mbata kwa madai kwamba vinaongeza urijali kwa wanaume kumeelezwa kuwa ni dhana potofu inayostahili kupigwa vita kwa kuwa haina uhusiano kati ya urijali wa mwanaume na vyakula hivyo.
Kauli hiyo imetolewa na Dk.Cuthbert Maendaenda wakati akitoa mada yake kwenye semina ya wahariri iliyofanyika Morogoro iliyojadili nafasi ya mwanaume katika kuleta mabadailiko katika jamii juu ya afya ya uzazi na jinsia.
Alisema katika miji mingi kwa sasa supu ya pweza huuzwa ambapo wauzaji wamekua wakinadi kama msaada wa kurejesha heshima ndani ya jamii.
Alisema ufanyaji mapenzi unaathirika na vitu vingi na jamii lazima kuangalia ukweli huo ili kuwa na watu wanaojiamini katika mapenzi na wale ambao wana matatizo kupata ushauri wa kidaktari
Kauli hiyo imetolewa na Dk.Cuthbert Maendaenda wakati akitoa mada yake kwenye semina ya wahariri iliyofanyika Morogoro iliyojadili nafasi ya mwanaume katika kuleta mabadailiko katika jamii juu ya afya ya uzazi na jinsia.
Alisema katika miji mingi kwa sasa supu ya pweza huuzwa ambapo wauzaji wamekua wakinadi kama msaada wa kurejesha heshima ndani ya jamii.
Alisema ufanyaji mapenzi unaathirika na vitu vingi na jamii lazima kuangalia ukweli huo ili kuwa na watu wanaojiamini katika mapenzi na wale ambao wana matatizo kupata ushauri wa kidaktari