Utafiti: Kwanini walimu wamefika hapa walipo leo

Utafiti: Kwanini walimu wamefika hapa walipo leo

Huu utafiti una ukweli ndani yake. Lakini mleta mada amekuwa "too general" hajasema amehoji walimu wa kada gani! Je ni chekechea, shule za msingi, sekondari au vyuo vya ualimu? Mimi naamini sio walimu wote ni wanyonge kiasi hicho. Hata mifumo ya nchi, serikali yetu, Sera ya elimu na mambo kadha wa kadha vimechangia Taaluma hii ya ualimu ambayo ndo taaluma yenye watumishi wengi kuliko zote; kuonekana ni taaluma isiyo na maana.
 
kuna mambo madogo madogo ambayo poa yanasababisha walimu kuzalaulka ikiwemo weledi wa kutenda kazi zao.kwa mfano hiki kilichoandikwa hapa sio research report bali ni malalamiko na mtazamo wa mtoa mada.

kanuni za kuandika ripoti zinajulikana,kwanza hujasema title ya utafiti wako,research methodology,objectives,target population, literature review nk.kwa ufupi huu sio utafiti ila ni malalamiko kama kawaida yenu walimu.

kama walimu hamuwezi kufanya hata research ndogo kama hii msitegemee jipya kutoka serikalin.lieni tu.

Kwa ninavyowajua wa TZ wenzangu kama mleta mada angeweka hapa the whole research report, say 150 pages, asingepata hata mtu mmoja, hata wewe ungesema too long, weka summary etc. Nimpongeze mtoa mada kwani ameweka executive summary ambayo ni timilifu.
 
walimu tunajizalau wenyewe ati tunawaogopa maafisa wa juu utazani wao ni miungu acheni woga wa kijinga uo..ati kisa usipo waogopa na kuwanyenyekea utanyimwa semina na warsha au kusimamia mitihani.huu upuuzi nimeuona kwa walimu wengi TANZANIA hii...ATI mwalimu anamkimbia afisa eliimu wakikutana njiani...wewe mwalimu wa namna hiyo ukapimwe akali...umesahau ya kuwa binadam haogopwi bali anaheshimiwa pale atakapo jiheshimu...hivi walimu waoga huwa wanafundishwa vyuo gani HAPA TANZANIA????...
 
Utafiti wako Uko sahihi Kwa 90% ,kada ya ualim inapuuzwa sana hasa Kwa wenye level hizi tatu,,certificate, diploma na degree
 
Ukitaka udharaulike au ukose demu...jutambulishe kama ww mwalimu
 
Mtoa mada umeeleza vizuti sana juu ya mentality iliyojengeka juu ya walimu hii ni kwa waalimu wenyewe kutojiamini na kwa jamii nzima na serikali kwa ujumla lakini yote ya yote tatizo hapa ni maslahi kwa maana ya mshahala pamoja na posho, kwani uzoefu unaonyesha taaluma yenye maslahi makubwa kwa maana ya mishahara ndiyo yenye kuheshimika zaidi kwa mfano afya,jeshi,uhasibu na uhandisi. ILI TAALUMA YA ELIMU IHESHIMIKE NI KUIBORESHEA MASLAHI TU NA SI VINGINEVYO....
 
Mtalaumu Maafisa Elimu na viongozi wa Serikali, hakuna kitengo kilaini kuongoza kama Walimu. Nina ushahidi wa kutosha....
 
tena nasema mimi ni mwalimu wala sikufeli anayesema walimu wote wamefeli hayupo sahihi..ILA NASEMA HAKUNA YEYOTE KATIKA WATU ATAKAYE NI SUMBUA AWE ANACHEO AU LAAH..NAJIAMINI NA KUJIKUBALI TENA SIKUBAHATISHA...KWANGU WAJIPANGE SAAANA...KARIBUNI KILINDI
 
Huwa najiuliza hawa walimu waoga kama kunguru wamesoma vyuo gani hapa tz vinavyofundisha uoga na kutojiamini?????????????????????????????????????????????????????/
 
Kwa ninavyowajua wa TZ wenzangu kama mleta mada angeweka hapa the whole research report, say 150 pages, asingepata hata mtu mmoja, hata wewe ungesema too long, weka summary etc. Nimpongeze mtoa mada kwani ameweka executive summary ambayo ni timilifu.
asante ndugu yangu kwa kunisaidia maana pengine kakoment kwa kusoma title tu
 
UTAFITI KWANINI WALIMU TUMEFIKA HAPA TULIPO
Wanajamvi ni muda wa miaka kama mitatu nimekuwa nikifanya utafiti binafsi juu ya maendeleo ya walimu nchini Tanzania na kikubwa niliangalia kwanini walimu wapo hivi walivyo leo?.. utafiti huu umeshirikisha baadhi ya walimu walioko kazini, waliostaafu, wanachuo baadhi (wanaosomea ualimu) walimu wapya baadhi na wanfunzi baadhi, kwa haraka haraka nimewahoji watu zaidi ya 150 kwa kipindi hicho nilikuwa mwanafunzi na nikaendelea hadi wakati nimeajiriwa rasmi kama mwalimu na wale niliowakuta kazini pia nilipata nafasi ya kuwauliza? hata hivyo sikuweza kuandika utafiti huu kutokana na sababu mbali mbali

Kuna sababu nyingi zilizosababisha walimu kufikia hapa tulipo sasa?. Kwa nyakati tofauti nimekutana na walimu na mara kadhaa wanachuo mbali mbali wanaosomea ualimu nimejifunza kuwa tupo leo kutokana na sababu zifuatazo..

1. (a) Walimu wenyewe:
Wakati nikifanya utafiti huu nimegundua wapo walimu ambao huona aibu hata kujitambulisha mbele za watu kuwa wao ni walimu? nilijaribu kuwauliza walimu kadhaa swali hili ?unajisikiaje kuwa mwalimu? Ulichagua mwenyewe kazi hii au imetokea tu baada ya kukosa kazi ile uliyoipenda??
Majibu niliyokutana nayo yanasikitisha, idadi kubwa ya walimu walisema kuwa hawakuipenda kazi hiyo na wengine wamediriki kusema wana mpango wa kubadilisha fani! Sasa kama wewe mwenyewe huijali na huipendi taaluma yako nani atakujali? Hebu walimu tubadilike kwa kujiamini kuwa kazi yetu ni bora na ni nzuri JIHESHIMU KWANZA NDIPO UHESHIMIKE!

(b) chama cha walimu Tanzania (CWT)
Chama hiki kilikuwa na malengo mazuri lakini chama hiki hakina madhumuni na nia ya moja kwa moja kumkomboa mwalimu wa Tanzania zaidi ya kutumia mgongo wa walimu wengi kunufaisha walimu viongozi wachache.. katika hili 90% ya walimu wapo tayari kujitoa CWT hata leo.. katika utafiti wangu huu walimu wengi (nikiwemo mimi) nimeipinga CWT hadharani kuwa haina mchango wowote mkubwa kulinganisha na vyama vingine vya wafanyakazi! Mara mia bora chama cha madereva Tanzania kuliko cwt!

(c) maafisa Elimu
Huu ni ukweli mchungu kuwa baadhi ya maafisa elimu wengi ndio wanaosababisha walimu kuonekana vituko mbele ya jamii.. unaweza kwenda ofisini kufuatilia madai yako lakini afisa akakuwekea zengwe utadhani hela analipa yeye! Lakini maafisa wengine hubania walimu kwenda kujiendeleza kimasomo kuhofia nafasi zao! Kitu kinachouma zaidi maafisa hawa WENGI walikuwa walimu lakini ndio wanaongoza kwa kukandamiza walimu wenzao!
(d) walimu hawana umoja
Walimu hawana umoja! Utakuta mwalimu aliyelipwa madai yake hawezi kumsaidia Yule ambae bado! Walimu hawana sauti ya pamoja! Wanaweza kukubaliana wasiingie darasani na wakasaini lakini wengine wakaingia kufundisha! Na yote hii ni kufeli kwa cwt katika kuunganisha walimu kuwa kitu kimoja.
2 .JAMII
Kutokana na walimu kujidharau wenyewe jamii pia huambukizwa tabia hiyo na ndio maana utakuta mzazi anamuuliza motto wake ?mwanangu umekosa hata ualimu?? hapa akimaanisha ualimu ndio ?the cheapest? kuliko ajira zote, na wengine wakaenda mbali kudai kuwa kazi ya ualimu ni kazi ya watu waliofeli! Nakumbuka wakati Fulani nilifundisha shule moja ya English medium darasa la tano siku moja nikawauliza kama wanatamani kuwa walimu, nilishangaa wakikataa kabisa na hata wale wachache waliokubali walichekwa na wenzao! Nilipowauliza kwanini wakasema eti mishahara midogo hahahahaha! Sasa jiulize mtoto mdogo anajua eti walimu wanalipwa kidogo? nikaishia kuwauliza ?who told you??


3.VIONGOZI WA SERIKALI
Baada ya hayo yote viongozi wa serikali wamewafikisha walimu hapa walipo leo hii, walimu wametumika kama daraja kupitisha viongozi wengi ambao hutoa ahadi kedekede lakini baada ya hayo huwadharau walimu! Ni mwalimu yupi asiyekumbuka kauli ya Madam Mwantum Mahiza? Ni mwalimu yupi aliyesahau kauli ya Raisi kikwete uchaguzi wa 2010? Sasa kauli za kuvunja moyo kwa walimu zinapotolewa na viongozi wakubwa ndipo sasa hata wanafunzi wa chekechea wanachukia ualimu!

MAPENDEKEZO:
1. Mwalimu jiheshimu mwenyewe kuanzia unavyokula, unavyovaa, unavyoongea, usipende maisha ya shida shida sana hata kama mshahara ni mdogo? kuna kipindi nilienda halmashauri nikakutana na mwalimu kavaa yebo yebo anaenda kuchukua mshahara! Sasa hapa watoto wakikuona watatamani kazi yetu kweli!!?

2. Walimu tupiganie kujitoa CWT hebu tuanze kwanza kupinga 2% ya mshahara kuliwa kienyeji na wahuni wachache.
3. Walimu tuwe na umoja, umoja uanzie shuleni, kasha kwenye kata zetu kisha wilaya kasha nchi nzima, wakuu wa shule msiwe kimbele mbele kuwachongea walimu wenu halmashauri kuweni wa kwanza kuwatetea hebu cheki.. Rais JPM kaenda ofisi ya fedha kauliza wafanyakazi wengine wako wapi kajibiwa wameenda kunywa chai! Lakini mkuu wa shule akiulizwa wako wapi walimu wako wawili atasema ?hata mimi sijui, tena wana siku ya tatu leo hawajaonekana kazini mheshimiwa!?
MWISHO.
Yapo mambo mengi lakini sikuyataja hapa kwa kuhofia uzi huu kuwa mrefu sana na kuchosha watu? hata hivyo nina mpango wa kuchapa makala kuhusu utafiti huu. Nasubiri maoni na mtazamo wenu.
Mwalimu allan
allanclement6@gmail.com

kwa sababu ya viongozi wazur wa serkari hapa kazi tu ccm mbele kwa mbele
 
Kiukweli Uzi nimeupenda na una hoja kali tu!!Nachoweza kusema...Ukiachiachikia mapungufu mengne madogomadogo...bhna tatizo kubwa ni MASLAHI MABOVU(MISHAHARA MIDOGO)

Mi mwenyewe ni mwalimu na hata napokaa kujadili changamoto mbalimbali zinazotukabili waalimu..ishu ni mishahara mibovu,,kukosa posho hata kidogo japokua ualimu ni kazi ngumu yenye shughuli nyingi kama kufundisha,,kusahisha,,kutunga mitihani,,kusimamia,,kuaandaa matokeo n.k...

Waalimu hawapewi kipaumbele kabisa na wanakosa msaada!!Yani Mimi nimeajiriwa ajira mpya 2015 katika halmashauri flani...Tangu Mei lakini.mshahara nimekuja kuanza kupata Mwezi wa 9!!Can u imagin??na nilikua na kila kigezo ikiwemo vyeti na vielelezo vyoote vilivyohitajika!!

Je unadhani Askari polisi,,mwanajeshi,,au daktari anaweza kufanyiwa uhaini kama huu??haya umenlipa mshahara mwezi wa 9 ,vipi mishahara iliopta??Yashakua malimbikizo!!Kulipwa??ni Majaliwa...nimefika kituo cha kazi nakuta watu wanadai malimbikizo tangu mwaka 2012,,hadi leo hii hawajalipwa!!Napataje moyo wa kufanya kazi kwa bidii?Naanzaje kujituma ikiwa serikali hainijali??Lazima nitaondoka kazini mapema kwenda kujitafutia kipato cha ziada Mtaani!!

Serikali haithamini waalimu miaka na miaka!!Hilo lipo wazi!Mwalim wa degree mshahara Laki 5 na...hana posho,,Baada ya miaka 55_60 kazini kw usumbufuu sana Ataambulia milion 60 kqmq pensheni,,Mbunge anaejua kusoma tu na kuandika mshahara milioni 11.8 kwa mwezi,,posho laki 3 kwa siku,,Mkopo wa magari milion 90,,Baada ya miaka mitano bungeni Milioni 238 tena bila usumbufu....

We unategemea kuinuka kwa Elimu kwa Tabaka hilo???Teeeh shida tu...mi mwenyewe michongo ikinyooka naachana na Ualimu!!
 
ni kweli mr adam, but tunarudi pale pale kuwa sisi walimu tunachangia kuonewa, ikiwa hadi leo kuna walimu wanatetemeka mbele ya maafisa elimu, ikiwa hadi leo CWT inaiba pesa za walimu, ikiwa hadi leo kuna kuna walimu wanafanya kazi za kitaifa na hawalipwi kwa wakati, ikiwa hadi leo wapo walimu wanaogopa kudai haki zao kwa kuogopa kunyimwa fursa kama kusimamia mitihani, uchaguzi n.k je huoni serikali nayo haiwezi kuacha kuwadharau na kuwapuuza walimu wakijua kuwa hawataifanya chochote? kama tumeshindwa kuikataa CWT tutaiweza serikali?
 
mshahara wa mwalimu mwenye degree ni sawa na posho ya siku mbili ya mbunge kweli huu unyonyaji hivi huyo mbunge bila mwalimu angefika hapo alipo?
 
Back
Top Bottom