Utafiti: Kupungua kwa viwango vya mbegu za kiume kutasababisha kutoweka kwa binadamu

GTA

JF-Expert Member
Jul 25, 2013
878
649
_97089495_sperm.jpg

Watafiti wanaochunguza matokeo yao tafiti 200 wanasema kuwa upungufu wa kiwango cha mbegu za kiume miongoni mwa Wanaume kutoka Marekani kaskazini, Ulaya, Australia na New Zealand ufikia nusu yake.

Baadhi ya wataalam wanashaka kuhusu matokeo hayo.

Lakini mtafiti bingwa anayeongoza utafiti huo Dkt Hagi Levine anasema kuwa alikuwa na wasiwasi mkubwa kuhusu kile kitakachofanyika katika siku za usoni.

Dkt. Levine ambaye ni mtaalamu wa magonjwa aliambia BBC kwamba iwapo mwenendo huo utaendelea basi huenda binadamu wakatoweka.

Utafiti huo ambao ni miongoni mwa tafiti kubwa ulileta matokeo ya tafiti 185 kati ya 1973 na 2011.

''Iwapo hatutabadili mienendo yetu ya kuishi mbali na kemikali na mazingira yetu ,nina wasiwasi mkubwa kuhusu kile kitakachofanyika siku za usoni''.

Hatimaye tutakuwa na tatizo hususan na uzazi kwa jumla na huenda ikawa kutoweka kwa binaadamu.

Wanasayansi ambao hawakushirikishwa katika utafiti huo wameusifu ubora wake lakini wanasema kuwa huenda ni mapema mno kutoa tangazo hilo.

Dkt. Levina kutoka chuo kikuu cha Hebrew mjini Jerusalem alibaini kupungua kwa asilimia 52.4 ya manii huku asilimia 59.3 ya mbegu za kiume kutoka kwa wanaume kutoka maeneo ya Marekani kaskazini, Ulaya, Australia na New Zealand yakishuka zaidi.
Credit:BBCSWAHILI
 
Back
Top Bottom