Sizinga
Platinum Member
- Oct 30, 2007
- 9,101
- 6,027
Utafiti uliofanywa na vituo bingwa duniani unaonyesha kuwa watu wengi akili(brain) inaanza kupwaya pindi unapofikia miaka 40 na kuendelea. Hii imeushangaza ulimwengu ukioamini kwamba akili ya mtu inapwaya kuanzia miaka 60. Utafiti huu unaonesha kumbukumbu za mtu afikapo miaka 40 zinapungua kwa kadri miaka inavyoongeza 40+, Hii ilijumuisha idadi ya watu 7000, ambao walifanyiwa research na watu wenye aged 40 mpaka 49 ndio walionyesha wanapoteza kumbukumbu zaidi. SOURCE: GAZETI LA KISWAHILI MWANANCHI(Kama sijakosea) MY TAKE: Hapa Tanzania kwa system yetu ya elimu inaonesha watu wengi wenye umri kati ya 15-30, wapo masomoni(mostly 1st degree). Wengi wanaanza kulitumikia Taifa kuanzia miaka 30+ either kuajiliwa au kujiajili...so kuna miaka 10 tu inayobaki wakati akili bado iko fresh ya kulitumikia taifa hili. Hii ni hatari sana kwani kuanzia miaka 40+ na kwa maisha haya ya sasa yenye stress inaonesha kabisa tunapiga hatua 5 mbele na 10 tunarudi nyuma. Je kweli Tutafika??