Imeandikwa kwenye gazeti la Nipashe, Jumanne Novemba 15, 2016 kwa kichwa cha habari "Binadamu ataweza kubadilisha kichwa mwakani", kwamba 'Marekani itaingia katika machafuko yatakayogawanyisha majimbo ya nchi hiyo, ya Kaskazini na Kusini'.
Baba Vanga ni nani?
View attachment 434520
Baba Vanga (alijulikana kama 'the Nostradamus of the Balkans') ni mtabiri, mwanamke, kipofu, mzaliwa wa Strumica, Macedonia. Alfariki miaka 20 iliyopita (1996). Jina lake halisi ni Vangelia Pandeva Dimitrova.
Alipoteza uwezo wake wa kuona akiwa na miaka 12, kutokana na kimbunga kikubwa kilichomkumba akapotea kwa siku kadhaa. Alifariki kwa ugonjwa wa kansa ya titi.
Katika tabiri zake nyingi zilizokuwa sahihi ni kama zifuatazo:
1) Kujiimarisha kwa ISIS
2) Kuporomoka kwa Ghorofa Pacha (Twin Towers).
3) Tsunami ya 2004.
4) Kuongezeka kwa joto duniani(global warming).
5) Rais wa 44 wa Marekani atakuwa mtu mweusi, akaja kuwa Barack Obama, nk
Tabiri zinazosisimua ni kama zifuatazo;
1) Bara la Ulaya halitakuwepo ifikapo 2016, iwapo silaha za kemikali zitatumika. Kinachoendelea barani Ulaya kwa sasa mwelekeo ni kwenye utabiri huo.
2) Waislamu watavamia bara la Ulaya. Hili linaendelea kutokea.
3) China litakuwa Taifa jipya lenye nguvu ifikapo 2018 badala ya Marekani. Akaongezea kuwa mataifa nyonyaji (exploiters) yatanyonywa (exploited).
4) Mwisho wa dunia ni mwaka 3797 ila binadamu watakuwa wamendelea kiteknolojia na kuhamia sayari nyingine. Utafiti kuhusu hili unaendelea kwa kasi na matumaini mazuri.
Kuhusu Marekani kuparaganyika, kinachoendelea huko, baada ya kumchagua Trump kuwa Rais, ni dalili tosha kuelekea huko. Kwa kuwa sikio la kufa halisikii dawa, ni kusubiri tu kama huo utabiri utakuwa kweli.