Utabiri wa Baba mchungaji

Utabiri wa Baba mchungaji

Vaislay

JF-Expert Member
Joined
Jun 26, 2011
Posts
4,532
Reaction score
1,840
Habari wana Jf,

Nashukuru kama wote tumepita salama katika kipindi hiki cha sikukuu, kwa upande wangu ni kama ndoto tu..Nisiwachoshe....

Rafiki yangu kipenzi,amekuwa akimcha Mungu sana na kumlilia Mungu ampe mume kwani akidhani umri umepita/unaenda bila kuwa na mwenza..
Akaamua kwenda kumuona Baba Mchungaji na kumwomba amsaidie kwenye maombi ya kusaka Hubby.Mchungaji akamwambia apeleke majina ya wanaume aliowahi na anaodate nao kwa kipindi hicho,Akapeleka majina matano.
Baba Mchungaji akazama rohoni na kuibuka na Jibu HAKUNA MUME katika majina yale.Dada akapiga chini jamaa aliekuwa nae na kidogo jamaa alikuwa na kauelekeo...

Tisa na Kumi.....:bange:
Baba mchungaji akaibuka na utabiri HATAREEEE....akamwambia nimepata maono unabooongee mume, Tajiri, marafiki zake ni bwana IPP na Azam,yani hapa unagari la M 200 linakusubiri,ukionana nae tu shopping ya Engagement ulaya,Utakutana nae tar 20 mwezi fulani.dada wa watu roho juu usubiri tarehe,wakijitokeza Magarasa,magarasa yanapigwa teke akiamini mume wa roho anakuja..
Hatimae tarehe ikaja....masaa yakaenda ...siku ikaisha ziiiiiii.....siku ya pili,ya tatu,mwezi umeisha....

Ungekuwa wewe ungemfanya nini baba Mchungaji?

ANGALIZO; wanaopiga goti kuomba mahubbitioz angalia na wapi unaenda kuomba msaada.
 
Azidi Kumtegemea Mungu,Huyo Mchungaji sina imani naye
 
Ulimwengu wa leo tunao waumini waliopitiliza. Wamepitiliza kwa kuwa hawasomi neno (wamwemwachia Mchungaji/Padre). Wanaamini kila wanachoambiwa masikini. Wachungaji nao ni watu. kuna wa kweli na wa uwongo pia. Mtu anaweza kuwadanganya kadiri awezavyo (nina visa vingi kwenye hili)

Hakuna miujiza kwenye uhalisia. Mungu anakupa mtu wa kufanana na wewe na anakupa kitu unachoweza kukibeba. Tatizo injili inaelekea kufurahisha watu, wewe utoke from know where ukakae na wafalme kabla hujaandaliwa /hujafinyangwa? Kwenye maandiko sijawahi kuona hiko.. Wote waliokuwa wakubwa kuna hatua walipitishwa kabla. Injili ni uhalisia na sio miujiza.

Pili: Waumini wameaminishwa kuwa ni mchungaji pekee anayeweza kuwaombea ikasikiwa, Hio ilikua zamani. Pazia la hekalu lilipasuka kutoa ACCESS ya mimi na wewe kupaendea patakatifu. Unaendaje hio ni habari nyingine.

Tatu: Mungu ana njia nyingi ''Njia zangu sio njia zenu na mawazo yangu sio mawazo yenu '' na kwenye maandiko tumeona namna mbali mbali alivyojifunua kwa matukio mbali mbali, basi katika hayo tujifunzeni ufanyaji kazi wake..

Tujazwe NENO kwa wingi, vinginevyo tutahangaishwa hadi tukome.. mara njooni mchukue waume, mashamba, safari za ulaya, sijui magari, sijui nyumba.... n.k. ''Mungu si mwanadamu hata aseme uwongo na Anafuatilia NENO lake aweze kulitimiza''... anything out of His WORD ni ya kwetu.

Wachungaji tuwasikilize lakini tuyafanyie reference maneno yao kwenye NENO. vinginevyo ni hatari kwa nyakati hizi kuwa wasikivu WASIOFIKIRI.
 
Ulimwengu wa leo tunao waumini waliopitiliza. Wamepitiliza kwa kuwa hawasomi neno (wamwemwachia Mchungaji/Padre). Wanaamini kila wanachoambiwa masikini. Wachungaji nao ni watu. kuna wa kweli na wa uwongo pia. Mtu anaweza kuwadanganya kadiri awezavyo (nina visa vingi kwenye hili)

Hakuna miujiza kwenye uhalisia. Mungu anakupa mtu wa kufanana na wewe na anakupa kitu unachoweza kukibeba. Tatizo injili inaelekea kufurahisha watu, wewe utoke from know where ukakae na wafalme kabla hujaandaliwa /hujafinyangwa? Kwenye maandiko sijawahi kuona hiko.. Wote waliokuwa wakubwa kuna hatua walipitishwa kabla. Injili ni uhalisia na sio miujiza.

Pili: Waumini wameaminishwa kuwa ni mchungaji pekee anayeweza kuwaombea ikasikiwa, Hio ilikua zamani. Pazia la hekalu lilipasuka kutoa ACCESS ya mimi na wewe kupaendea patakatifu. Unaendaje hio ni habari nyingine.

Tatu: Mungu ana njia nyingi ''Njia zangu sio njia zenu na mawazo yangu sio mawazo yenu '' na kwenye maandiko tumeona namna mbali mbali alivyojifunua kwa matukio mbali mbali, basi katika hayo tujifunzeni ufanyaji kazi wake..

Tujazwe NENO kwa wingi, vinginevyo tutahangaishwa hadi tukome.. mara njooni mchukue waume, mashamba, safari za ulaya, sijui magari, sijui nyumba.... n.k. ''Mungu si mwanadamu hata aseme uwongo na Anafuatilia NENO lake aweze kulitimiza''... anything out of His WORD ni ya kwetu.

Wachungaji tuwasikilize lakini tuyafanyie reference maneno yao kwenye NENO. vinginevyo ni hatari kwa nyakati hizi kuwa wasikivu WASIOFIKIRI.

Wewe ndo unapotosha watu ukimuabudu Mungu katika roho na kweli lazima atakupa haja ya moyo wako haijalishi ni kitu gani inaweza kuwa mme au mke, shamba, kazi, afya njema, Na kama usipomwamini kiongozi wako whether ni Shekhe, Nabii, Mchungaji, Padre actually huwezi kumuamini Mungu pia,
Ushuhuda mimi hapa Mungu kaniinua from zero to hero
 
Wanabidii katika kumtafuta MUNGU lakini si katika Maarifa,

Na watu wangu wanapotea kwa kukosa Maarifa..

Amelaaniwa amtumainie mwanadamu

najaribu kumbuka vifungu vya kumsaidia mhanga.....

soma NENO ishi NENO tenda NENO...usingoje thimuliwa NENO:israel:
 
Wachungaji wa siku hizi hawana tofauti na waganga wa kienyeji...
 
asa kwanini alimpiga chini kaka wa watu wakat alikuwa na uelekeo???? jaman sio kila mambo unamshirikisha mchungaji hata wew mwenyew una uwezo wa kumuomba mungu na mambo yakaenda vizur mweeee masikini dada wa watu kwaio anasubir muujiza??? aiseeer atasubir sana
 
Ulimwengu wa leo tunao waumini waliopitiliza. Wamepitiliza kwa kuwa hawasomi neno (wamwemwachia Mchungaji/Padre). Wanaamini kila wanachoambiwa masikini. Wachungaji nao ni watu. kuna wa kweli na wa uwongo pia. Mtu anaweza kuwadanganya kadiri awezavyo (nina visa vingi kwenye hili)

Hakuna miujiza kwenye uhalisia. Mungu anakupa mtu wa kufanana na wewe na anakupa kitu unachoweza kukibeba. Tatizo injili inaelekea kufurahisha watu, wewe utoke from know where ukakae na wafalme kabla hujaandaliwa /hujafinyangwa? Kwenye maandiko sijawahi kuona hiko.. Wote waliokuwa wakubwa kuna hatua walipitishwa kabla. Injili ni uhalisia na sio miujiza.

Pili: Waumini wameaminishwa kuwa ni mchungaji pekee anayeweza kuwaombea ikasikiwa, Hio ilikua zamani. Pazia la hekalu lilipasuka kutoa ACCESS ya mimi na wewe kupaendea patakatifu. Unaendaje hio ni habari nyingine.

Tatu: Mungu ana njia nyingi ''Njia zangu sio njia zenu na mawazo yangu sio mawazo yenu '' na kwenye maandiko tumeona namna mbali mbali alivyojifunua kwa matukio mbali mbali, basi katika hayo tujifunzeni ufanyaji kazi wake..

Tujazwe NENO kwa wingi, vinginevyo tutahangaishwa hadi tukome.. mara njooni mchukue waume, mashamba, safari za ulaya, sijui magari, sijui nyumba.... n.k. ''Mungu si mwanadamu hata aseme uwongo na Anafuatilia NENO lake aweze kulitimiza''... anything out of His WORD ni ya kwetu.

Wachungaji tuwasikilize lakini tuyafanyie reference maneno yao kwenye NENO. vinginevyo ni hatari kwa nyakati hizi kuwa wasikivu WASIOFIKIRI.

LIKE,LIKE LIKE. Mkuu Tized umemaliza,ni kweli kabisa wakristo wa leo tumekuwa wavivu sana kusoma neno na kuomba tunategemea watu wengne watufanyie matokeo yake tunapewa matango pori.

Neno la Mungu linatuagiza kwamba tumtafute Bwana maadam anapatikana tumuite yu karibu.,lakin ajabu wanadamu wa leo hatuishi kubun njia zetu kinyume na mapenzi yake.

Matokeo ya kutopenda kuomba sisi wenyewe ni kupewa unabii wa uongo,kupewa maji,mafuta,vitambaa,chumvi n.k mwisho wa siku ni kugeuka na kumkejel Mungu kwamba hatendi kumbe tatizo ni sisi wenyewe kutopenda ushirika na Mungu moja kwa moja.
 
Last edited by a moderator:
Sina hamu nao hao nilitabiriwa kujifungua mtoto mpaka jina la mtoto nikapewa.nikapangiwa hadi atakaomshika badala yake mtoto alikufa hata hakuiona dunia.Kiasi kikubwa imani yangu imeshuka saaana.
 
Tatizo wadada mnachagua sana siku hizi halafu mileage ikishasoma ndio mnahaha makanisani.
 
Sina hamu nao hao nilitabiriwa kujifungua mtoto mpaka jina la mtoto nikapewa.nikapangiwa hadi atakaomshika badala yake mtoto alikufa hata hakuiona dunia.Kiasi kikubwa imani yangu imeshuka saaana.
No usiseme hivyo...Endelea kumuomba Mungu tu...Usitegemee kwa mchungaji mana mchungaji ni mtu kama mimi au wewe...Mtegemee Mungu wako,
Kama huyo rafiki yangu ni mpaka amekata tamaa kwasababu akili yake ilitegemea baba mchungaji atende miujiza na sio Mungu
 
Mwadunda. Swali dogo Ukimwabudu kama ulivyosema una haja ya kwenda kuombewa ili Mungu akupe haki zako?

Maana amesema mkikaa ndani yangu nami ndani yenu OMBENI lolote Nami ntalifanya n.k.

Simwekei Mungu mipaka kwamba ila hakuna analofanya nje ya NENO lake. Kama lipo uniambie ntakupa maandiko yake. Ulimwengu tunaouishi umeshaandikwa siku nyingi sana. Yohana ameshaandika yatakayotukia likiwemo la wachungaji feki.. si kweli? Na neno linasema mpinga Kristo na manabii wa uwongo wamekwisha kuwepo? Na neno si linasema tutawajua kwa matunda yao?

Inawezekana uko sahihi sana. Lakini kila kinachotokea kina MSINGI na KUSUDI lake. Na si kama tutakavyo ila ni kwa MAPENZI yake.

Hatumwabudu Mungu kwa kuwa atatupa maisha au mali nyingi (yafaa nini basi mtu aupate ulimwengu wote kisha akaipoteza nafsi yake) ila tunamwabudu Mungu kwa kuwa TUNAMPENDA. (MUNGU NI PENDO)

NB: TUNAPASWA KUMTEGEMEA MUNGU Na MUNGU PEKEE. Baadhi yetu wana funguo za tuyatakayo twaweza kutumia zao au tukatafuta funguo zetu. Ila kwa kutumia zao haitupi kibali cha kuweka tumaini letu kwao. (Ole wake amtegemeaye mwanadamu.....)


Wewe ndo unapotosha watu ukimuabudu Mungu katika roho na kweli lazima atakupa haja ya moyo wako haijalishi ni kitu gani inaweza kuwa mme au mke, shamba, kazi, afya njema, Na kama usipomwamini kiongozi wako whether ni Shekhe, Nabii, Mchungaji, Padre actually huwezi kumuamini Mungu pia,
Ushuhuda mimi hapa Mungu kaniinua from zero to hero
 
Last edited by a moderator:
Kweli kabisa everlenk. Neno linasema "watu wanaangamia kwa kukosa maarifa" Hosea 4:6.

MAARIFA ni ya kuzingatia sana. Tunaangamia kwa kuwa tumechagua ufahamu wetu dhidi Yake. Shetani na ujinga wake wote amefanikiwa sana keenye kuwafanya watu wawe busy na anasa na mambo mengine ili wapwaye kwenye Neno. Pia muda wa kuwasiliana kwa sala nao uko limited sana.

MUNGU ATUSAIDIE kwa kweli tuzidi kumtegemea Yeye peke yake.
LIKE,LIKE LIKE. Mkuu Tized umemaliza,ni kweli kabisa wakristo wa leo tumekuwa wavivu sana kusoma neno na kuomba tunategemea watu wengne watufanyie matokeo yake tunapewa matango pori.

Neno la Mungu linatuagiza kwamba tumtafute Bwana maadam anapatikana tumuite yu karibu.,lakin ajabu wanadamu wa leo hatuishi kubun njia zetu kinyume na mapenzi yake.

Matokeo ya kutopenda kuomba sisi wenyewe ni kupewa unabii wa uongo,kupewa maji,mafuta,vitambaa,chumvi n.k mwisho wa siku ni kugeuka na kumkejel Mungu kwamba hatendi kumbe tatizo ni sisi wenyewe kutopenda ushirika na Mungu moja kwa moja.
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom