Utabiri: Simba kubeba taji la Kombe la Shirikisho barani Afrika 2021/22

Simba mwaka huu wangefika mbali sana kwenye Shirikisho lakini kitachakachowaangusha ni safu yao ya ushambuliaji. Hata kama watavuka hatua hii ya makundi bado kuendelea mbele zaidi itakuwa ngumu sana. Na hii hata kwenye NBC ligi imeshawagharimu na itaendelea kuwagharimu sana na pia itamrahisishia sana Yanga kubeba ndoo kilaini. Na huu ni ukweli mchungu ambao wanasimba wengi hawataki kuukubali mpaka sasa lakini ndio uhalisia wenyewe.

Kwa mtu aliyeitazama mechi ya juzi na Berekane kwa umakini ni lazima atakuwa ameona jinsi fowadi ya Simba inavyotaabika. Boko hata kukaa na mpira dakika moja wenzake wafike hawezi na akituliza mpira "control" chumba na sebule. Anapigiwa pasi beki wa Berekane anatoka nyuma yake anawahi mpira kabla yeye haujamfikia. Mugalu naye amekuwa na majeruhi ya mara kwa mara na hata akiwa mzima anakosa magoli ya wazi kabisa. Kagere ndiyo hivyo tena hatabiriki leo anacheza vizuri anafunga mechi ijayo anazurura tu uwanjani mpaka mpira unaisha.

Iwapo Simba ingekuwa na fowadi imara hata ile mechi ya Gendamarie wangeshinda ugenini na si kupata sare. Kwa hili Simba wapate funzo na waanze maandalizi mapema kwa kuanza kutafuta washambuliaji kwa ajili ya msimu ujao. Na wanatakiwa wafanye maamuzi magumu kweli kweli kuhusiana na safu yao ya ushambualiaji.
Mada yote inazungumzia simba na Caf confederation cup wewe unakuja kucomment unaitaja Yanga hivi simba anashindana na Yanga kweli kwenye hilo kombe au ni wewe uelewa wako wa mada umekuwa mdogo mkuu
Hebu tuchangie kulingana na mada iliyopo mezani sio mahaba yako niue kwa klabu yako
 
Hivi nyie viumbe akili zenu zikoje? Inaamana Manula anacheza Ndanda FC na siyo Simba SC? Kwanini mafaniko ya golikipa yabaguliwe ilhali yeye ndo muundo wa wachezaji 11.

Kwahivyo kama Sakho akifunga mabao matatu, utakuja kusema Simba SC siyo bora ila Sakho ndo bora..!

Unajua maana ya Team Work?
Mkuu na mimi nimemshangaa sana huyo jamaa na hoja yake eti Manula ndio bora ila simba sio bora as if kwamba Manula huwa tunamuazima Ndanda au Mbeya kwanza ili atudakie mechi zetu za shirikisho
 
Kuendelea kupata vichekesho vingine kama hivi andika ujumbe VICHEKESHO kwenda namba 7773
 
Nitajie hizo timu kwenye kombe hili la shirikisho ambazo zina forward imara kiasi kwamba hata ugenini wanabeba tu point 3 zote kama wapo kwao
Soma score board
Screenshot_2022-03-02-11-38-56-72.jpg
 
Kweli huu utabiri . Yaan kama TMA wangekuwa na utabiri kama huu tusingewaamini hata kido....
Yaan mkae mkijua kuwa Yanga anahitaji kushinda match 10 tu kati ya hz 14 zilizobaki na hyo itategemeana na Matokeo ya Mikia kama Kolos wakipoteza point kidogo tu basi fahamu match hazitakuwa 10 tena zitakuwa pungufu ya hzo. Sasa hyo nguvu ya kukaa na kutabiri kuwa Simba anaweza kuwa bingwa unajitolea wapi..?

Duuuuh mnasikitisha sana
Kumbe simba anashindana na yanga msimu huu kuwania Caf confederation cup? mimi sikuelewa hebu niweke sawa wao (Yanga) wapo kundi gani kwenye hii michuano?
 
Kumbe simba anashindana na yanga msimu huu kuwania Caf confederation cup? mimi sikuelewa hebu niweke sawa wao (Yanga) wapo kundi gani kwenye hii michuano?
Acha kujitoa ufahamu dogo.. ukija uku mjini utaolewa mapema sana
 
Angalia ushangiliaji wao kama wamebanwa na ngiri, hawawaoni wenzetu wa Yanga wanavyoshangilia na Mayele wao.
 
Simba imekuwa bora au Manula kawa bora? Mechi ya USGN simba walikuwa wanafungwa goli 2+ mechi dhidi ya Berkane walikuwa wafungwe 5+ ila Manula kafanya kazi ya ziada kusahisha makosa yaliyofanywa na wachezaji wake. Bado timu inafanya makosa mengi mno, spidi hakuna, mpira wa counter attack ni moja ya weakness ya Simba.

Unaposema timu bora umeitumia gizezo gani kuipima kwa performance au umepima kwa matokeoa?

Je kama umetumia muda wako kufatilia timu zote zinashiriki michuano hii mechi zao ili kuweza kujua uwezo wao?
Manula ni mchezaji wa Mgambo eee?
 
Hivi nyie viumbe akili zenu zikoje? Inaamana Manula anacheza Ndanda FC na siyo Simba SC? Kwanini mafaniko ya golikipa yabaguliwe ilhali yeye ndo muundo wa wachezaji 11.

Kwahivyo kama Sakho akifunga mabao matatu, utakuja kusema Simba SC siyo bora ila Sakho ndo bora..!

Unajua maana ya Team Work?
Upeo wao wa kufikiri ndipo unapoishia. Unategemea akupe nini cha ziada zaidi ya hizo pumba?
 
Kwenye timu zote 16 unaleta timu moja tu ndio ujue ni jinsi gani ilivyo ngumu kufanya hivyo na ndio maana unaona pamoja na dharau zako zote kwa simba ila ndio timu pekee kundi D kupata point ugenini sio Asec Mimosas wala Barkane
 
Back
Top Bottom