Utabiri: Ni suala la muda tu kabla hatujakazimika kuirudisha Bungeni Sheria ya maliasili za Gesi na Madini

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,014
144,371
Tangu sheria inayohusu maliasili za gesi na madini kufanyiwa marekebisho na serikali na kisha kupitishwa na Bunge,kumekuwa na madai mbalimbali yakiwemo malalamiko kutoka kwa wadau mbalimbali wa sekta hiyo yakiwemo makampuni ya utafutaji na uchimbaji wa madini na gesi.

Kuna madai pia kuwa baadhi ya makampuni yamesitisha shughuli zake ingawa pia ziko taarifa kuwa kuna makampuni mengine mapya yanaomba leseni za kufanya hizo zinazohusiana na uchimbaji na utafutai wa madini ama gesi.

Binafsi naona ni swala la muda tu kabla hatujalazimika kuirudisha tena Bungeni sheria husika ili ifanyiwe marekebisho kuondoa hii sintofahamu as long as madai/ taarifa hizi tunazosika na kuzisoma ni za kweli.

Sijui na siamini kama tumejianda na yatakayokuwa matokeo ya kubadili sheria hizi maana kila uamuzi una gharama zake.

Muda utaongea.
 
Binafsi sikubahatika kupata elimu lakini kutokana na kauli ya awali kutoka kwa maprofesa na mkulu mwenyewe kuwa Acacia walikuwa wametuibia zaidi ya trillion 400, nilitegemea kitendo cha bosi wao kutokea tena 'kujiingiza mtegoni' kwa kjipeleka magogoni angekamatwa pale pale na kupelekwa Segerea kunganishwa na akina Rugemalila na Kitilya. Ajabu akapokelewa kwa heshima!
Sasa watu hao hao wanaamua kuuza mali zao ili waondoke tuweze kupata 'waaminifu' na wasio wezi lakini serikali inawazuia wasiuze mitambo ambayo kimsingi imetumika 'kutuibia'!!!
Sasa kwa ile principle ya kufa na tai shingoni sijui ukifikia wasaa wa kuirudisha hiyo sheria itakuwaje ...au ndi inatakiwa 'upinzani ufe' kwanza alafu ndio irudishwe!
 
Mambo mengi aliyokua akiongea lisu kuanzia mwaka 2016 nilikua namuona kama mwehu! Lkn kwa sasa nimamin jamaa ni kiona mbali.
 
Back
Top Bottom