Utabiri: Ni suala la muda tu kabla CCM hawajamtosa Mwigulu

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,034
144,388
Napenda kumshauri na kumsihi naibu katibu mkuu wa CCM bara,mh.Mwigulu Nchemba,kuwa awe makini na aina ya siasa anazoziendesha.Anapaswa kutokujisahau,kutokulewa madaraka na kusoma alama za nyakati.

Jambo analopawsa kutambua kuwa CCM ni chama cha kisiasa na yeye kapewa nafasi hiyo wakiamini atakisaidia chama kukabiliana na siasa za ushindani.Anapaswa pia kutambua hali mbaya inayokikabili chama chake na kujiuliza endapo atafanya siasa za kukigharimu chama nani ataendelea kumvumilia?Nina uhakika si wote ndani ya CCM wanaridhika na siasa za sasa za Mwigulu Nchemba.

Kitu anachotakiwa kutambua kuwa CCM siku zote huangalia upepo wa kisiasa unakwendaje na kuweza kuchukua maamuzi yoyote ikiwa ni pamoja na kumtoa mtu kafara.Yeye mwenyewe teyari ameshaonyesha hali hii kwa kumgeuka waziri wa maliasili na utalii,mh kagasheki,baada ya kuona hali ya kisiasa kwa CCM ni mbaya huko Loliondo.Wamempinga Kagasheki wazi wazi kama vile sio mwenzao.Hata wale waliotakiwa kujivua gamba nao chama kiliamua kuwageuka tu ili kujisafisha mbele ya umma.kilichowaokoa kila mtu anakijua.

Huko Loliondo analaumiwa kufukuza waandishi wa habari,kesi ya Lwakatare anatajwa yeye,mikutano ya vurugu,mauji n.k jina lake lipo! Vurugu bungeni yeye na mambo mengine mengine.Yote haya ni hatari kwa chama chake.

Mwigulu Nchemba,pamoja na kusifiwa na mwenyekiti wako,bado hao hao wanaokusifu wanaweza wakakugeuka.Hawakawii kukwambia mwenzetu naona utupishe kwani mwenendo wako unaharibu jina la chama.Kama nilivyokwambia hapo awali,waliotakiwa kuvuliwa magamba ni mfano mzuri kwani baada ya kuonekana wao ndio wanaharibu "image" ya chama wakawataka wajiuuzulu nafasi zao ili kukinusuru chama.Unapaswa ujiulize, kama wale jamaa walitakiwa kujiuzulu,wewe je itashindikana nini?

Leo wanaweza wakakutuma,kesho wakakugeuka!
 
ha ha ha ha ha ha...

Sidhani kama kuna mwanasiasa Tanzania aliye na hati miliki ya kukaa kwenye madaraka forever.

Uongozi ni kupokezana vijiti. Timu iliyokuwepo ikimaliza ngwe yake inawapa kijiti wengine.

Hata Mwigulu kabla hajaingia hapo kulikuwa na mwingine.

Acha USHAMBA...
 
Tatizo vijana wa kibongo mnadhani kutoka madarakani ni adhabu.

Kutoka madarakani kwa watu fulani na kuingia wengine ndio afya ya nafasi husika. Nafasi ikikaliwa na mtu mmoja inadhoofika kiafya.

Just imagine binadamu tungekuwa na uwezo wa kurenew moyo na mishipa ya damu. Tungeweza kuishi MILELE.

Hivi ndivyo ilivyo kwa nafasi za uongozi. Kadri zinavyopata sura mpya ndio zinavyokuwa kama mwili uliwekewa moyo na mishipa ya damu mipya na zinavyozidi kuremain healthy.

Ndio maana mtu aliyedhihirisha kuishindwa kusimami ofisi kama Dr. Slaa anatakiwa ajiuzuru, hasahasa baada ya kushindwa kabisa kutunza siri za ofisi...
 
ha ha ha ha ha ha...

Sidhani kama kuna mwanasiasa Tanzania aliye na hati miliki ya kukaa kwenye madaraka forever.

Uongozi ni kupokezana vijiti. Timu iliyokuwepo ikimaliza ngwe yake inawapa kijiti wengine.

Hata Mwigulu kabla hajaingia hapo kulikuwa na mwingine.

Acha USHAMBA...

Siasa za ndani ya CCM tunazijua.Siku zote mnaanglia upepo unakwendaje.
 
Kama ungejua nguzo ya siasa endelevu ndani ya vyama vya siasa nafikiri usingepoteza muda wako kufikiria hatima ya Mh. Mwigulu Nchemba kisiasa.

Vyama vya siasa vilivyo makini havina adui wa kudumu na rafiki wa kudumu, vivyo hivyo hata kwa wanasiasa. FINITO.
 
Mkuu Salary Slip, I completely differ with you!! Mwigulu Nchemba really plays CCM's political mode,,,,pamoja na kwamba hana muda mrefu, the guy really sings and plays the real CCM Drama. By the way, humu JF hamna siku inayopita bila ya thread ya kumshambulia Mwigulu....threads hizi zina signals za u-CHADEMA! So, i really hate to say this, but i'll say it! Do you know the interpretation of these threads from POLITICAL POINT OF VIEWS? Maana yake ni kwamba CHADEMA mnanyimwa usingizi na Mwigulu coz' he really plays CCM's/African politics well. From civilized political world, Nchemba hafai na hayo usemayo yangetimia lakini from African Politics, your dream will never come true unless either he changes or CCM change or both!

Hapa JF mkiacha kumjadili Mwugulu, itakuwa ni ushindi kwa CHADEMA coz' ina-imply you have no time ya kumjadili mtu asiye na madhara but as long as kila siku mnamjadili, i can say this's BIG CREDIT FOR HIM! Hivi huoni hata CCM? Umeshawahi kusikia wakimjadili mtu kama Lucy Awenya(correct the name)? They don't coz' she's not threat to them but they'll always keep on kumjadili the one and only threat to them; DR. SLAA! So, wapeni CCM psychological punch kwa kuacha kumjadili Nchemba kila wakati.....baada ya hapo wataamini kwamba, Nchemba kwenu si lolote si chochote!
 
Last edited by a moderator:
Tatizo vijana wa kibongo mnadhani kutoka madarakani ni adhabu.

Kutoka madarakani kwa watu fulani na kuingia wengine ndio afya ya nafasi husika. Nafasi ikikaliwa na mtu mmoja inadhoofika kiafya.

Just imagine binadamu tungekuwa na uwezo wa kurenew moyo na mishipa ya damu. Tungeweza kuishi MILELE.

Hivi ndivyo ilivyo kwa nafasi za uongozi. Kadri zinavyopata sura mpya ndio zinavyokuwa kama mwili uliwekewa moyo na mishipa ya damu mipya na zinavyozidi kuremain healthy.

Ndio maana mtu aliyedhihirisha kuishindwa kusimami ofisi kama Dr. Slaa anatakiwa ajiuzuru, hasahasa baada ya kushindwa kabisa kutunza siri za ofisi...
Kutoka si tatizo, tatizo ni anatokaje?
 
ha ha ha ha ha ha...

Sidhani kama kuna mwanasiasa Tanzania aliye na hati miliki ya kukaa kwenye madaraka forever.

Uongozi ni kupokezana vijiti. Timu iliyokuwepo ikimaliza ngwe yake inawapa kijiti wengine.

Hata Mwigulu kabla hajaingia hapo kulikuwa na mwingine.

Acha USHAMBA...

hivi mkuu huwa hupumziki au ni wewe na key board all the time...duuh hii ni zaid ya utumwa!
 
ha ha ha ha ha ha...

Sidhani kama kuna mwanasiasa Tanzania aliye na hati miliki ya kukaa kwenye madaraka forever.

Uongozi ni kupokezana vijiti. Timu iliyokuwepo ikimaliza ngwe yake inawapa kijiti wengine.

Hata Mwigulu kabla hajaingia hapo kulikuwa na mwingine.

Acha USHAMBA...

Kwahiyo na mukama alimaliza muda wake akapeana kijiti, acha ushamba
 
Mkuu Salary Slip, I completely differ with you!! Mwigulu Nchemba really plays CCM's political mode,,,,pamoja na kwamba hana muda mrefu, the guy really sings and plays the real CCM Drama. By the way, humu JF hamna siku inayopita bila ya thread ya kumshambulia Mwigulu....threads hizi zina signals za u-CHADEMA! So, i really hate to say this, but i'll say it! Do you know the interpretation of these threads from POLITICAL POINT OF VIEWS? Maana yake ni kwamba CHADEMA mnanyimwa usingizi na Mwigulu coz' he really plays CCM's/African politics well. From civilized political world, Nchemba hafai na hayo usemayo yangetimia lakini from African Politics, your dream will never come true unless either he changes or CCM change or both!

Hapa JF mkiacha kumjadili Mwugulu, itakuwa ni ushindi kwa CHADEMA coz' ina-imply you have no time ya kumjadili mtu asiye na madhara but as long as kila siku mnamjadili, i can say this's BIG CREDIT FOR HIM! Hivi huoni hata CCM? Umeshawahi kusikia wakimjadili mtu kama Lucy Awenya(correct the name)? They don't coz' she's not threat to them but they'll always keep on kumjadili the one and only threat to them; DR. SLAA! So, wapeni CCM psychological punch kwa kuacha kumjadili Nchemba kila wakati.....baada ya hapo wataamini kwamba, Nchemba kwenu si lolote si chochote!
Yeah..!
Mwigulu kamfunikia Nape Kwa mbali mno, imagine sasa Nape mpaka watu wanauliza Yupo kweli.. Men..!! Ha ha haaa.. Yupo, anatema vitu lakini maskini ya Mungu Nyota yake ishafunikwa mbaya chezea mwigulu wewe .. !!

Jamaa kafeli Kwenye operation zote, IGUNGA NA ARUMERU, jamaa anamwaga mimatusi mingi Kwenye majukwaa ya kisiasa, jamaa anazusha mashimo ya hatari Kwa Chama but still wanambackup.. Kaaaaaz kwel kwel..
 
Last edited by a moderator:
Huyu mwingulu hata akili zake sio mzuri sana na hajui siasa its better 100 times angepewa lowassa

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
hivi mkuu huwa hupumziki au ni wewe na key board all the time...duuh hii ni zaid ya utumwa!

kweli mkuu hii ni zaidi ya utumwa jamaa nilishawahi kumuuliza analipwa sh ngapi? na maccm maana sisi tunabadilishana yeye kakomaa tu nafikiri hata ndoa hana
 
Kwangu huyu mshenzi si kitu na naungana na member mmoja humu kuwa tuacheni kumjadili kimsingi anapenda sana sifa hata awapo bungeni japo anailaisishia cdm kupita kiulaini,mwacheni mjinga abaki kuwa mjinga.stop talking nchemba.
 
Back
Top Bottom