Usomi wa Rais Magufuli na Kasumba ya Kiingereza

Ndugu yangu umejitahidi sana kupangilia mawazo yako lakini katika fact ya msingi ya matumizi ya lugha ya kiingereza nchini tanzania na kwingineko umechemka , kwani umeshindwa kwakua kiingereza ni rugha ya kujifunzia na kufundishia tofauti na nchi ulizo zihusisha hapo kwani wao hujifunza na kufundisha kutumia lugha zao .....by the way mtajwa hapo juu inawezekena amefikia level hiyo ya elimu kwa kuwa na cramming capacity kubwa....vinginevyo angekua vizuri katika lugha husika!!!!!!@$
 
Acheni limbukeni zenu....... leave our president alone plz....... ni icon ya Taifa

Icon ?? kina Nyerere,Mkapa ,Mwinyi ,Salim,Kikwete waitwije>>
asubiri tuone kwanza kazi yake ndio tutampa u LEGEND !!!! AKUBALI TU KUWA PHD YAKE FEKIIIIIII.
NAONA KAMATI YA MADINI KAMUWEKE NA "SUPERVISOR " WAKE WA PHD

BEN SAANANE!!!
 
Mkuu sasa ndio tuelewane hapa kuwa kwa mukatdha huu RAIS MAGUFULI NI LAZIMA AJIFUNZE KIINGEREZA...... i hope message imefika
Hoja niliyokuwa naipinga hasa kwamba Magufuli hajui kiingereza kiasi cha kutilia mashaka elimu yake.
 
Mgfl anajua kiingereza vizuri ila hana fluency. Hii ni kitu cha kawaida kabisa kwa watu wengi. Hata Waingereza wenyewe si wote wenye fluency.
Tatizo watu wanadhani watanzania hawaongei kiingereza vizuri et kwa sababu hatufundishwi vizuri kiingereza.
 
Lugha ni njia ya mawasiliano, ni chombo kinachotumika katika kuwasilisha ile hali ya kuelimika kwa jamii fulani. Wasomi wengi wa Tanzania wamepata elimu katika mataifa kama China, Russia, France, Germany na zile nchi za Scandinavia. Wengi wa wasomi hawa, mwaka wao wa kwanza ulitumika katika kujifunza lugha ya wenyeji, halafu miaka inayofuata ndipo huanza kusomea fani mbalimbali za kitaaluma.

Wale maprofesa ambao wanafunzi wa kitanzania wanalazimika kujifunza mwaka wa lugha ili waweze kufundishwa nao yale masomo ya fani, mara nyingi hawajui kabisa lugha ya kingereza.

Lakini kwa sababu kujua kingereza sio kuelimika, maprofesa hao wala hawaoni aibu kutokuijua lugha ya kingereza. Wameshaelimika kiasi cha kuigawa elimu yao kwa wanafunzi wa kigeni kutoka Tanzania, bila ya wao kulazimika kuwa watumwa wa lugha ya kingereza.

Kuna wale ambao wanamkejeli rais Magufuli, wakisema kwamba hapandi ndege kwenda Ulaya kwa sababu ya tatizo la lugha ya kingereza, wanasema kuwa anashindwa kuongea na wageni wa kimataifa kwa sababu hajui vizuri kingereza. Huyu anayekejeliwa ni msomi wa ngazi ya PHD, ambaye baadhi ya watu wanamkejeli kwa sababu ya kasumba ya kupenda vituu vya kigeni.

Maprofesa wa mataifa yasiyozungumza lugha ya kingereza, waliowafundisha wasomi wetu ambao ndio "vichwa" vya taifa hili, ni watu walioelimika bila hata ya kulazimika kuwa watumwa wa lugha ya kigeni kwao yaani kingereza.

Sisi tuliotawaliwa tunaona fahari kukifahamu kingereza!. Wakati hatuna maendeleo yoyote ambayo yanahusiana na kingereza, ambayo tunaweza kujivunia kwamba yametokana na sisi.

Tunamkejeli rais wetu tukisema kwamba hayuko vizuri kwenye kingereza, wakati hicho kiswahili chenyewe hatukijui!!. Hicho kiswahili ambacho ni lugha ya taifa kinaishia kutamkwa midomoni peke yake, hakuna maendeleo yoyote yale ya kiteknolojia ambayo yanahusishwa na lugha ya kiswahili kwa asilimia mia moja.

Miaka ya nyuma huko migodini wazungu ambao huko Uingereza na Australia walikuwa ni wafungwa, walipewa kazi na kulipwa mishahara mikubwa kwa sababu tu ya kuongea kwao lugha ya kingereza!.

Hawakuwa na utaalamu kuwazidi wataalamu wazalendo waliosomea VETA na vyuo vingine vya ufundi hapa hapa Tanzania. Ulimbukeni wetu ukawapa maisha bora wageni, kwa sababu akili zetu zilinasa kwenye mtego wa kubabaikia kingereza.

Watanzania tuachane na huu ushamba wa kuiona lugha ya kingereza kama vile ndio kila kitu maishani.
Sasa wewe endelea kubaki hivyo hivyo,unless huna plans za kuwa exposed na outside world,ila ukae ukijua vitu vingine havitaki ujuaji na ni bora tuu uwe submissive to the reality..ni aibu kubwa profesa wa kitanzania kama huyo unaemtetea kutojua lugha ya kiingereza,ni aibu kubwa mno,ukiangalia mfumo wetu wa elimu toka form one mpaka PhD lugha kuu ya ufundishaji ni kiingereza ambapo humlazimu mtu kuijua vizuri ili aweze kuleta ushindani hata kwenye outside world,usipoijua unategemea nini au ndo kusoma kwa kurariri na kutimiza madarasa huku kichwani mweupe,ni bora ukawalaumu watunga mitaala kuwa kwa nini hawakuifanya lugha ya kiswahili kuwa lugha kuu ya ufundishaji kama rwanda,japan,tunisia,egypt,south korea etc,ndo ujue utumwa wa lugha ulipoanzia!
 
Wabongo akili zao Very medieval,
Hivi hao waliojua kiingereza wameifikisha nchi wapi?

Kuna raisi alikuwa anazungumza kiingereza kama Mkapa?
Lakini hakuna mtu aliyeongoza kwa kuliweka taifa rehani kama Mkapa.

Hovyo kabisa,
To hell with their English.
Hivi kuna ubaya gani wa kujua Kingereza hasa.Mimi nadhani the more languages you know the better.Sasa kwa nini Watanzania wengi hata pamoja na ukweli huu wanasisitiza kwamba Kiingereza sio lazima?The reason is simple,hakipandi kabisa.
 
Hiyo PHD aliipata katika lugha ipi ya Swahili au English? Unatoa mifano kwa nchi ambazo kingereza sio official kama hapa kwetu..mwalimu gani asiyeweza kujieleza kwa kingereza lugha aliyoisoma kuanzia from one mpaka PhD? Kuna mtu aliwahi kuhoji uhalali wa PhD ya mkulu sijui aliishia wapo...Na hata utendaji wake haupo kisomi haiwezekani msomi wa PhD ushindwe kutekeleza mpango wa mwaka (budget) kwa 100%. Wahenga walisema lisemwalo lipo. Kuna mtu kamtaja Mkapa kaiweka nchi rehani lakini Unazingua Tsh20 ya mkapa ilikua na thamani wakati watoto wa Leo kuna baadhi hawajui Tsh.200.
 
Mtu anasema mwenyewe kuwa Magufuli hajui kabisa kiingereza halafu yeye tena anauliza PHD ameipataje?
 
Kwahiyo unamaanisha kama mheshimiwa alikuwa anasoma vitabu vya kemia vilivyoandikwa kwa kiingereza fasaha lakini anachuja kemia inaingia akilini na kuacha kiingereza fasaha kitabuni, hilo kwako si tatizo?
Hoja ya hapa ni kwamba kwa sababu Magufuli hawezi kuongea kiingereza vizuri hivyo hajui kabisa kiingereza, na kwa maana hiyo hata hivyo vitabu vya kemia hawezi kusoma maana kiingereza hajui.
 
Hoja ya hapa ni kwamba kwa sababu Magufuli hawezi kuongea kiingereza vizuri hivyo hajui kabisa kiingereza, na kwa maana hiyo hata hivyo vitabu vya kemia hawezi kusoma maana kiingereza hajui.
Shida yake ni ufasaha. Sarufi, msamiati, matumizi sahihi ya maneno,na utungaji wa sentensi kwa ujumla. Shida hii anayo katika kiswahili na kiingereza. Inawezekana hata kisukuma anachoongea siyo fasaha, lakini kwakuwa sijui kisukuma siwezi kuwa shuhuda wa hilo. Katika ufahamu wangu wa saikolojia ya elimu, hali ya mtu kutokumudu lugha ambayo amepata fursa ya kuizoea ni tatizo kabisa, tena linalohitaji ufumbuzi uliopangiliwa vizuri. Akili inayoshika kemia na kushindwa kushika lugha iliyobeba hiyo kemia ina kasoro. Sasa kama tuko tayari tujadili hiyo kasoro na utatuzi wake.
 
Shida yake ni ufasaha. Sarufi, msamiati, matumizi sahihi ya maneno,na utungaji wa sentensi kwa ujumla. Shida hii anayo katika kiswahili na kiingereza. Inawezekana hata kisukuma anachoongea siyo fasaha, lakini kwakuwa sijui kisukuma siwezi kuwa shuhuda wa hilo. Katika ufahamu wangu wa saikolojia ya elimu, hali ya mtu kutokumudu lugha ambayo amepata fursa ya kuizoea ni tatizo kabisa, tena linalohitaji ufumbuzi uliopangiliwa vizuri. Akili inayoshika kemia na kushindwa kushika lugha iliyobeba hiyo kemia ina kasoro. Sasa kama tuko tayari tujadili hiyo kasoro na utatuzi wake.
Mkuu sijakataa kuwa Magufuli kiingereza chake kina tatizo,lakini mkuu itakuwa ni sahihi kusema Magufuli hajui kabisa kiingereza kiasi cha kutilia mashaka elimu yake?
 
Hakuna mtanzania aliesoma hadi degree tu akaongea kiingereza dubwasha ka huyu mwenye PhD ya kemia. Alikariri boiling points tu akaenda watisha na uwaziri wake wakamtunukia PhD Kama zawadi tu.
 
Maelezo yako pamoja na hilo swali lako yote yana neno LABDA lakini mmekazania kuwa Magufuli hajui kiingereza!

Mna mashaka na elimu yake kwa sababu mnadai hajui kiingereza kilichotumika kufundishiwa toka form 1,lakini hapo hapo mnasema science hailazimishi sana kujua kiingereza kwa maana unaweza ukawa msio mzuri kwenye kiingereza ila masomo ya science yasikusumbue sana.

Huoni kuwa hoja zenu ni dhaifu?
mkuu mbona unanlisha maneno??? mie nlishikilia msimamo kuwa hajui english ndo maan tunadoubt elimu yake ssa wwe ndo ukaulixa kapataje phd ndo nkakupa a balanced story kuwa either ALIKARIRI au ndio kisa science haihitaji english!!!!

hyo ndo hoja yangu the rest nlijibu tu maswali yako kwa kukupa benefit of doubt
 
Hoja ya mashaka na elimu yake inakujaje ikiwa kumbe masomo yake hayahitaji sana kujua kiingereza?
Mkuu nmekupa tu benefit of doubt kuwa IF AND ONLY IF...... ila nachojua kafanya phd miaka 10 na inavyoonekana alikariri tu akapata phd ila sijui kma content anayo labda karatasi tu maana kma lugha ya kufundishia huijui ulichifundishwa utakijua????
 
Back
Top Bottom