Samahani
JF-Expert Member
- Oct 29, 2018
- 237
- 355
Maisha yanatupa nafasi ya kufanya maamuzi kila siku. Tunafanya maamuzi juu ya kila kitu kinachotuzunguka. Tunaamua muda wa kuamka na muda wa kulala, nini tufanye na nini tusifanye… Karibu kila wakati tunajikuta tunahitajika kufanya maamuzi. Kwa kiasi kikubwa, tuko jinsi tulivyo ni kutokana na maamuzi tunayoyafanya.
Umewahi kumiliki amali (asset) yoyote na ukalazimika kuiuza kutokana na sababu yoyote? Mfano, unaweza kuwa na kiwanja, nyumba, gari, redio, kitanda, kochi, simu, laptop, jokofu, vyombo vya ndani, nguo au kingine chochote kama hivyo. Wakati Fulani, unaweza kujikuta unalazimika kuuza mojawapo kati ya vitu hivi kwa sababu mbalimbali kama vile kukwama kiuchumi, kuhitaji fedha ya kukabiliana na dharura kubwa (msiba, ugonjwa, sherehe n.k), kuhitaji kubadilisha aina ya amali (kupata iliyo bora Zaidi), kuhamisha makazi, kupunguza idadi ya amali na sababu nyingine nyingi.
Hata hivyo, uzoefu unaonyesha kuwa, mara nyingi unapouza amali fulani, haiwi rahisi kununua tena amali hiyo!!! Hata pale unapofanikiwa kununua, huenda isiwe tena ya ubora na/au viwango vya amali iliyouzwa awali.
Mathalani, binafsi niliwahi kuuza shamba eneo ambalo sasa ni katikati ya mji kabisa. Wakati nauza eneo lile, nililiuza kwa shilingi milioni nne hivi. Lakini miaka sita baadae, eneo lile lile limekuwa na thamani ya Zaidi ya mara kumi!! Kwa kiasi kile kile ambacho niliuza, leo siwezi kupata hata eneo ambalo liko ndani ya kilometa kumi kutoka mjini lenye ukubwa ule ule!!!
Ni kutokana na sababu hii, nimejifunza juu ya yafuatayo kabla ya kuuza amali yoyote.
Umewahi kumiliki amali (asset) yoyote na ukalazimika kuiuza kutokana na sababu yoyote? Mfano, unaweza kuwa na kiwanja, nyumba, gari, redio, kitanda, kochi, simu, laptop, jokofu, vyombo vya ndani, nguo au kingine chochote kama hivyo. Wakati Fulani, unaweza kujikuta unalazimika kuuza mojawapo kati ya vitu hivi kwa sababu mbalimbali kama vile kukwama kiuchumi, kuhitaji fedha ya kukabiliana na dharura kubwa (msiba, ugonjwa, sherehe n.k), kuhitaji kubadilisha aina ya amali (kupata iliyo bora Zaidi), kuhamisha makazi, kupunguza idadi ya amali na sababu nyingine nyingi.
Hata hivyo, uzoefu unaonyesha kuwa, mara nyingi unapouza amali fulani, haiwi rahisi kununua tena amali hiyo!!! Hata pale unapofanikiwa kununua, huenda isiwe tena ya ubora na/au viwango vya amali iliyouzwa awali.
Mathalani, binafsi niliwahi kuuza shamba eneo ambalo sasa ni katikati ya mji kabisa. Wakati nauza eneo lile, nililiuza kwa shilingi milioni nne hivi. Lakini miaka sita baadae, eneo lile lile limekuwa na thamani ya Zaidi ya mara kumi!! Kwa kiasi kile kile ambacho niliuza, leo siwezi kupata hata eneo ambalo liko ndani ya kilometa kumi kutoka mjini lenye ukubwa ule ule!!!
Ni kutokana na sababu hii, nimejifunza juu ya yafuatayo kabla ya kuuza amali yoyote.
- Usiuze amali ikiwa hujaweka mipango madhubuti inayotekelezeka juu ya kununua amali mbadala ikiwa unaihitaji
- Usiuze amali kutokana na dharura ambayo unaweza kupata suluhisho mbadala kwa wakati huo. Hii inaweza kukulazimisha kuuza amali yenye thamani kubwa kwa bei ndogo mno.
- Epuka kutumia mtu wa tatu (kama vile dalali) wakati wa kuuza amali. Hii inaweza kupelekea kukosekana usawa wa bei ya amali unayoiuza.
- Unapolazimika kuuza amali, jitahidi kujua thamani halisi ya amali unayoiuza kwa wakati huo. Hii itakusaidia kuhakikisha kuwa, unauza amali husika kwa bei halisi au walau inayoakisi uhalisia wa wakati husika
- Mapato unayoyapata wakati umeuza chochote ulichowahi kukimiliki, hasa kama ni cha kudumu, ni vema ukahakikisha kuwa sehemu yake unaielekeza kwenye ununuzi wa amali nyingine.
- Penda kushirikisha watu wengine wakati wa kufanya maamuzi ya kuuza amali zako, hasa wale unaowaamini. Hii inaweza kukusaidia kupata msaada wa mawazo na wakati mwingine, unaweza kupata msaada wa kuweka rehani mali husika badala ya kuiuza.