Usisubiri aondoke ndiyo uanze kukosoa

Bob12

JF-Expert Member
Feb 27, 2017
11,422
58,787
Habari za asubuhi.

Kukosolewa ni njia moja wapo ambayo viongozi na watoa huduma wengi duniani huitumia kama njia moja wapo ya kujitathimini na kuboresha huduma zao.

Kuna mtu mwingine akikosolewa anakaa kimya,anatathimini na anafanyia kazi kimya kimya watu wanaona matunda kupitia matendo.

Kuna mtu mwingine akikosolewa anajitokeza hadharani na kuwashukuru wanao mkosoa na kuwa ahidi kufanyia kazi,hapo anaweza akafanyia au asifanyie kazi.

Kuna huyu ambae akikosolewa anakaa kimya mpaka mwisho wake bila kufanyia kazi hizo critics. Wa mwisho ni huyu ambaye akikosolewa anajitokeza hadharani na kujibu watu kibabe kwamba yeye ndiyo yeye,hakuna wa kumuendesha wala kumjaribu na anatoa onyo kali kwa atakae endelea kukosoa.

1a1b8dccce14a16201880eb301bf5071.jpg


Tafakakari
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom