Usipokuwepo, Hakuna Kilichopo!

Unaona sasa hapo? Tofauti ya mie na wewe ni kwamba mimi nazungumza vitu ambavyo naviexperience kutokana na uwepo wangu hapa duniani na kumbuka kuwa unaposema mtu kuwepo au kutowepo tunakusudia uwepo wa hapa duniani,sasa wewe unazungumzia vitu vya kufikirika tu.

Kwa kuwa tunazungumzia kuwepo hapa duniani na mie kuwepo kwangu duniani najua kabisa mtu ambaye bado hajazaliwa(hayupo) hana athari yeyote kwa huku duniani,na mtu akifa huiacha dunia uwepo wake unakuwa umeondoka hapa duniani.

Sasa ni ajabu kuacha mambo ambayo unayashuhudia na kutaka kutumia mambo ya kufikirika,halafu pia uthibitisho haufanyi jambo liwepo bali uthibitisho unatoa uhakika wa kuwepo hilo jambo ni suala la kujiridhisha.

Kwahiyo mie kabla ya kuja duniani dunia ilikuwepo(nimetumia uzowefu wangu wa uwepo wa hapa duniani) hata kama nilikuwa sijui na nasingeweza kuthibitisha hilo kuwa kuna dunia.

Mkuu, ninafurahi kuwa bado tupo pamoja. Maelezo yako yanasisitiza umuhimu wa wewe kuwepo. Hiki ndicho kiini cha mada, kwamba uwepo wako ndio unaosababisha kila kitu kiwepo. Unashuhudia mambo (ya duniani) kwa kuwa upo. Hakuna namna unaweza kushuhudia mambo (ya duniani) usipokuwepo. Je, tuisemee vipi hali ya wewe kushindwa kushuhudia mambo ya dunia milele katika hali yako ya kutokuwepo milele?
 
Vitu vipo hata bila ya wewe kuvithibitisha.
Hata akili yako ipo japo huwezi kuithibitisha

Inawezekana mkuu, kuthibitisha unaweza kuwa ni mchakato mwingine. Pengine tuseme kufahamu au kuwa kwenye nafasi ya kufahamu kuhusu uwepo wa kitu.
 
Vitu vipo hata bila ya wewe kuvithibitisha.
Hata akili yako ipo japo huwezi kuithibitisha

Hata ukiamua kufuata taratibu za kuthibitisha, jambo la kwanza ni lazima uwepo. Hata akili yako unayohitaji kuithibitisha haiwezi kuwepo bila wewe kuwepo.
 
Hata ukiamua kufuata taratibu za kuthibitisha, jambo la kwanza ni lazima uwepo. Hata akili yako unayohitaji kuithibitisha haiwezi kuwepo bila wewe kuwepo.
Tambua Uwepo wa Mungu hautegemei uchambuzi unaofanywa na akili zetu.
 
Siri ya uumbaji it's beyond human thinking. Majini, mapepo, mizimu, malaika na viumbe vingine visivyoonekana (visivyo na mwili bali nafsi) vinatuzidi kidogo kuhusu nini hasa siri ya uumbaji; vyote vinajua Mungu yupo na vinamuheshimu na kumwogopa; ila vingine vinafanya ujeuri tu sababu kiasi vinajua siri ya uumbaji.

Mambo yote haya yapo kwa kuwa wewe upo. Usipokuwepo, mambo haya kwako hayapo kabisa. Usingekuwepo, kusingekuwa na chochote, hata hawa malaika, mashetani, Mungu n.k.
 
Hilo ni suala la kutokujua na hivyo haina maana kuwa hicho usichokijua hakipo kisa wewe hukijui,mie nazungumza kwa kutumia uzowefu ila wewe mkuu unazungumzia ya kufikirika yenye kupingana na uhalisia uliyopo na unataka hayo ya kufikirika yawe na athari kwenye mambo yenye uhalisia.

Uhalisia ni wewe kuwepo au vitu kuwepo au wewe na vitu kuwepo mkuu? Mbona ninaona hali ya kutokuwepo ama kuwepo inakuwepo pale wewe unapokuwepo tu? Mimi nisipokuwepo, hali ya kutokuwepo kwangu itakuwepo kwa kuwa wewe upo ila, hali ya kutokuwepo kwangu ina sababisha kwangu mimi kusiwepo na chochote kabisa. Ni sawa na kusema mtu aomboleze msiba wake mwenyewe. Kumbuka mada ni usipokuwepo, hakuna kilichopo.
 
Oltunganyi, unaweza Ukanieleza chumba ni nini? Je, chumba ni kuta na paa? Au vitu vilivyomo ndani ya chumba?
Kiukweli jibu ni kwamba chumba ni empty space or nothing. Nothing can exist without nothing.

Sijui nimekuelewa vyema ndugu? Kwamba bila kuta na pengine paa, chumba kinaweza kuwepo au ni ile nafasi tupu? Kwamba, unaweza kufika mahali ukasema unaingia chumbanni kwenye empty space. Hakuna kinachoweza kuwepo bila kuwepo kwa kitu.
 
Sijui nimekuelewa vyema ndugu? Kwamba bila kuta na pengine paa, chumba kinaweza kuwepo au ni ile nafasi tupu? Kwamba, unaweza kufika mahali ukasema unaingia chumbanni kwenye empty space. Hakuna kinachoweza kuwepo bila kuwepo kwa kitu.
Jombaaaa vitu vipo hata bila ya wewe kuvithibitisha. Your dream house it's an imaginary but yet exist
 
Your ideas will keep on existing even after your death. All inventions lives on, even after the deaths of those who invented them

Baada ya kifo changu, hakuna kitakachokuwepo, hata mawazo yangu.
Hatuelewani! Ninasema kuwa, KUTOKUJUA KWAKO KWAMBA KITU KIPO, HAKUKIFANYI KUTOKUWEPO! UWEPO WAKO WEWE HAUFANYI KITU KISIWEPO KWA SABABU TU HUJUI KUWA KIPO!! AND THE FACT IS, WEWE UPO. USINGEKUWEPO, THAT COULD BE ANOTHER CASE. UNLESS KAMA WEWE MADAI YAKO KWA SASA NI KUWA HAUPO, WHICH IS WRONG KWA SABABU FACT INAONYESHA KWAMBA UPO!

Kuna siku ambayo sitakuwepo kama mabavyo sikuwepo, je unaweza kuelezea katika hali hii, ki kipi kitakuwepo kwa upande wangu?
 
Jombaaaa vitu vipo hata bila ya wewe kuvithibitisha. Your dream house it's an imaginary but yet exist
How can my imaginary house exist without my existence? Hoja ndio ipo hapa, kwamba vitu vipo kwa kuwa mimi nipo. Nisipokuwepo, hakuna kilichopo.
 
Mkuu, ninafurahi kuwa bado tupo pamoja. Maelezo yako yanasisitiza umuhimu wa wewe kuwepo. Hiki ndicho kiini cha mada, kwamba uwepo wako ndio unaosababisha kila kitu kiwepo. Unashuhudia mambo (ya duniani) kwa kuwa upo. Hakuna namna unaweza kushuhudia mambo (ya duniani) usipokuwepo. Je, tuisemee vipi hali ya wewe kushindwa kushuhudia mambo ya dunia milele katika hali yako ya kutokuwepo milele?

Hebu sasa eleza ni vp hii dunia tuliyopo ipo kwa sababu ya uwepo wetu?
 
Baada ya kifo changu, hakuna kitakachokuwepo, hata mawazo yangu.


Kuna siku ambayo sitakuwepo kama mabavyo sikuwepo, je unaweza kuelezea katika hali hii, ki kipi kitakuwepo kwa upande wangu?
Hata mifumo ya siasa ni ideas za watu.... Shati ulovaa hapo Mwanza lilikuwa wazo LA mtu. Na sasa hao watu hawaishi duniani tena lakini mawazo yao yapo yanaishi.
 
How can my imaginary house exist without my existence? Hoja ndio ipo hapa, kwamba vitu vipo kwa kuwa mimi nipo. Nisipokuwepo, hakuna kilichopo.
Jinga kabisa wew . Unafikiri hiyo suruali ulovaa iliumbwa kama wewe ulivoumbwa?
Hio suruali lilikuwa wazo LA mtu hapo kabla na huyo mtu hayupo tena lakini suruali zipo
 
Bado ninaona kuwa, kila kitu kinaanza na uwepo wangu. Siwezi kumtambua Mama au Baba bila kuwepo. Hakuna dunia, hakuna kila kitu, hadi Mungu hayupo, ikiwa mimi sipo. Kwa hiyo, kwangu mimi, na kwako pia, uwepo wa kila kitu ni wa muda muda tu. Muda ambao wewe au mimi nipo, nisipokuwepo, hakutakuwa na kitakachokuwepo.

Ninajua kuna kuzaliwa na kufa kwa kuwa nipo lakini haya hayajui ambaye hayupo (kafa au hajazaliwa). Lazima niwepo ili nijue kama wewe haupo au upo.
 
Hata mifumo ya siasa ni ideas za watu.... Shati ulovaa hapo Mwanza lilikuwa wazo LA mtu. Na sasa hao watu hawaishi duniani tena lakini mawazo yao yapo yanaishi.

Je, unaweza kuwa na uwezo angalau wa ufahamu wa hili pasipo kuwepo? Wewe unajua kuwa mawazo yao bado yanaishi, je, kwa upande wao, unaweza kusema kusema nin kwa kiasi gani wana ufahamu wa mawazo yao kuendelea kuishi? Uwepo wako ndugu ni kila kitu, usipokuwepo, kwako hakika hakuna kilichopo.
 
Uhalisia ni wewe kuwepo au vitu kuwepo au wewe na vitu kuwepo mkuu? Mbona ninaona hali ya kutokuwepo ama kuwepo inakuwepo pale wewe unapokuwepo tu? Mimi nisipokuwepo, hali ya kutokuwepo kwangu itakuwepo kwa kuwa wewe upo ila, hali ya kutokuwepo kwangu ina sababisha kwangu mimi kusiwepo na chochote kabisa. Ni sawa na kusema mtu aomboleze msiba wake mwenyewe. Kumbuka mada ni usipokuwepo, hakuna kilichopo.
Uhalisia ni haya yote nayokueleza mimi ndiyo uhalisia wenye mkuu,ni tofauti na wewe unayezungumzia jambo la kufikirika.
 
Baada ya kifo changu, hakuna kitakachokuwepo, hata mawazo yangu.


Kuna siku ambayo sitakuwepo kama mabavyo sikuwepo, je unaweza kuelezea katika hali hii, ki kipi kitakuwepo kwa upande wangu?
Huo uelewa wa baada ya kifo chako wewe umeutoa wapi? unawezaje kujua mambo ya baada ya kifo hali ya kuwa upo hai na hujawahi kufa?

Na ndiyo maana nakwambia wewe unapingana na uhalisia kwa mambo ya kufikirika .
 
Back
Top Bottom