Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 21,341
- 51,904
Kwa mkono wa Robert Heriel.
Wangestahili huruma lakini si sasa.
Wangestahili kupendwa lakini si Zama hizi.
Wangestahili kujaliwa na kuheshimiwa lakini hiyo ingefaa zama zile sio zama hizi.
Hata zamani walipokuwa wanasifa za wanawake hawakuonewa huruma sembuse sasa ambapo wamepoteza sifa ya uanamke Kwa 90%. Sasa hivi ndiyo hawapaswi kuonewa huruma hata kidogo.
Ni mama zetu, shangazi zetu, wake zetu, dada na bibi zetu lakini kamwe usimuonee mwanamke huruma hasa katika zama hizi. Ni kitanzi na kaburi lako mwenyewe.
Siwafundishi roho mbaya kwa maana sio asili yetu wanaume. Sisi ni watu wema tangu kale mpaka pale huruma mbaya ilipotuingia na hapo ndipo ubaya ukatuingia.
Jitahidi kuwa mbinafsi kwa kadiri utakavyoweza ili kujifurahisha wewe mwenyewe kuliko kuhangaika kumfurahisha mwanamke. Haitakusaidia popote pale zaidi ya kujiumiza na kuonekana kazi bure.
Usimuonee huruma mwanamke hata kama macho yako na akili yako vinaona anastahili kuonewa huruma.
Pengine mama yako tuu angalau huyo waweza mkumbuka kidogo lakini waliobaki cheza nao kwa akili nyingi huruma sifuri.
Huruma yako iwe na maslahi mapana. Apate kumi upate mia. Apate mia upate elfu. Usitumie moyo wako, tumia akili.
Usiwe na huruma kwa maana wanawake hupenda kuonewa huruma kwa wale watu wasiowapenda, huziweka nyuso zao za huruma ili kukulaghai na kuziteka hisia zako, usiwaangalie usoni wala usisikie sauti zao pindi wazungumzapo.
Walakini usimsahau mke wa ujana wako, ukamtendee wema ikiwa ulimchukua akiwa mwali, bikra safi. Huyo na mama yako walau unaweza wapa huruma yako kidogo hata kama wangekutenda makosa kadha wa kadha.
Lakini kama hawana sifa hizo kamwe huruma yako isiwe karibu na mwanamke.
Pia usitake huruma zozote kutoka kwa yeyote, tena akiwa mwanamke ndiyo usizitafute huruma zake.
Sina la ziada. Mwaka mpya mwema.
Robert Heriel,
Taikon wa fasihi,
Kwa sasa Makanya, Kilimanjaro.
Wangestahili huruma lakini si sasa.
Wangestahili kupendwa lakini si Zama hizi.
Wangestahili kujaliwa na kuheshimiwa lakini hiyo ingefaa zama zile sio zama hizi.
Hata zamani walipokuwa wanasifa za wanawake hawakuonewa huruma sembuse sasa ambapo wamepoteza sifa ya uanamke Kwa 90%. Sasa hivi ndiyo hawapaswi kuonewa huruma hata kidogo.
Ni mama zetu, shangazi zetu, wake zetu, dada na bibi zetu lakini kamwe usimuonee mwanamke huruma hasa katika zama hizi. Ni kitanzi na kaburi lako mwenyewe.
Siwafundishi roho mbaya kwa maana sio asili yetu wanaume. Sisi ni watu wema tangu kale mpaka pale huruma mbaya ilipotuingia na hapo ndipo ubaya ukatuingia.
Jitahidi kuwa mbinafsi kwa kadiri utakavyoweza ili kujifurahisha wewe mwenyewe kuliko kuhangaika kumfurahisha mwanamke. Haitakusaidia popote pale zaidi ya kujiumiza na kuonekana kazi bure.
Usimuonee huruma mwanamke hata kama macho yako na akili yako vinaona anastahili kuonewa huruma.
Pengine mama yako tuu angalau huyo waweza mkumbuka kidogo lakini waliobaki cheza nao kwa akili nyingi huruma sifuri.
Huruma yako iwe na maslahi mapana. Apate kumi upate mia. Apate mia upate elfu. Usitumie moyo wako, tumia akili.
Usiwe na huruma kwa maana wanawake hupenda kuonewa huruma kwa wale watu wasiowapenda, huziweka nyuso zao za huruma ili kukulaghai na kuziteka hisia zako, usiwaangalie usoni wala usisikie sauti zao pindi wazungumzapo.
Walakini usimsahau mke wa ujana wako, ukamtendee wema ikiwa ulimchukua akiwa mwali, bikra safi. Huyo na mama yako walau unaweza wapa huruma yako kidogo hata kama wangekutenda makosa kadha wa kadha.
Lakini kama hawana sifa hizo kamwe huruma yako isiwe karibu na mwanamke.
Pia usitake huruma zozote kutoka kwa yeyote, tena akiwa mwanamke ndiyo usizitafute huruma zake.
Sina la ziada. Mwaka mpya mwema.
Robert Heriel,
Taikon wa fasihi,
Kwa sasa Makanya, Kilimanjaro.