Usimdharau mtu, jifunze kupitia Historia ya maisha ya Kevin de Bruyne

Intelligent businessman

JF-Expert Member
Sep 6, 2022
26,110
52,836
Hadithi ya Kevin de Bruyne na mwanamke aliyemwacha

Picha ni marafiki wawili waliokua pamoja ndani timu ya kukuza vipaji nyumbani kwao Belgium mmoja wa kishua Thibaut mwingine wa maisha ya chini kabisa Kevin De Bruyne baadae wakanunuliwa na Chelsea ya vijana baadae mwanamke akawafanya kutengena na kuwa maadui mpaka Leo na hawajawahi kusemeshana licha ya kua wanaitwa timu ya taifa.

Mwadada unaemwona pichani hapo amevalia Uzi wa Real Madrid hapo awali alikua mpenzi wa Kevin De Bruyne na mwamba unaambiwa alimpenda sana na walipanga mambo mengi lakini kutokana na ujaujanja aliokua nao rafiki ake na Kdb Thibaut Coutouis alimzunguka rafiki ake kipenzi kwa kumshawishi shemeji Ake Kisha akamchukua kwakua yeye alikua kwenye nafasi nzuri na kumuoa kabisa huku akiacha machungu kwa msela wake ambaye alikua ameotea mtoto mkali kipindi icho

Wakati KDB anapambana na kipaji chake Chelsea na uongozi wake waliona Kevin De Bruyne hana kiwango Cha kucheza kwenye klabu yao

Mwamba alipa pigo baya sana kwenye maisha yake ambalo alishawai kusema kua ilimuumiza sana aliondokewa na mwanamke anaempenda na kwenda kwa rafiki ake ambaye yeye kipindi hicho alikua na maisha mazuri akiwa amesajiliwa na Atletco De Madrid anakula mshahara mzuri huku Kevin akiwa bado anasota na maisha baada ya Jose Mourinho kumkataa kua Hana kiwango Cha kuanza wa kucheza kwenye timu yake

Kutokana na mapito aliokua anapitia Kevin mwanamke huyo mrembo kabisa aliamini kua Moja Kwa Moja Thibaut ndiye mwaname sahihi kwenye maisha yake kuliko Kevin aliekua anahangaika na maisha kwa wakati huo kumbuka Kevin De Bruyne alikua na urafiki na Thibaut tangu wakiwa kwenye timu Yao ya nyumbani ya kurea vipaji Krc Genk walifanya mengi walisaidia mengi na mwisho mwamba akamuibia demu na maneno mengi ya kejeli .

Golikipa Coutouis alionekana kuanza kupata maisha mazuri mapema baada ya yeye kusajiliwa Atletco Madrid mwaka 2011 huku Kdb akiwa bado anahangaika pale darajani

Kutokana na pigo Hilo ambalo lilimyumbisha akili na kumfanya kukosa amani kabisa kutokana na upendo aliokua nao kwa bidada huyo na msaada aliokua akimpatia wakati Kevin Hana kitu changanya na maneno ya baadhi ya viongozi wa Chelsea waliosema kua Kevin Hana kipaji hivyo watamuuza hastahili kucheza Chelsea Kevin alipitia kipindi kigumu sana kwenye maisha yake kwani mwanamke aliekua anamsaidia mwazo pesa kidogo ameibiwa rafiki ake ambaye angemsaidia hata kidogo nae alimsaliti kisa mwanamke kiufupi Kevin alikua na wakati mgumu sana akiangaria na maisha ya nyumbani kwao ni magumu sana 💔✍🏿

KEVIN alipelekwa kwa mkopo na Chelsea Genk baadae wakamuuza kwenda Weeder Bremen ya Ujeruma kwa Euro laki nne na nusu huku wao wakiwa walimnunua kwa Euro million 08 kutoka Genk

Maisha ya mwamba yaliendelea kua magumu sana huko ujeruman kwani kocha wa kipindi hiko wa Werder Bremen alionekana kuukosoa usajili wa kiungo huyo na kusema kua hana kiwango hivyo hawezi kumpatia nafasi💔 mwamba alikua anajitahidi kujituma lakini kocha aligoma kabisa kukubali uwezo wa Kevin De Bruyne ✍🏿

Alikaa bench sana mpaka mkataba wake ukamalizika ameporwa mchumba home kwao maisha ni magumu sana Kwa kutokana na ugumu wa maisha ya wazazi wa kdb mama yake alimshawishi mwanawe aende kuishi kwa kaka ake ambaye ni mjomba wake ili aendeleze kipaji chake kwani mama ake aliamini mwanawe anakipaji Cha soka kikubwa anko wake alimtia moyo sana alimwambia mda utafika mambo yatabadilika .

Kevin De Bruyne Akiwa Werder Bremen na mkataba ukiwa umeisha uongozi uligoma kumuongeza mkataba wakimtaka atafute sehemu nyingine ya kwenda💔.

C.e.o wa Chelsea kipindi hicho mwanadada Marina aliamru Kya Kevin De Bruyne arejeshwe Chelsea na apewe nafasi acheze kweli bana mwamba akarejea darajani lakini mambo yalikua Yale Yale kubaguliwa changanya na uarubino alionao alikua akiishi maisha mabaya na ya uchungu sana pale Chelsea

Mnamo mwaka 2014 kocha alieitwa mwendawazimu na asiejua kuona vipaji wa klabu yenye mashabiki wengi watukutu Wolfsburg walitoa kitita Cha Euro Million 22 wakamsajili Kevin De Bruyne kutokea Chelsea na alipofika ujeruman kocha wa Wolfsburg alimwambia 🗣️ Kevin achana na kila kitu sahau kila kitu huu ni mda wako wa kuonyesha kipaji chako na uwezo wako dunia ikufahamu cheza soka

Kocha alianza kumtumia kama kiungo mchezeshaji na mwamba alianza kujituma na kocha alimpa nafasi mwanzo mwisho na Maisha ya Kevin yalianza kubadilika akiwa huko.

Kutokana na moto aliouwasha na machungu ya demu wake alienwambia kua yeye sio Romantic wara Hana dalili za kufanikiwa na akamkimbia na kwenda kwa rafiki ake mwamba alikua anacheza mpaka anabadilika rangi anakua mwekundu .

Mnamno mwaka 2015 basi hapo mda ukaamua na kusema ukweli kua nani Bora nani anapanga maisha ya watu Manchester City the Citizen walimsajili Kevin De Bruyne kwa kitita Cha Euro Million 76 kutoka kwa wahuni wa ujeruman Wolfsburg na hapo ndipo maisha ya Kdb yalipoanza kubadilika.

Mwamba alioa mwanamke mwingine mrembo ambaye hivu sasa amemzalia watoto wazuri na warembo mwamba amebadilisha maisha ya nyumbani kwao na mwamba arimjengea Jumba la kifahari mjomba wake huko Belgium.

Yule bidada aliemkimbia kwakuona kua mwamba hawezi kufanikiwa kutokana na mapito ya Dunia nafikiri moyoni hua anakili kua mwamba ningemvumilia kidogo mambo yangejipa kwani Kevin anacheza nafasi ya kiungo uwanjani huku bwana ake akicheza nafasi ya golikipa kwenye klabu ya Real Madrid Kdb analipwa mshahara mara 6 ya mshahara anaolipwa Coutouis na Kevin kwa sasa ndiye mfalme pale Manchester City na mashabiki wa Manchester City wanamuita The Manchester City wakimanisha kua yeye Kevin ndiye Manchester City kwani mafanikio mengi walioyapata City yamepitia kwenye mikono yake.

Kevin De Bruyne anapokea kiasi Cha Euro Laki nne kwa Kila mwezi kwenye klabu yake ya Manchester City na ndiye mchezaji mwenye assists nyingi kuliko mchezaji yoyote yule tangu City ianzishwe.

Kutokana na dharau walizowahi kumuonyesha Chelsea kama unafuatiria vizuri mechi za Manchester City na Chelsea kama Kevin yumo basi hua Hana huruma kabisa hupiga mashuti makali Sana na hujituma mara dufu zaidi.

Pia Wakati Real Madrid wanaiondoa Manchester City michuano ya UEFA Champions League mwaka 2021/22 Mwamba aliumia sana kitendo ambacho kilipelekea yeye kushindwa kupata usingizi siku hiyo bahati nzuri msimu uliopita Real Madrid wakapangwa mtoano na Manchester City Tena unaambiwa Kevin alikua akicheza kwa tahadhali kubwa mechi za ligi ili asiumie akutane na Real Madrid.

Mashabiki waliokua karibu na lango walisema Kevin alikua akipiga mashuti makali sana mara 3 ya Yale anayopiga Kila alipokua akikalibia lango la Real Madrid na wengi walitafsiri kua huenda anafanya hivyo kumuonyesha mwanamke wake aliemkimbia kua yeye hawezi kufanikiwa kama ulicheck game ya City na Madrid Ile Madrid anakufa goli nne utaelewa nachokwambia mwamba alikua anakamia sana .

Kevin De Bruyne hua haipendi Chelsea Toka moyoni kwani anaamini yeye alikua na uwezo wa kuichezea Chelsea ila wao walimkatisha tamaaa na kumtenga sana hivyo anaamini Chelsea walihusika zaidi kwenye maumivu yake aliopitia pia hajawahi kua na maelewano na Rafiki ake wa zamani hata wakiwa nation Team unaambiwa Kevin hua Hana story nae japo Coutouin hua anajitahidi lakini mwamba hua hataki shobo kabisa wara hua hataki Salamu yake.

Sasa wanangu wa Chelsea Nyie mlishawahi kua na mchezaji hatari kama alivyo Kevin De Bruyne au ndo Ile N'gombe ni N'gombe tu 😂

HII ICHUKUE KAMA FUNZO KUNA WATU MNATABIA YA KUONA WENZENU HAWAWEZI KUFANIKIWA KWENYE HIII DUNIA NAKUKUMBUSHA KAMA UNA TABIA YA HIVYO ACHANA NAYO MUNGU HATOKI KWENYE FAMILIA YENU NA KAMA UMEFANIKIWA NI WEWE ACHA DHARAU NA WANANGU PUNGUZENI TAMAA KAMA UNATAMAA ZA GOLIKIPA WA REAL MADRID KUTUMIA UDHAIFU WA MSELA
FB_IMG_17022424190816671.jpg
 
Stori nzuri sana, ila umenifanya nikumbuke umuhimu wa kujifunza namna ya kuwa mwandishi mzuri wa machapisho, si ajabu nimekua nikikosa kazi pale nnapoomba kutokana na uandishi wangu mbovu wa Barua.. content ninayo ila namna ya kutiririka pamoja na makosa ya kisarufi ndo kasheshe.
Anaeweza kunisaidia website ya Bure ya kujifunza uandishi (Content writing) Msaada Tafadhali..
Kongole kwako Intelligent Businessman.. stori nzuri sana!
 
Stori nzuri sana, ila umenifanya nikumbuke umuhimu wa kujifunza namna ya kuwa mwandishi mzuri wa machapisho, si ajabu nimekua nikikosa kazi pale nnapoomba kutokana na uandishi wangu mbovu wa Barua.. content ninayo ila namna ya kutiririka pamoja na makosa ya kisarufi ndo kasheshe.
Anaeweza kunisaidia website ya Bure ya kujifunza uandishi (Content writing) Msaada Tafadhali..
Kongole kwako Intelligent Businessman.. stori nzuri sana!
Nenda YouTube Kaka, Kuna video nyingi Zina fundisha Hilo.
 
Mwamba hatari kwa mikoma huyoo.Kuna muwa mmoja alimpelekea Emi Martinez (Dibu) mpaka keeper mwenyewe akabaki anacheka tu.
 
Mkuu, hii story ni nzuri sanaaaa ila utanisamehe uandishi wako sio mzuri, Hujaitendea haki inavyostahili.

Back to the story, Kevin namkubali sana. He is one of my favorite.
Hii story yake naijua vyema, na kuna wakati hadi alishindwa kumaliza mechi kati yao na Madrid... huwa namuonea huruma mke wake kwa kuwa ni wazi bado mumewe anampenda na kuumizwa sana na mpenzi wake wa zamani.

Kuachana na mtu uliyempenda sana, ni pigo lisilo na ukomo wa maumivu!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom