Nendubotho Sunguya
Senior Member
- Oct 9, 2019
- 126
- 109
Sikumbuki tarehe ila nakumbuka ilikuwa ni karibu kabisa na uchaguzi mkuu 2015, nikiwa nimelala chumba cha upande wa mbele wa nyumba yetu huko kijijini katika jimbo alilokuwa anawania Dkt Mollel kwa tiketi ya CHADEMA.Ghafla kama kimondo nilisikia jiwe kubwa limepiga kioo likatoa sauti kubwa sana ya mpasuko wa kioo.
Niliogopa na kufikiri ni ndoto lakini kabla sijang'amua kama ile ilikuwa ni ndoto au ni kweli, nilisikia watu wanatembea kwa vishindo na hali ya kuogofya huku wakiulizana maneno ambayo sikuyaelewa - ni kama fujo fulani. Watu wengine wakaamka ila kwa tahadhari sana.
Nikaenda sebuleni kuungana nao ndipo nilipowasikia wakitafuta sehemu ya kupanda ili washushe bendera ya CCM iliyoko juu ya bati letu. Ndipo wote tulijua hawa ni CHADEMA hofu ilitanda
Tuliogopa na kukimbilia jikoni huko ambako ni upande wa nyuma wa nyumba.
Hofu ilitujaa ukizingatia siku mbili zilizopita mwanachama mmoja kindaki ndaki wa CCM alilawitiwa na kutupwa maeneo ya makaburini na CHADEMA walijigamba baada ya tukio lile kwamba watakomesha na wengine.
Walifanikiwa kupanda juu wakashusha bendera kama baada ya dakika 10 pakawa kimya.
Ndipo baba akapigiwa simu na mlinzi wa maeneo ya maduka ambako na sisi tunaduka pale kwamba jamaa wamepanda juu ya bati la duka wanatoa bendera na pia wanachana picha za wagombea wa CCM zilizobandikwa kwenye kuta za duka letu.
Nikiri baba alikua mpenzi kindakindaki wa CCM na alitupa mifano mingi kwa nini tunapaswa kuienzi CCM.
Sikuwahi muelewa ila usiku ule nilimuelewa. Sikulala usiku kucha nikiwaza kama kweli hawa jamaa wakiingia ikulu itakuwaje?
Joto la uchaguzi lilipanda sana na kampeni za CHADEMA zilihusisha kuvamiavamia maeneo ya biashara za wanachama wa CCM na vitisho vingi matusi ya waziwazi niliyashuhudia.
CHADEMA walifanya uvunjifu mkubwa wa haki za kibinadamu na pia amani kipindi cha uchaguzi wa 2015 na kama kuna mwanahabari anayetaka kutengeneza habari nitampa evidence zote
Maana hata huyo jamaa aliyelawitiwa na CHADEMA aliwaona na anawajua sema alienda mafichoni na eneo alipo ninalifahamu.
CHADEMA wanaimba haki,utawala bora na usawa lakini vitendo walivyofanya wakati wa uchaguzi viliumiza watu wengi sana.
Naamini uchaguzi wa mwakani na huu wa Serikali za Mitaa mtaufanya kwa amani maana kwa staili ile hamkutakiwa kupata hata kitongoji kimoja.
Niliogopa na kufikiri ni ndoto lakini kabla sijang'amua kama ile ilikuwa ni ndoto au ni kweli, nilisikia watu wanatembea kwa vishindo na hali ya kuogofya huku wakiulizana maneno ambayo sikuyaelewa - ni kama fujo fulani. Watu wengine wakaamka ila kwa tahadhari sana.
Nikaenda sebuleni kuungana nao ndipo nilipowasikia wakitafuta sehemu ya kupanda ili washushe bendera ya CCM iliyoko juu ya bati letu. Ndipo wote tulijua hawa ni CHADEMA hofu ilitanda
Tuliogopa na kukimbilia jikoni huko ambako ni upande wa nyuma wa nyumba.
Hofu ilitujaa ukizingatia siku mbili zilizopita mwanachama mmoja kindaki ndaki wa CCM alilawitiwa na kutupwa maeneo ya makaburini na CHADEMA walijigamba baada ya tukio lile kwamba watakomesha na wengine.
Walifanikiwa kupanda juu wakashusha bendera kama baada ya dakika 10 pakawa kimya.
Ndipo baba akapigiwa simu na mlinzi wa maeneo ya maduka ambako na sisi tunaduka pale kwamba jamaa wamepanda juu ya bati la duka wanatoa bendera na pia wanachana picha za wagombea wa CCM zilizobandikwa kwenye kuta za duka letu.
Nikiri baba alikua mpenzi kindakindaki wa CCM na alitupa mifano mingi kwa nini tunapaswa kuienzi CCM.
Sikuwahi muelewa ila usiku ule nilimuelewa. Sikulala usiku kucha nikiwaza kama kweli hawa jamaa wakiingia ikulu itakuwaje?
Joto la uchaguzi lilipanda sana na kampeni za CHADEMA zilihusisha kuvamiavamia maeneo ya biashara za wanachama wa CCM na vitisho vingi matusi ya waziwazi niliyashuhudia.
CHADEMA walifanya uvunjifu mkubwa wa haki za kibinadamu na pia amani kipindi cha uchaguzi wa 2015 na kama kuna mwanahabari anayetaka kutengeneza habari nitampa evidence zote
Maana hata huyo jamaa aliyelawitiwa na CHADEMA aliwaona na anawajua sema alienda mafichoni na eneo alipo ninalifahamu.
CHADEMA wanaimba haki,utawala bora na usawa lakini vitendo walivyofanya wakati wa uchaguzi viliumiza watu wengi sana.
Naamini uchaguzi wa mwakani na huu wa Serikali za Mitaa mtaufanya kwa amani maana kwa staili ile hamkutakiwa kupata hata kitongoji kimoja.