Asante kwa bandiko zuri always nasema jamiiforum itabaki Kua ni kimbilio pekee nikipitia matatizo.
Nilkua nasikia watu wanasema sina hata shilingi mia! Nilikua najua ni masikhara. Duh kumbe hii hali hipo aisee? (Usicheke), Haya maisha bana ni basi tu..
hata ukisali saana hata uombe vipi sielewi haya maisha yakoje.
Haya maisha hayako fair hata kidogo. Unaweza kusali saaana hata usifanikiwe na mwingine ambaye hana time na Mungu akafanikiwa. Mfano mdogo, nimemaliza form six 2017 nikaenda Jkt kwa mujibu wenzangu walibakizwa (waliokua kambi zingine kambi yetu hawakuchukua) ndio hivyo sasahivi wengine wapo Russia, egpty n.k wengine wana nyota sasa. Japo nilifight kuipata hiyo nafasi nikaishia kufukuzwa tu pale lugalo(sitasahau), lakini kwenye biblia nafundishwa kumshukuru Mwenyezi Mungu kwa kila jambo. Pia tunafundishwa ya kwamba Mungu anampa kila mtu kwa wakati wake hila sioni future kabisa..
Wakuu Nipo nyumbani sasa baada ya vyuo kufungwa na aijulikani tunafungua lini(kutokana na hili janga la Corona) mwenye kazi yoyote hile anisaidie nitaifanya niingize hata buku mbili kwa Siku, popote tu hata walioko machimboni,ziwani wanipe direction tu mimi nije.
professional yangu Mimi ni Mwalimu wa physics na mathematics pia naweza fundisha masomo yote ya science (biology and chemistry).
so kwa mda huu watoto wako wakiwa nyumbani wasikae kizembe naweza fika popote pale nikawafundisha wakiwa nyumbani! (Napatikana mwanza). Nisaidieni wakuu maana nadaiwa kodi na mwenye nyumba (huko Chuo nimepanga).
Asanteni!!!