Usijenge kwa Matofali ya Udongo Utajuta Baadaye

Braza Kede

JF-Expert Member
Nov 1, 2012
1,669
3,314
Ukijaaliwa kupata uwezo jenga kwa kutumia tofali za simenti hizi mnaita blocks maana zinadumu dahari.

Mzee wangu alijenga miaka hiyo kwa kutumia hizi tofali za blocks saivi kashastaafu anapeta tu. Ila wenzie waliojenga kwa tofali za madongo saivi nyumba zimeshachoka hoi nyingine zimeshaegama tenge baada ya tofali kuliwa na maji na unyevunyevu wa miaka mingi.

Wajamen kijana wa leo ni mzee wa kesho tujenge kwa simenti japo kwa sasa inaweza kuonekana ni gharama kubwa. lakini unajikinga na gharama kubwa zaidi ya kutakiwa kufanya ukarabati wa jengo au kujenga tena hapo mbeleni.
 
Ukijaaliwa kupata uwezo jenga kwa kutumia tofali za simenti hizi mnaita blocks maana zinadumu dahari.

Mzee wangu alijenga miaka hiyo kwa kutumia hizi tofali za blocks saivi kashastaafu anapeta tu. Ila wenzie waliojenga kwa tofali za madongo saivi nyumba zimeshachoka hoi nyingine zimeshaegama tenge baada ya tofali kuliwa na maji na unyevunyevu wa miaka mingi.

Wajamen kijana wa leo ni mzee wa kesho tujenge kwa simenti japo kwa sasa inaweza kuonekana ni gharama kubwa. lakini unajikinga na gharama kubwa zaidi ya kutakiwa kufanya ukarabati wa jengo au kujenga tena hapo mbeleni.
Sawa nimekuelewa sana .

Sent from my SM-J410F using JamiiForums mobile app
 
Labda ambazo hazijachomwa!
La udongo lilichomwa likaiva ni mkataba miaka mia.
unachosema ni sahihi LAKINI ni hadi huo udongo uwe umechomwa vizuri kwelikweli na hapo ndo mtihani ulipo.

kuna mambo mengi yanaingia hapo kwenye iyo kazi ya uchomaji. kwa mfano aina ya udongo unaoutumia maana sio kila udongo unazalisha tofali zuri la kuchoma. utaalamu wa hao wachomaji.

kifupi unatakiwa uanze kiusahihi kuanzia hatua ya mwanzo ya uaandaji wa izo tofali hasa kuchagua sehem sahihi ya kupigia izo tofali.
 
Labda ambazo hazijachomwa!
La udongo lilichomwa likaiva ni mkataba miaka mia.
Naafikiana nawe, nadhani mleta mada ni muuzaji wa hayo matofari, ila ukweli ni kwamba tofari za kuchomwa hazichakachuliwi kama zile za cement ambazo wanaminya sana ratio, ukitazama majengo ya wamishenari mengi yalijengwa kwa matofari ya kuchomwa na hadi leo yako kama mapya
 
Ukijaaliwa kupata uwezo jenga kwa kutumia tofali za simenti hizi mnaita blocks maana zinadumu dahari.

Mzee wangu alijenga miaka hiyo kwa kutumia hizi tofali za blocks saivi kashastaafu anapeta tu. Ila wenzie waliojenga kwa tofali za madongo saivi nyumba zimeshachoka hoi nyingine zimeshaegama tenge baada ya tofali kuliwa na maji na unyevunyevu wa miaka mingi.

Wajamen kijana wa leo ni mzee wa kesho tujenge kwa simenti japo kwa sasa inaweza kuonekana ni gharama kubwa. lakini unajikinga na gharama kubwa zaidi ya kutakiwa kufanya ukarabati wa jengo au kujenga tena hapo mbeleni.
Kama ni ya kuchoma ni mkataba. Nyumba moja huko kijijini kwetu aliishi babu yangu zaidi ya miaka 40 iliyopita imesimama hadi. Sio hiyo almost huko ninakotoka asilimia 98 ya nyumba zimejengwa kwa tofali za kuchoma na zina miaka zaidi ya 50
 
kuna mambo mengi yanaingia hapo kwenye iyo kazi ya uchomaji. kwa mfano aina ya udongo unaoutumia maana sio kila udongo unazalisha tofali zuri la kuchoma. utaalamu wa hao wachomaji.
Siku zote wachomaji wa hizo tofari wanazingatia sana ubora kwasababu tofari hujisema zenyewe katika kila hatua ya utengenezaji, kwenye cement hapana kuna wizi mwingi sana, mtu anaweka ratio ya 1:40 si unajitengenezea kifo likipita tetemeko? isitoshe ukitumia tofari za cement unalazimika kujenga kwa cement na mchanga wakati ukitumia tofari za kuchoma unajenga hata kwa tope na nyumba inakuwa imara hata ikiungua bado hulazimiki kubomoa kuta
 
Kama ni ya kuchoma ni mkataba. Nyumba moja huko kijijini kwetu aliishi babu yangu zaidi ya miaka 40 iliyopita imesimama hadi. Sio hiyo almost huko ninakotoka asilimia 98 ya nyumba zimejengwa kwa tofali za kuchoma na zina miaka zaidi ya 50
Mkuu zipo hata zisizochommwa zinakaa miaka na miaka
 
Naafikiana nawe, nadhani mleta mada ni muuzaji wa hayo matofari, ila ukweli ni kwamba tofari za kuchomwa hazichakachuliwi kama zile za cement ambazo wanaminya sana ratio, ukitazama majengo ya wamishenari mengi yalijengwa kwa matofari ya kuchomwa na hadi leo yako kama mapya
Mm sio mfyatuaji ila nimeongea kitu nilichokiona live mtaani kwangu.

hapa tunazungumzia hizi nyumba tunazojenga wenyewe huku kitaa kwa kutumia kina fundi maiko. Hizo za misheni ni exception mkuu. misheni wana wataalam wao waliosomea kabisa hizo mambo.
 
unachosema ni sahihi LAKINI ni hadi huo udongo uwe umechomwa vizuri kwelikweli na hapo ndo mtihani ulipo.

kuna mambo mengi yanaingia hapo kwenye iyo kazi ya uchomaji. kwa mfano aina ya udongo unaoutumia maana sio kila udongo unazalisha tofali zuri la kuchoma. utaalamu wa hao wachomaji.

kifupi unatakiwa uanze kiusahihi kuanzia hatua ya mwanzo ya uaandaji wa izo tofali hasa kuchagua sehem sahihi ya kupigia izo tofali.
Kifupi tu jua tofali ya kuchoma ni durable mara 10 ya tofali ya saruji(cement)
 
We jamaa tofali za kuchoma ni imara kuliko hizo za block, sema jamaa zako walijengea tofali ambazo hazikuchomwa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom