Einstein
Senior Member
- Dec 5, 2009
- 121
- 26
Ilikuwa ijumaa majira ya saa mbili jioni, nilipokea simu ya rafiki yangu wa karibu akanambia yuko Mlimani City akanambia anahitaji kuonana na mimi maana kesho yake alikua ana "interview" kwa hiyo alitaka kupata uzoefu wangu wa "interview". Nilikuwa nimechoka, ila sikusita, nikamkubalia aje ili niweze ongea nae mawili matatu.
Huyu jamaa alikuwa rafiki yangu wa karibu sana nimesoma nae shule ya msingi, 1996 mpaka 2001. Alikuwa ni kati ya marafiki tuliosaidiana sana katika masomo yetu ya shule ya msingi.
Basi, kwa sababu ya kuamini kuwa ni mtu makini, nilimkaribisha nyumbani, nikamwandalia msosi, tukala na baadae tukapata muda wa kuzungumza mawili matatu.
Ukafika muda wa kulala, tukaenda tukajipumzisha, ingawa ye alibaki kidogo sebuleni kuangalia TV na baada ya kama dakika 40 hivi nae akaja kulala.
Tumelala mpaka ilipofika mishale ya asubuhi, mie nikaamka kwenye saa moja hivi, nikawa napiga stori na mdogo wangu niliekuwa nae pembeni yangu. Ye huyo rafiki yangu alikuwa bado amelala, ingawa alikuwa anajigeuza geuza, nikidhani bado yuko kwenye usingizi.
Baada ya kuwa amejigueza geuza hivyo, kidogo tu akainuka, akaenda washroom kidogo, baadae akaaga hapo hapo.
Nikamwuliza mbona unaaga mapema sana, kwanini usisubiri tunywe chai ndo uende. Akasema hapana anawahi Mbezi kwenye interview kwa hiyo kama vipi atarudi baadae ili aje kunywa chai wakati akiwa njiani kurudi kwake Magomeni(alidai anaishi huko). Akanambia nimsaidie nauli kidogo. Nikarudi chumbani nikachukue vijisenti kidogo nikampatia. Tukaagana.
Mishale ya saa tatu kasoro hivi nikawa nahitaji kuingia kwenye internet kupitia simu yangu. Mara nyingi simu huiacha kwenye chaji, chini ya kitanda, kwenye kapeti.
Nilipoangalia pale sikuiona simu, nikiipiga haipatikani wakati nimeiacha kwenye chaji na ilikuwa ON. Simu yangu ilikuwa aina ya SAMSUNG GALAXY NOTE II, ambayo gharama yake ni kati ya laki sita na saba.
Basi nikatatufa weee nikawa siioni. Lakini nkajiuliza inakuaje kitu kipotee, tena ndani, na wakati nimekiacha kwenye chaji wakati nalala, halafu simu yenyewe ni kubwa, kwa hiyo ni rahisi kuiona, halafu mbaya zaidi haipatikani. Basi nikajua hii simu imeibiwa. Na mtu wa kwanza kumhisi ni huyo rafiki angu tulielala nae.
Nikaona nikimpigia moja kwa moja inawezekana namwonea. Nilichofanya, ikabidi nianze kuulizia tabia yake. Dah! Kumbe rafiki yangu alishabadilika siku nyingi amekuwa tapeli mkubwa. Katapeli watu kibao. Kila mtu akawa ananishangaa kwanini nakaribisha nyumbani mtu kama huyo. Nikasikitika sana, nikajua moja kwa moja ni yeye ndie aliechukua simu.
Nikampigia simu nikimwambia arudishe simu yangu. Akakataa kwamba hajachukua simu, na akasema, yaani yeye kufika kwangu siku hiyo inakuwa tabu mpaka naanza kumsingizia kaiba. Nikamwambia basi njoo nyumbani angalau tusaidiane kuitafuta maana tumelala wote. Akanikatia simu, nikawa nampigia hapokei, wala SMS hajibu. Nikasikitika sana.
Nikawa najiuliza nitaipataje hii simu yangu nzuri niliyokua naipenda, na bora simu unaweza nunua tena, ila kulikuwa na documents (nyaraka) muhimu niliziweka kwenye simu ile, na zilikuwa na assignment na projects zangu. Nitaipataje.
Basi, siku nzima ya jumamosi na jumapili nilijitahidi kuwasiliana nae bila mafanikio. Ingawa siku ya jumamosi usiku aliniahidi atakuja nyumbani baada ya kushauriwa na moja ya rafiki yangu wa shule ya msingi, lakini sikumwona kufika.
Jumatatu majira ya saa tano akanipigia simu, nilikuwa ndani ya training ya kiofisi, akanambia kuwa, simu yangu kaiweka bond (sidhani kama ilikuwa kweli) ya TSh elfu arobaini, kwa hiyo akataka nimrushie elfu arobaini ili aikomboe simu yangu ndo aniletee, na akanitishia kuwa, nikichelewa hiyo simu sitaiona tena.
Nikajiuliza, simu ni yangu, kaiiba, halafu kaiweka bond (naamini bond ni uongo), halafu nimrushie pesa akakomboe simu yangu? Duh! Kweli ujinga mzigo.
Ila kwa sababu niliihitaji sana hiyo simu, nikamwuliza, "Uko wapi??" akanambia, "Niko Africana.." .. Nikamwambia, hapo Africana, kuna tawi la ofisi yetu, kwa hiyo nenda pale ofisini, nitawaelekeza wafanyakazi wa hapo wakupe elfu arobaini na uwaachie simu yangu.
Akanambia, "Aiseee!! Mie naona unazingua, huyu jamaa(jamaa wa bond) nikimwacha hapa sitamwona tena, kwa hiyo inabidi urushe tigopesa fasta ili niikomboe simu (uongo)"..
Basi nikamwambia,
"Nielekeze mlipo ili nimtume mtu aje hapo akupe hela na achukue simu"..
Akanambia, "Huyu jamaa hataki mtu yeyote aje hapa..."
Nikamwambia, "Basi nipe namba ake nimpigie ili asiondoke na simu yangu"
Akanambia, "Hapana we tuma tu hela, halafu naona unazingua simu unaweza usiione tena.."
Nikamwambia, "Basi mie nakuja huko Africana ili kulishughulikia hilo swala"
Nikatoroka training nikaenda mpaka Africana, nilipofika, nikampigia simu ili aje anipe simu yangu. Kumpigia akanambia, "Tuma kwenye tigopesa yangu"..
Nikamwambia,"Sasa kama ntakutumia kwenye tigopesa hiyo simu naipataje (kupitia tigopesa)? "..
Akanambia, "J ... mie naona unazingua, mie nakwambia tuma kwenye tigopesa we unachelewa, hii simu utakua hauipati tena"..
Nikamwambia, "Hivi nimekukosea nini mpaka unanifanyia unyama wa aina hii, simu yangu halafu initese kiasi hiki??"..
Basi akanikatia simu.
Nikaenda mahali, nikakaa, nikawa nampigia hapatikani.. Ilinichukua kama masaa mawili hivi nikiwa nimekaa kwenye ki restaurant flani maeneo ya africana, nikijifariji na lunch kidogo, huku nikisubiri nikiamini huenda tukaonana nikachukua simu yangu.
Baadae nikajaribu kumpigia akawa anapatikana nikamwambia, nimekusubiri sana bila mafanikio. Nikaamua kurudi zangu home, na mpaka dakika hii sijaipata simu yangu.
CHA KUJIFUNZA.
Usiamini mtu yeyote, hata kama ni rafiki yako. Hakikisha unamjua vizuri kabla ya kumkaribisha nyumbani kwako. Ameniudhi sana, maana ni mtu ambae nimekua nae, tumezaliwa wote sehemu moja, tumekua wote, tumesoma wote, tulikua tukisaidiana enzi hizo halafu anakuja kuwa mtu wa kuniibia, kunipotezea documents zangu za mhimu ambazo ni za mhimu sana kwenye kazi zangu.
Kiukweli nimemchukia sana na itanichukua muda kumsamehe na kumsahau. Ipo siku tutakutana tu, na sheria lazima ichukue mkondo wake.
Huyu jamaa alikuwa rafiki yangu wa karibu sana nimesoma nae shule ya msingi, 1996 mpaka 2001. Alikuwa ni kati ya marafiki tuliosaidiana sana katika masomo yetu ya shule ya msingi.
Basi, kwa sababu ya kuamini kuwa ni mtu makini, nilimkaribisha nyumbani, nikamwandalia msosi, tukala na baadae tukapata muda wa kuzungumza mawili matatu.
Ukafika muda wa kulala, tukaenda tukajipumzisha, ingawa ye alibaki kidogo sebuleni kuangalia TV na baada ya kama dakika 40 hivi nae akaja kulala.
Tumelala mpaka ilipofika mishale ya asubuhi, mie nikaamka kwenye saa moja hivi, nikawa napiga stori na mdogo wangu niliekuwa nae pembeni yangu. Ye huyo rafiki yangu alikuwa bado amelala, ingawa alikuwa anajigeuza geuza, nikidhani bado yuko kwenye usingizi.
Baada ya kuwa amejigueza geuza hivyo, kidogo tu akainuka, akaenda washroom kidogo, baadae akaaga hapo hapo.
Nikamwuliza mbona unaaga mapema sana, kwanini usisubiri tunywe chai ndo uende. Akasema hapana anawahi Mbezi kwenye interview kwa hiyo kama vipi atarudi baadae ili aje kunywa chai wakati akiwa njiani kurudi kwake Magomeni(alidai anaishi huko). Akanambia nimsaidie nauli kidogo. Nikarudi chumbani nikachukue vijisenti kidogo nikampatia. Tukaagana.
Mishale ya saa tatu kasoro hivi nikawa nahitaji kuingia kwenye internet kupitia simu yangu. Mara nyingi simu huiacha kwenye chaji, chini ya kitanda, kwenye kapeti.
Nilipoangalia pale sikuiona simu, nikiipiga haipatikani wakati nimeiacha kwenye chaji na ilikuwa ON. Simu yangu ilikuwa aina ya SAMSUNG GALAXY NOTE II, ambayo gharama yake ni kati ya laki sita na saba.
Basi nikatatufa weee nikawa siioni. Lakini nkajiuliza inakuaje kitu kipotee, tena ndani, na wakati nimekiacha kwenye chaji wakati nalala, halafu simu yenyewe ni kubwa, kwa hiyo ni rahisi kuiona, halafu mbaya zaidi haipatikani. Basi nikajua hii simu imeibiwa. Na mtu wa kwanza kumhisi ni huyo rafiki angu tulielala nae.
Nikaona nikimpigia moja kwa moja inawezekana namwonea. Nilichofanya, ikabidi nianze kuulizia tabia yake. Dah! Kumbe rafiki yangu alishabadilika siku nyingi amekuwa tapeli mkubwa. Katapeli watu kibao. Kila mtu akawa ananishangaa kwanini nakaribisha nyumbani mtu kama huyo. Nikasikitika sana, nikajua moja kwa moja ni yeye ndie aliechukua simu.
Nikampigia simu nikimwambia arudishe simu yangu. Akakataa kwamba hajachukua simu, na akasema, yaani yeye kufika kwangu siku hiyo inakuwa tabu mpaka naanza kumsingizia kaiba. Nikamwambia basi njoo nyumbani angalau tusaidiane kuitafuta maana tumelala wote. Akanikatia simu, nikawa nampigia hapokei, wala SMS hajibu. Nikasikitika sana.
Nikawa najiuliza nitaipataje hii simu yangu nzuri niliyokua naipenda, na bora simu unaweza nunua tena, ila kulikuwa na documents (nyaraka) muhimu niliziweka kwenye simu ile, na zilikuwa na assignment na projects zangu. Nitaipataje.
Basi, siku nzima ya jumamosi na jumapili nilijitahidi kuwasiliana nae bila mafanikio. Ingawa siku ya jumamosi usiku aliniahidi atakuja nyumbani baada ya kushauriwa na moja ya rafiki yangu wa shule ya msingi, lakini sikumwona kufika.
Jumatatu majira ya saa tano akanipigia simu, nilikuwa ndani ya training ya kiofisi, akanambia kuwa, simu yangu kaiweka bond (sidhani kama ilikuwa kweli) ya TSh elfu arobaini, kwa hiyo akataka nimrushie elfu arobaini ili aikomboe simu yangu ndo aniletee, na akanitishia kuwa, nikichelewa hiyo simu sitaiona tena.
Nikajiuliza, simu ni yangu, kaiiba, halafu kaiweka bond (naamini bond ni uongo), halafu nimrushie pesa akakomboe simu yangu? Duh! Kweli ujinga mzigo.
Ila kwa sababu niliihitaji sana hiyo simu, nikamwuliza, "Uko wapi??" akanambia, "Niko Africana.." .. Nikamwambia, hapo Africana, kuna tawi la ofisi yetu, kwa hiyo nenda pale ofisini, nitawaelekeza wafanyakazi wa hapo wakupe elfu arobaini na uwaachie simu yangu.
Akanambia, "Aiseee!! Mie naona unazingua, huyu jamaa(jamaa wa bond) nikimwacha hapa sitamwona tena, kwa hiyo inabidi urushe tigopesa fasta ili niikomboe simu (uongo)"..
Basi nikamwambia,
"Nielekeze mlipo ili nimtume mtu aje hapo akupe hela na achukue simu"..
Akanambia, "Huyu jamaa hataki mtu yeyote aje hapa..."
Nikamwambia, "Basi nipe namba ake nimpigie ili asiondoke na simu yangu"
Akanambia, "Hapana we tuma tu hela, halafu naona unazingua simu unaweza usiione tena.."
Nikamwambia, "Basi mie nakuja huko Africana ili kulishughulikia hilo swala"
Nikatoroka training nikaenda mpaka Africana, nilipofika, nikampigia simu ili aje anipe simu yangu. Kumpigia akanambia, "Tuma kwenye tigopesa yangu"..
Nikamwambia,"Sasa kama ntakutumia kwenye tigopesa hiyo simu naipataje (kupitia tigopesa)? "..
Akanambia, "J ... mie naona unazingua, mie nakwambia tuma kwenye tigopesa we unachelewa, hii simu utakua hauipati tena"..
Nikamwambia, "Hivi nimekukosea nini mpaka unanifanyia unyama wa aina hii, simu yangu halafu initese kiasi hiki??"..
Basi akanikatia simu.
Nikaenda mahali, nikakaa, nikawa nampigia hapatikani.. Ilinichukua kama masaa mawili hivi nikiwa nimekaa kwenye ki restaurant flani maeneo ya africana, nikijifariji na lunch kidogo, huku nikisubiri nikiamini huenda tukaonana nikachukua simu yangu.
Baadae nikajaribu kumpigia akawa anapatikana nikamwambia, nimekusubiri sana bila mafanikio. Nikaamua kurudi zangu home, na mpaka dakika hii sijaipata simu yangu.
CHA KUJIFUNZA.
Usiamini mtu yeyote, hata kama ni rafiki yako. Hakikisha unamjua vizuri kabla ya kumkaribisha nyumbani kwako. Ameniudhi sana, maana ni mtu ambae nimekua nae, tumezaliwa wote sehemu moja, tumekua wote, tumesoma wote, tulikua tukisaidiana enzi hizo halafu anakuja kuwa mtu wa kuniibia, kunipotezea documents zangu za mhimu ambazo ni za mhimu sana kwenye kazi zangu.
Kiukweli nimemchukia sana na itanichukua muda kumsamehe na kumsahau. Ipo siku tutakutana tu, na sheria lazima ichukue mkondo wake.