Usia wangu kwa Zitto na washirika wake

Usia wangu kwa Zitto na washirika wake

Zitto must resign kwa sababu alikua anajua kuna kundi lipo linaendesha harakati ki chini chini na kinyume cha taratibu za chama na ye kama kiongozi hakuchukua hatua yoyote ya hao watu kutammbulika na kuchhukuliwa hatua kwa taratibu za chama.
 
SOURCE: VIJANA WANAOMHUJUMU DR. SLAA HAwa HAPA

VIJANA WANAOTUMIWA KUMUHUJUMU DR. SLAA.
Nimesikitishwa sana na vijana wenzangu kutumika kisiasa kiasi cha kuudhalilisha utu wao. Kijana aiitwaye EDO MWAMA LALA, aliyekuwa katibu wa BAVICHA mkoa wa Mbeya na Adam CHEGULANI (diwani wa jiji la mwanza aliyenyang’anywa kadi),wote hawa walifukuzwa Chadema kwa kutokuwa waadilifu. Wapo kwenye kibarua haramu cha kuhakikisha wanawashawishi vijana (hasa BAVICHA)kutoa matamko ya kumhujumu Dr. Slaa kisiasa kupitia vyombo vya habari.

Na wameanza mpango wao na kwa kiasi kikubwa wameanza kufanikiwa, kwani wamefanikiwa kumshawishi katibu wa BAVICHA mkoa wa MWANZA, ndugu SALVATORY SHUKURU MAGAFU kutoa tamko kwenye vyombo vya habari kuomba chama kimfukuze Dr. Slaa chamani. Pia leo hii tayari wanaye kijana mwingine maarufu wa chadema, atakae toa tamko muda wowote kuanzia sasa, kijana huyu wamemlipia hoteli moja maarufu iliyopo hapa jijini na kumpa fedha za kutosha ili atoe tamko kali la kumlaani Dr. Slaa.
Wengine ni: Usiwasahahu Juliana Shonza, Grayson Nyakarungu, Habib Mchange, Ben Saanane… tunawafahamu wote na mtu wanayemtumikia ndani ya Chadema… acha hao kina Nape!!
Kwasbabu lengo sio kulumbana wenyewe kwa wenyewe, wakae tu wakifahamu tunawafahamu na muda ukifika kuhangaika nao tutahangaika nao!!!!@ Alex by SeriaMtoto WikiLiks Tumainiel
Wenye nia ya dhati watabaki… wenye nia ovu watajionesha hadharani na wataungwa mkono na waovu wengine!!
Kwa huu mpango (walioupa jina la MWISHO WA SLAA) ulivyo watajitokeza vijana wengi sana watakaotoa matamko kumlaani Dr. Slaa kwa kutumia mwavuli wa BAVICHA imesema. Kwa akili zao zilivyofupi kama maisha ya funza wanadai wanadhamiria kumuua kabisa Dr. Slaa kisiasa. Na vijana wengi wamekuwa wakishawishika na upumbavu huu wa EDO na ADAM kwasababu ya fedha nyingi wanazopewa baada ya kukamilisha kazi hiyo.
Mpango huu unaofanywa na EDO MWAMALALA na CHAGULANI nyuma yake unafadhiliwa na BERNARD MEMBE, MWIGULU NCHEMBA, NAPE NNAUYE, kwa taarifa nilizo nazo na za kuaminika vijana hawa wanalipwa fedha nyingi sana na viongozi hao waandamizi wa CCM na SERIKALI ambao wamekosa sera na kuamua kuingia kwenye siasa za taarabu.
Kwa Binafsi yangu napenda nitoa tamko rasmi la kulaani kwa nguvu zote vijana wote wa BAVICHA wanaoendekeza njaa mbele na kuweka masilahi ya chama kando kuacha mara moja mchezo huu mchafu. Waache kuwa na akili za Samaki na hatimaye wajitegemee kisiasa. Na niwaombe viongozi hawa wa CCM waache kutumia tatizo la umasikini wa vijana hawa kuwarubuni na kuwatumia wenzao kama mipira ya mapenzi.
Ili kuepuka siasa hizi zisizo na tija kwa jamii niwaombe viongozi wenzangu wa BAVICHA kuachana na kujibizana na hawa wapumbavu, kwani ukijibizana na mpumbavu na wewe pia utakuwa mpumbavu, dhumuni lao tutumie muda mwingi kujibizana nao na tupuuze kujadiliana mambo ya msingi kwa mustakabali wa TAIFA.
CHADEMA tutaendelea kuwa na nguvu na kamwe hatuwezi kupunguzwa nguvu na siasa laini kama hizi. Kinachoshangaza ni kuona anayefadhili ushenzi huu ana ndoto za kuwania Uraisi katika nchi yetu, kweli kwa siasa laini hivi uraisi atauweza?
Imekuwa ni kama tabia yake ya kuwatumia vijana kutimiza malengo yake, kwani ni wazi katika mkutano mkuu wa CCM uliofanyika mkoani Dodoma alituhumiwa na wajumbe wenzie kutumia vijana kusambaza vipeperushii vilivyokuwa vikiwaomba wajumbe wa mkutano huo kumkataa Mwenyekiti wao kwa kisingizio cha kumpunguzia majukumu.
Sasa kashindwa huko anakuja kuingilia siasa za CHADEMA kwa kuwatumia vijana wetu wasiokuwa waadilifu; nimwambie kwa upendo tu kwamba CHADEMA TUKO IMARA KAMA CHUMA.
Na. Alex Nicholaus Thomas MUSHI,
Mjumbe wa Baraza kuu la CHDEMA-Taifa,
Mjumbe wa kamati tendaji BAVICHA-Taifa.
UONGOZI WA CHADEMA MAKAO MAKUU IFANYE UCHUNGUZI WA KINA NA KUCHUKUA HATUA KALI NA MWAFAKA JUU YA WANAOTAJWA HAPO JUU INAONEKANA HAO HAWATUMIWI NA CCM TU INAONEKANA WENYE UCHU WA MADARAKA NDANI YA CHADEMA WANAOTAKA KUGOMBEA URAIS 2015 WANATAKA KUGAWA CHAMA KTK VIPANDE KWA KUMDHOOFISHA DR. SLAA KWANI WENYEWE WANAMUOGOPA, KUWA NDIYE MGOMBEA BORA WA CHADEMA WAKIHOFIA KUWA CHAMA CHAKE KITAMSIMAMISHA TENA 2015 KM ILIVYOKUWA 2010 NA AKATULETEA USHINDI MNONO WANACHADEMA.
BAVICHA PIA IWE MACHO MPAKA SASA SIJASIKIA MATAMKO ILIYOTOLEWA NA BAVICHA KUPINGA NA KUDHIBITI UTOMVU HUU WA NIDHAMU UNAOFANYWA NA VIJANA TENA WENGINE WAJUMBE NA VIONGOZI WA BAVICHA WANAOTUMIWA KM CONDOMS NA WAGOMBEA WA URAIS 2015 KUTOKA KTK VYAMA MBALIMBALI WAKIPEWA HELA CHAFU!!
 
Tatu, Mchange anasema, Ben alikuwa anamtafuta Zitto ili akifadhiri kikundi, wakati mstari wa Nne, wakati Mchange na Mwampamba wakidai kwamba Ben ndiye aliyekuwa analifadhiri kundi la kukihujumu chama na kuwachafua viongozi wa chama. sasa hawa vilaza mbona wanajichanganya kwy kauli zao, mara waseme ben ndio ana fadhili, mara anamtafuta zitto ili afadhili kikundi. sasa tuwaelewe lipi au ndio kuchanganyikiwa? chama chukue maamuzi magumu hawa ni kuwafukuza tu hakuna cha mchange, mtela, shonza, nyakarungu, gwakisa wote ni kuwa sack out.
Ongeza na line ya nne, Ben alikuwa na sumu alikuwa ana mtafuta zitto ili kuumua?
yaani wamechemsha kivibaya, hiyo sumu alikuwa nayo mkononi au aliwajulisha? mbaya zaidi na ushahidi wanao!!! yet they never react on issue, mpaka zitto alipomkana na yeye kujitokeza na kumwaga UZI humu jamvini wenye uzito mkubwa
 
Zitto must resign kwa sababu alikua anajua kuna kundi lipo linaendesha harakati ki chini chini na kinyume cha taratibu za chama na ye kama kiongozi hakuchukua hatua yoyote ya hao watu kutammbulika na kuchhukuliwa hatua kwa taratibu za chama.
Wote: Mchange, Mwampamba na Jualiana ambao tayari wametoa utetezi kwa pamoja wanakiri kumfahamu Zitto vizuri. Kwa hiyo ni dhahiri kwamba walikuwa wanafanya kazi pamoja. Je Zitto kama kiongozi kwanini hakuwakemea kutokana na propaganda ambazo hawa jamaa walikuwa wanaziendesha dhidi ya chama na uongozi wa juu wa chama? Kwani Zitto hakujua kwamba kwa propaganda zile walikuwa wanawapa faida akina Nape na CCM? Ukichunguza kiundani sana, unaweza ona kwamba Zitto hana mapenzi mema na CHADEMA.
 
Hawawezi kuomba radhi hawaaa! Sababu kubwa nasema hawawezi ni kuwa kinachowasumbua sio akili zao. Kinachowasumbua kufanya ushenzi woote huu ni PRIDE. Hivyo until they start dealing with their personal characters - hawaoni kama wamekosea. Hapa shida ni PRIDE na CHARACTER mbovu. Zito namjua kwa kiasi. Ana Akili ambayo haina ushirikiano na moyo wake...... Ni mbishi kiama! Na kijana ni mkatili sijapata kuona!
 
"Lakini zaidi ya yote, Zitto una bahati mbaya sana kwamba watu uliowachagua kukupigia debe au kukubeba kuelekea huko unakotaka kufika ni weupe mno katika uwezo wa kuchambua mambo."

Hapa kuna ukuna ukweli sana!
 
Umemaliza kila kitu, hawa wanatuona watoto, hivi huyo binti ana guts zipi za kumshambulia bosi wake Dr. Slaa hadharani!! Yele yale ya kafulila mwishowe ni kutoa mayowe asamehewe... She is so stupidy...
 
Kwa uchambuzi huu,ni fundisho kwa Zitto kuwa hayuko smart kwa jinsi anavyojikiria kibinafsi binafsi...sijawahi kumkubali huyu jamaa.Washiriki wa Zitto wanapaswa wafunzwe kupayuka kwa mantiki,na si kila upayukaji unakubalika kisiasa na jamii kwa ujumla.
Nimependa na kuukubali chambuzi hii.very fair!!!
 
Tatu, Mchange anasema, Ben alikuwa anamtafuta Zitto ili akifadhiri kikundi, wakati mstari wa Nne, wakati Mchange na Mwampamba wakidai kwamba Ben ndiye aliyekuwa analifadhiri kundi la kukihujumu chama na kuwachafua viongozi wa chama. sasa hawa vilaza mbona wanajichanganya kwy kauli zao, mara waseme ben ndio ana fadhili, mara anamtafuta zitto ili afadhili kikundi. sasa tuwaelewe lipi au ndio kuchanganyikiwa? chama chukue maamuzi magumu hawa ni kuwafukuza tu hakuna cha mchange, mtela, shonza, nyakarungu, gwakisa wote ni kuwa sack out.

Ndugu yangu mbona unaweka mafuta ya petroli kwenye moto? hivi kufukuzana ndio suluhu pekee? naamini CDM sii hiyo unayoisemea hapo ebu kila mmoja wetu afunge macho halafu umfikirie political role model wako and i guess to many of you in this time and at such a difficult time Nelson Mandela will be the obvious choice. If that is a case then go for a reconciliation now na msameheane kwa sifa na ustawi wa CDM CHONDE SANA VIONGOZI WA CDM NISIKIENI MIE MUUMINI WENU BILA KUWA NA KADI YENU.
 
ole wenu wale wote wenye vipaji vya kutapatapa na usaliti ndani ya mioyo yenu kwani umauti wenu utaambatana na dhoruba kali ya nguvu ya umma: Samwel 7:9-11
 
Somo ni kwa vijana wanaoshabikia vyama na wanasiasa bila kujua agenda zote za siri. Mtauzwa bila kujijua, shauri yenu...
 
Ndugu yangu mbona unaweka mafuta ya petroli kwenye moto? hivi kufukuzana ndio suluhu pekee? naamini CDM sii hiyo unayoisemea hapo ebu kila mmoja wetu afunge macho halafu umfikirie political role model wako and i guess to many of you in this time and at such a difficult time Nelson Mandela will be the obvious choice. If that is a case then go for a reconciliation now na msameheane kwa sifa na ustawi wa CDM CHONDE SANA VIONGOZI WA CDM NISIKIENI MIE MUUMINI WENU BILA KUWA NA KADI YENU.
ivi kama mtela kuendelea kumtakana dr slaa siasa hizo badala ya kujibu hoja za ben yeye anamrukia dr. mimi huwa naamini dawa ya moto ni moto tu.
 
Kuna kitu mnaki ruka naona.
Ben anasema walianzisha PM7 ili iwe vuguvugu la mabadiliko kwa vijana nje ya chama. Ila alipoona PM7 inatumika kutukana viongozi ndipo alipo amuia kuhasi na ameongeza kule kuwa kazii ya kuvunja kundi kimya kimya aliianza siku nyingi chini ya ushahuri wa Kitila.
 
Mkuu hongera sana, umefanya tathmini na hitimisho sahihi kabisa.

Nilivyokuwa nasoma hii analysis yako nikahisi kama mimi mwenyewe ndie naandika kwa sababu umefanya hitimisho kama nilivyowaza. Nimekupa like nikatafuta zingine zikakosa nikatamani kungekuwa na like very much!

Huu ndio ukweli
 
Zitto kajiharibia sana!
Nilimwamini ila kimeo sana
 
Hawa jamaa ndio wanaofanya mapango wa MapinduziChadema/BAVICHA?? Kweli?
 
Ndugu yangu mbona unaweka mafuta ya petroli kwenye moto? hivi kufukuzana ndio suluhu pekee? naamini CDM sii hiyo unayoisemea hapo ebu kila mmoja wetu afunge macho halafu umfikirie political role model wako and i guess to many of you in this time and at such a difficult time Nelson Mandela will be the obvious choice. If that is a case then go for a reconciliation now na msameheane kwa sifa na ustawi wa CDM CHONDE SANA VIONGOZI WA CDM NISIKIENI MIE MUUMINI WENU BILA KUWA NA KADI YENU.
Hata mimi siungi mkono mpango wa kufukuzana. Ila yataka moyo kumvumilia mtu kama Mwampamba. Kwa kweli hoja zake zile zina utata mkubwa sana. Bado naona kwamba Mchange anaweza kuonywa na akabadilika na kuwa mwanachama mtiifu kabisa kwa CHADEMA, lakini sina uhakika na Mwampamba, Juliana na wengine ambao bado hawajatoa utetezi wao. Ukisoma hoja za Mchange, unaona kabisa ni mtu anayejutia kosa lake, lakini si hoja za Juliana na Mwampamba.
 
Last edited by a moderator:
Nashangaa hawa vijana tena ambao tunawategemea wajenge chama na kushika nyadhifa mbalimbali kwenye chama tena baadae waweze kushika nyadhifa serikalini badala ya kuheshimu wazee wetu waliowafanya hata watambulike uwepo wao Leo wanakubali kurubunika kwa pesa za kifisadi na kusahau uzalendo!

Wanakubali kutumika kama toilet paper na viongozi wenye uchu wa madaraka!
 
Back
Top Bottom