Kimbunga
Platinum Member
- Oct 4, 2007
- 14,952
- 10,037
CHAMA CHA MAPINDUZI kitakapobadili sera yake ya Muungano wa Serikali Mbili, sera yake mpya itakuwa sera ya Muungano wa Serikali moja. Chama Cha Mapinduzi chenye wanachama wenye akili, na ukweli, na ujasiri, hakiwezi katu kukubali sera ya serikali tatu, kikijua wazi wazi kwamba matokeo na shabaha ya sera hiyo ni kuiua, na kuizika Tanzania. Chama Cha Mapinduzi kikiwa na msimamo huo na wala kisiuonee haya, Tanzania itadumu.
Hakika Nyerere alikuwa na maono. Serikali tatu ni kuua Muungano tu wala hakuna lingine. Serikali moja ndiyo haswaaaaa sawia lakini Zanzibar hawataki?
Huu Muungano unapasua kichwa sasa.
Huku site watu wameng'aka kweli wanataka tatu!!