Tutor B
JF-Expert Member
- Jun 11, 2011
- 9,025
- 6,614
Wapiganaji habari za leo ...
Nimekuwa kwenye kujaribu kila ushauri niupatao hapa Jf kwenye ujasiriamali na namshukuru Mungu kwamba kuna vitu nimevifanyia kazi vikaleta matokeo chanya. Sina budi niwajuze ili nanyi mkafaidi.
1. Kuku wa kienyeji akipatiwa tiba asilia tu kuanzia hatua za awali anakuwa mstahimilivu wa maradhi.
Ifuatayo ni list ya majani nilowapatia vifaranga kwa kipindi cha miezi minne na sasa wana afya njema.
i) Vinasa nguo,
ii) Mchicha
iii) Majani ya Magimbi
iv) Alovera
v) Majani ya mpera
vii) Majani ya rosella - Haya sikuwahi kuyaona yameandikwa popote, niliyatumia kwa sababu yameandikwa sana kwenye tiba za binadamu.
Zaidi ya yote nimeyaona maajabu ya kitunguu maji. Hii ni tiba na kinga ya mafua kwa kuku wa umri wowote. Nakumbuka siku moja mwanangu alinipigia simu na kunieleza kwamba kwenye vifaranga wanapiga chafya sana. Nilipoenda sokoni nilikosa pilipili kichaa, nikataka kwenda kununua fulban (dawa ya mafua kwa kuku) - hela ikapungua. Nikakumbuka kwamba kuna bandiko moja kwenye JF linaongelea maajabu ya kitunguu maji .. basi nikanunua Kg 1 ya vitunguu, nilipofika nyumbani nikachukua vitunguu 3 nikavikatakata na kuninginiza kwenye banda la vifaranga ...
Asubuhi hakuwepo kifaranga hata mmoja alokuwa akipiga chafya. Hivyo nikajua kwamba kuna ukweli kwamba kitunguu maji kinakusanya bakteria walioko hewani.
Naendelea na majaribio mengine .. nitawajuza iwapo kutatokea jambo jingine la kuwashirikisha.
Nimekuwa kwenye kujaribu kila ushauri niupatao hapa Jf kwenye ujasiriamali na namshukuru Mungu kwamba kuna vitu nimevifanyia kazi vikaleta matokeo chanya. Sina budi niwajuze ili nanyi mkafaidi.
1. Kuku wa kienyeji akipatiwa tiba asilia tu kuanzia hatua za awali anakuwa mstahimilivu wa maradhi.
Ifuatayo ni list ya majani nilowapatia vifaranga kwa kipindi cha miezi minne na sasa wana afya njema.
i) Vinasa nguo,
ii) Mchicha
iii) Majani ya Magimbi
iv) Alovera
v) Majani ya mpera
vii) Majani ya rosella - Haya sikuwahi kuyaona yameandikwa popote, niliyatumia kwa sababu yameandikwa sana kwenye tiba za binadamu.
Zaidi ya yote nimeyaona maajabu ya kitunguu maji. Hii ni tiba na kinga ya mafua kwa kuku wa umri wowote. Nakumbuka siku moja mwanangu alinipigia simu na kunieleza kwamba kwenye vifaranga wanapiga chafya sana. Nilipoenda sokoni nilikosa pilipili kichaa, nikataka kwenda kununua fulban (dawa ya mafua kwa kuku) - hela ikapungua. Nikakumbuka kwamba kuna bandiko moja kwenye JF linaongelea maajabu ya kitunguu maji .. basi nikanunua Kg 1 ya vitunguu, nilipofika nyumbani nikachukua vitunguu 3 nikavikatakata na kuninginiza kwenye banda la vifaranga ...
Asubuhi hakuwepo kifaranga hata mmoja alokuwa akipiga chafya. Hivyo nikajua kwamba kuna ukweli kwamba kitunguu maji kinakusanya bakteria walioko hewani.
Naendelea na majaribio mengine .. nitawajuza iwapo kutatokea jambo jingine la kuwashirikisha.