Ushonaji wa Sare msibani na kiwango cha majonzi

Ushonaji wa Sare msibani na kiwango cha majonzi

MURUSI

JF-Expert Member
Joined
Jun 25, 2013
Posts
4,564
Reaction score
8,876
Sare misibani huendana na saa zingine watu kupimwa vipimo na nguo kwenda kushonwa na hata wengine kuulizaa anataka mshono gani na kadhalka.

Huwa najiuliza hivi umeondokewa na mpendwa wako ulie kuwa unampenda mno either mtoto/Mke/Mme/Baba/Mama/Babu/Bibi na kadhalika hivi kweli kwa majonzi yale kuna muda kweli wa kupimana vipimo vya kushona nguo?

kwa huzuni ile nani anakuwa na hamu ya kupimwa kwamba akashonewe sare?

Unless kama kila mtu ana definition yake ya majonzi.
 
Vitu vingine vinashangaza sana, hata sare za Tshirts kwa wafiwa, ni uharibifu wa rasilimali fedha ila basi tu.
 
Wewe endelea kujibana tu, ukifa tunapiga pilau na soda na sare kwa pesa yako!
 
Tatizo hadi misiba tunataka fasheni, badala hizo pesa mngempunguzia mfiwa madeni yatakayojitokeza wakati wa maandalizi ya mazishi.
 
Kuna Mwana - Classmate alifariki. Tukaenda Msibani pale. Akatokea Classmate mmoja ... kajiongeza... kaenda Kariakoo... karudi na fuko la Tshirts kaprint picha ya Marehemu... DOB... DOD... Jina... elfu 20! Kauza weeee... baada ya siku 4 msiba ukasafirishwa mkoani... mwana hata kusafiri hakuonekana!
 
Mimi huwaga nawafananishagaa na wale walioimba mapambio ya msiba wa JK nyerere yaani upo hai wenzio wanakuandalia tenzi za udongoni.

Wakati wengine tukifikwa na misiba hata chupi hattuikumbuki Mara ya mwisho kuibadili ni lini.
 
Sare misibani huendana na saa zingine watu kupimwa vipimo na nguo kwenda kushonwa na hata wengine kuulizaa anataka mshono gani na kadhalka.

Huwa najiuliza hivi umeondokewa na mpendwa wako ulie kuwa unampenda mno either mtoto/Mke/Mme/Baba/Mama/Babu/Bibi na kadhalika hivi kweli kwa majonzi yale kuna muda kweli wa kupimana vipimo vya kushona nguo?

kwa huzuni ile nani anakuwa na hamu ya kupimwa kwamba akashonewe sare?

Unless kama kila mtu ana definition yake ya majonzi.
mtu akifa inabidi mfurahie tu maana kila nafsi itaonja mauti,kizuri zaidi aliyekufa haelewi kuhusu lolote linalokuwa limebakia duniani,yaani anakuwa amepata pumziko la milele,baada ya tabu lawama na misukosuko ya hii dunia ambayo ni tambala bovu!
mimi mtu akifa siwezi kupatwa na huzuni,nitamuonea tu wivu kuwa mwenzangu kajikomboa na amepata pumziko!
 
Sare misibani huendana na saa zingine watu kupimwa vipimo na nguo kwenda kushonwa na hata wengine kuulizaa anataka mshono gani na kadhalka.

Huwa najiuliza hivi umeondokewa na mpendwa wako ulie kuwa unampenda mno either mtoto/Mke/Mme/Baba/Mama/Babu/Bibi na kadhalika hivi kweli kwa majonzi yale kuna muda kweli wa kupimana vipimo vya kushona nguo?

kwa huzuni ile nani anakuwa na hamu ya kupimwa kwamba akashonewe sare?

Unless kama kila mtu ana definition yake ya majonzi.
Ndo hao wafiwa wanapima mkuu japokuwa wana huzuni.

Wao huona kuwa kushona nguo ndio kunawaonesha nafsi zao namna gani wameguswa,ila kwangu ni mila ama tamaduni siyokuwa na mashiko yeyote ile.
 
Sare misibani huendana na saa zingine watu kupimwa vipimo na nguo kwenda kushonwa na hata wengine kuulizaa anataka mshono gani na kadhalka.

Huwa najiuliza hivi umeondokewa na mpendwa wako ulie kuwa unampenda mno either mtoto/Mke/Mme/Baba/Mama/Babu/Bibi na kadhalika hivi kweli kwa majonzi yale kuna muda kweli wa kupimana vipimo vya kushona nguo?

kwa huzuni ile nani anakuwa na hamu ya kupimwa kwamba akashonewe sare?

Unless kama kila mtu ana definition yake ya majonzi.
kuna tabisa hasa ya wasichana kuonyeshana kwamba msiba wao ulifana..lakini hakuna lolote zaidi ya ulimbukeni
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom