Chademakwanza
JF-Expert Member
- Jun 11, 2014
- 6,346
- 1,873
Wameshazoea kula vilivyochacha hao ndio maana wanaonga sana makamanda ili kuwapataWaache hao maCCM yaendelee kuwekeana kiporo hadi kitakapochacha ndio watajua kuwa kiporo hakiliki tena baada ya kuchacha.
Ukishakuwa mtu wa kitu kidogo kama wewe kweli inakua ngumu Kumeza
Ngoja Nimuulize kamanda Thomas Nyahende kama kweli Mwita Mwikabe ndio mwenyekiti wa Kivule, pia aniambie kama huyu ndie alikuwa Raisi wa Daruso nilipokuwa mwaka wa kwanza 2005, kama ni kweli basi tuna under utilize resources, maana jamaa anauwezo mkubwa sana katika uongozi
Kuna watu walikuwa wanasema yeye ndio yule MM3.
Ana sura ya kijambazi.
Wananchi wa Kata ya Kivule wamefurahishwa na ushindi wa Mwenyekiti wa Mtaa wa Kivule Mwita Mwikabe Waitara kutokana na kuanza kutumikia wadhifa huo kwa kishindo kikubwa.
Ni wiki moja sasa kuna ukarabati mkubwa wa barabara za mitaa ya Kivule na ile itokayo Banana kwenda Kivule.
Taarifa zinasema mara baada ya kuapishwa Mwenyekiti wa mtaa huo Mwita Waitara alivamia ofisi za Manispaa kuelezea kero za wananchi wa Kivule kutokana na ubovu mkubwa wa barabara.Waitara alitaka kuona bajeti nzima ya miundombinu ya manispaa.
Kutokana na hali hiyo Waitara aliahidiwa ukarabati wa barabara hiyo na kesho yake ukarabati ukaanza.
Akikagua ukarabati huo Mwita Waitara aliwaeleza wananchi waliomzunguka kwamba hiyo ndiyo CHADEMA na kuwaambia kamwe hatalala huku wananchi wake wakitembea kwa miguu kwa ubovu wa barabara.
Diwani wa Kivule na mbunge wa Ukonga Eugene Mwaiposa wanatoka CCM lakini siku zote wamepuuza kilio cha wananchi kuhusu ubovu wa barabara.
Picha chini ni Mwenyekiti wa mtaa wa Kivule Mwita Mwikabe Waitara
Ana sura ya kijambazi.
Hii sidhani kama itakuwa na ukweli, ngumu sana kukubali hili.
Kuna watu walikuwa wanasema yeye ndio yule MM3.
Hiyo avatar umeivamia ndugu, haiendani na akili ulizo nazo. Akili yako inaendana na ile avatar uloitoa. irudishe sababu unaabisha kichwa ulichokiweka hapo. Huna kitu wewe kichwani hadi kuweka avatar hiyo. Weka ya JK si ya Mwalimu! Ova!Chizi pekee ndiyo anaweza kuiamini hoja kama hii.
Ahsante sana kamanda Molemo kwa taarifa hii nzuri na yenye kuamsha ari.
Nampongeza kwa dhati kabisa Mwenyekiti wangu wa Mtaa wa Kivule kwa namna alivyoanza kazi za kuwatumikia wananchi mara moja baada ya kuchaguliwa kuwaongoza, hakusubiri mkurugenzi ajitafutie posho ya kumuapisha.
Na huu ndio mwelekeo kwa wenyeviti wangu wote wa mitaa tuliyoshinda Jimbo la UKONGA kufanya kazi kwa bidii, kwa kushirikisha wananchi lakini kwa ubunifu wa hali ya juu ili kutimiza matarajio ya waliowachagua.
Kazi yangu ni kuhakikisha kuwa nafuatilia hatua kwa hatua kutendaji na utekelezaji wa majukumu ya kila mwenyekiti wa mtaa anayetokana na Chadema katika jimbo la UKONGA na kuhakikisha kuwa wanatoa huduma bora kwa wananchi.