Ushindi wa CHADEMA Ukonga waleta neema

Ushindi wa CHADEMA Ukonga waleta neema

Molemo

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2010
Posts
14,620
Reaction score
13,361
Wananchi wa Kata ya Kivule wamefurahishwa na ushindi wa Mwenyekiti wa Mtaa wa Kivule Mwita Mwikabe Waitara kutokana na kuanza kutumikia wadhifa huo kwa kishindo kikubwa.

Ni wiki moja sasa kuna ukarabati mkubwa wa barabara za mitaa ya Kivule na ile itokayo Banana kwenda Kivule.

Taarifa zinasema mara baada ya kuapishwa Mwenyekiti wa mtaa huo Mwita Waitara alivamia ofisi za Manispaa kuelezea kero za wananchi wa Kivule kutokana na ubovu mkubwa wa barabara.Waitara alitaka kuona bajeti nzima ya miundombinu ya manispaa.

Kutokana na hali hiyo Waitara aliahidiwa ukarabati wa barabara hiyo na kesho yake ukarabati ukaanza.

Akikagua ukarabati huo Mwita Waitara aliwaeleza wananchi waliomzunguka kwamba hiyo ndiyo CHADEMA na kuwaambia kamwe hatalala huku wananchi wake wakitembea kwa miguu kwa ubovu wa barabara.

Diwani wa Kivule na mbunge wa Ukonga Eugene Mwaiposa wanatoka CCM lakini siku zote wamepuuza kilio cha wananchi kuhusu ubovu wa barabara.

Ahsante sana kamanda Molemo kwa taarifa hii nzuri na yenye kuamsha ari.

Nampongeza kwa dhati kabisa Mwenyekiti wangu wa Mtaa wa Kivule kwa namna alivyoanza kazi za kuwatumikia wananchi mara moja baada ya kuchaguliwa kuwaongoza, hakusubiri mkurugenzi ajitafutie posho ya kumuapisha.

Na huu ndio mwelekeo kwa wenyeviti wangu wote wa mitaa tuliyoshinda Jimbo la UKONGA kufanya kazi kwa bidii, kwa kushirikisha wananchi lakini kwa ubunifu wa hali ya juu ili kutimiza matarajio ya waliowachagua.

Kazi yangu ni kuhakikisha kuwa nafuatilia hatua kwa hatua kutendaji na utekelezaji wa majukumu ya kila mwenyekiti wa mtaa anayetokana na Chadema katika jimbo la UKONGA na kuhakikisha kuwa wanatoa huduma bora kwa wananchi.



Picha chini ni Mwenyekiti wa mtaa wa Kivule Mwita Mwikabe Waitara

Hili ni Jembe kama hautaki unaacha.

0037.jpg
 
Last edited by a moderator:
nawasubiri upande wa pili..team LB7
 
Samahani wakuu!
Huyu Mwita Waitara ndo yule aliyekuwa mbunge wa Tarime baada ya kifo cha Chacha Wangwe na baadaye jimbo kwenda kwa Nyambari Nyangwine?
 
Dah huyu Mwenyekiti anatisha kinoma noma! safi sana!

Hilo ndilo ndio Chama la ukweli CHADEMA. Hongera mwenyekiti, wananchi hawakukosea kukupa kura za kweli na za kutosha

Hakika watanzania wenzangu tujitendee haki na tufanye mabadiliko kwa kupiga kura na kuwachagua vionngozi wenye visheni ya maendeleo

#Mwita_Maranya Big Up
 
Career Path ya Waitara ni zig zag sana, kutoka katibu wa ccm mkoa mpaka mwenyekiti wa mtaa.
 
Samahani wakuu!
Huyu Mwita Waitara ndo yule aliyekuwa mbunge wa Tarime baada ya kifo cha Chacha Wangwe na baadaye jimbo kwenda kwa Nyambari Nyangwine?

sio huyo Mkuu!
 
Back
Top Bottom