MwanaHaki
R I P
- Oct 17, 2006
- 2,401
- 710
Tatizo lenu CCM nikwamba mmekuwa mkidhania kwamba Watanzania wote ni watu bongolala, na kwamb mkitumia nguvu kubwa ya kuwatisha na kuwapiga mkitumia hao Grreen Guards wenu, basi, watanyamaza na kuogopa kwenda kupiga kura.
Nakubali kwamba kwa kiasi kikubwa, mbinu yenu hiyo chafu imefanikiwa huko Arusha. Idadi ya waliopiga kura jana, 14 Julai 2013, ni ndogo ililinganishwa na wale waliojiandikisha. Lakini someni alama za nyakati; licha ya hilo, CHADEMA imeshinda kwa kishindo. Mmeangukia pua, pwaaaaaa! Hayo maumivu!!
Mmeipaka CHADEMA matope, mmetumia rafu zote, huku mkiwa na Jeshi la Polisi, JWTZ, Usalama wa Taifa na Jeshi la Magereza nyuma yenu. Mkaamua kuwaasi wananchi ambao wamewapa dhamana ya kuwa chama tawala.
LAKINI BADO MMESHINDWA!
Hivi mnadhani haya manyanyaso hayana mwisho? Nawasifu sana watu wa Arusha kuwa na msimamo. Wakiamua kufanya jambo, wanalifanya. Si waoga kama sehemu nyingine. Lakini nadhani Watanzania wote sasa watajifunza kutoka kwa wenzao wa Arusha. Hilo kaeni mkijua litafanyika, mtake msitake. Sasa tumefika ukomo wa uvumilivu; dawa yenu iko kwenye sanduku la kura.
CCM bado mna uwezo wa kuirejesha nchi mikononi mwenu, kwa amani, iwapo mtafanya yafuatayo:
1. Tekelezeni ahadi zenu zilizopo kwenye Ilani ya Uchaguzi ya 2010. Mlichoahidi hakijatimia.
2. Elekezeni nguvu zenu kubwa, ambazo mmekuwa mkizitumia kucheza rafu, kwa shughuli za maendeleo.
3. Acheni kutumia vyombo vya dola kinyume cha sheria.
Nahitimisha hapa kwa kuwaponda kidogo, mkae mkielewa jinsi tulivyo na furaha ya ushindi, japokuwa mimi si mwanachama wa chama chochote cha siasa, lakini ushindi huu wa CHADEMA ni ushindi wa WATANZANIA WOTE, kwani haki imetendeka.
Nawaponda kutumia wimbo wa marehemu Mbaraka Mwaruka Mwinshehe, "Jogoo la Shamba", kama ifuatavyo:
Hilooooo CCM!
Ulijidai wewe mbabe sana ooo!
Leo umepigwa na kijana mdogo CHADEMA!
Wewe uliona wapi jogoo la shamba CCM likawika mjini Arusha?
Utampiga nani we CCM?
Je ungepambana nami Mtanzania Mzalendo
Aibu ingekupata CCM!
Nakubali kwamba kwa kiasi kikubwa, mbinu yenu hiyo chafu imefanikiwa huko Arusha. Idadi ya waliopiga kura jana, 14 Julai 2013, ni ndogo ililinganishwa na wale waliojiandikisha. Lakini someni alama za nyakati; licha ya hilo, CHADEMA imeshinda kwa kishindo. Mmeangukia pua, pwaaaaaa! Hayo maumivu!!
Mmeipaka CHADEMA matope, mmetumia rafu zote, huku mkiwa na Jeshi la Polisi, JWTZ, Usalama wa Taifa na Jeshi la Magereza nyuma yenu. Mkaamua kuwaasi wananchi ambao wamewapa dhamana ya kuwa chama tawala.
LAKINI BADO MMESHINDWA!
Hivi mnadhani haya manyanyaso hayana mwisho? Nawasifu sana watu wa Arusha kuwa na msimamo. Wakiamua kufanya jambo, wanalifanya. Si waoga kama sehemu nyingine. Lakini nadhani Watanzania wote sasa watajifunza kutoka kwa wenzao wa Arusha. Hilo kaeni mkijua litafanyika, mtake msitake. Sasa tumefika ukomo wa uvumilivu; dawa yenu iko kwenye sanduku la kura.
CCM bado mna uwezo wa kuirejesha nchi mikononi mwenu, kwa amani, iwapo mtafanya yafuatayo:
1. Tekelezeni ahadi zenu zilizopo kwenye Ilani ya Uchaguzi ya 2010. Mlichoahidi hakijatimia.
2. Elekezeni nguvu zenu kubwa, ambazo mmekuwa mkizitumia kucheza rafu, kwa shughuli za maendeleo.
3. Acheni kutumia vyombo vya dola kinyume cha sheria.
Nahitimisha hapa kwa kuwaponda kidogo, mkae mkielewa jinsi tulivyo na furaha ya ushindi, japokuwa mimi si mwanachama wa chama chochote cha siasa, lakini ushindi huu wa CHADEMA ni ushindi wa WATANZANIA WOTE, kwani haki imetendeka.
Nawaponda kutumia wimbo wa marehemu Mbaraka Mwaruka Mwinshehe, "Jogoo la Shamba", kama ifuatavyo:
Hilooooo CCM!
Ulijidai wewe mbabe sana ooo!
Leo umepigwa na kijana mdogo CHADEMA!
Wewe uliona wapi jogoo la shamba CCM likawika mjini Arusha?
Utampiga nani we CCM?
Je ungepambana nami Mtanzania Mzalendo
Aibu ingekupata CCM!